Tetty
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 26,355
- 21,422
I
INA kuhusu nini??Je chadema wenzako umewashirikisha kwenye hili au unatafuta ugomvi?
INA kuhusu nini??Je chadema wenzako umewashirikisha kwenye hili au unatafuta ugomvi?
Akiwemo raisi na wabunge, si ndiyo; wote ni wanasiasa na hawathaminiki. Kwa maneno mengi unakiri kuwa raisi ni mwana siasa na ana sifa zile zile za mwana siasa kama ilivyo kwa TL!
Shauri yako poteza muda wako kuamini wanasiasa maboya wasio na misimamo kama Tundu. Hamna cha CCM wala CHADEMA. Siasa za sasa nikupigania interest zako tu.Huyu mh.sio tu jasiri na alieamua kujtoa mhanga bali ni mwanasiasa mwenye foresight.
Nakumbuka alituonya kuwa tunapoona vyama vya siasa na wanasiasa wanabanwa,basi na sisi wengine tusidhani tuko salama.
Leo hii ikiwa ni miezi kadhaa tangu Lissu atuonye kila mtu ni shuhuda wa namna kila mmoja wetu anavyoisoma namba.
Leo hii naona baadhi ya vyama vyama vya wafanyakazi vinaanza kutoa matamko,waandishi nao wanaanza kuungana na kutoa matamko ,n.k.Huu ni mwanzo tu wa kutimia kwa maneno ya Tundu Lissu.
Wakati anaongea baadhi walimbeza,baadhi walimuona ana wivu,baadhi walimuona si mzalendo,baadhi walimuona anafanya siasa na baadhi walimdharau na kumpuuza ila nina hakika wengi leo hii wanakubali maneno yake japo hawana ujasiri wa kukiri hadharani lakini wanakiri ndani ya nafsi zao.
Kweli muda kiboko yao.
Sisi wengine si wanafiki tutakusifu angali uhai.
Ungejua jinsi neno Politician lilivyokuwa ni neno negative wala usingelitumia kama kweli ulikuwa na nia ya kumsifia Tundu Lisu, lkn kama ulikuwa na nia ya kusema ukweli basi uko sawa kwamba Tundu Lisu ni Muongo, less intelligent na Fisadi hiyo ndo sifa ya Politician Dunia nzima!
Hakuna Kiongozi intelligent Dunia hii anayependa kuitwa Politician, na ndiyo maana Viongozi wote intelligent Duniani husema ,,I'm not a politician" au ,,Iam not a good politician" unajua kwa nini husema hivyo? Maana yake ni kwamba wao siyo waongo, wajinga na Wapumbavu, hizo ndiyo sifa za politician!
Kwa kifupi Politician yuko kwenye scale ya watu wanaothaminiwa na jamii yuko chini kabisa!
Shauri yako poteza muda wako kuamini wanasiasa maboya wasio na misimamo kama Tundu. Hamna cha CCM wala CHADEMA. Siasa za sasa nikupigania interest zako tu.
Kila siku ya Mungu.Wewe umeshapigania za kwako??
Kwani aloyasema ni uongo?? Kuna yeyote aliyekanusha???Lissu! Lissu yupi? Yule aliyesema Zanzibar ni koloni la Tanganyika? Aliyesema Nyerere amezoea vya kunyonga vya kuchinja hawezi? Hati ya Muungano ya 1964 Karume na Nyerere ni wa kughushi? Anayemwita Rais wa kuchaguliwa dikteta uchwara? Huna habari nyingine za kusema?
huyo Lameck ndio Mwigulu machembeee ahaaaWatu wa Singida Mashariki ndio pekee Tanzania wanaojua maana ya kumchagua Kiongozi. Tundu Antipas Lissu ni zaidi ya mbunge wa Singida. Huyu ni mwakilishi na mtetezi wa watanzania. Ana ujasiri kuliko Maaskofu na Masheik ambao siku zote hutuambia tuseme ukweli daima na tusiogope kumuonya na kumkaripia mtu anayepotoka na kuumiza wengine. Cha ajabu wao ndio wanaongoza kwa uoga wa kukemea waovu na wanaowaumiza wengine.
Tundu Lissu ndio zao halisi la wasomi wa University of Dar es Salaam (UDSM). Hao akina Bana huwa nasita hata kuwaita madaktari maana sioni udaktari wa falsafa ndani yao. Nyerere alitoa wito kwa wasomi kutumia maarifa yao kuwatumikia watanzania. Lissu hana deni katika hili. Nyie akina Lameck hamtaki kujifunza kwa Lissu wa port wenu, kwa nini? Mungu kawapa nafasi kuwatumikia watanzania, mtadaiwa siku moja kwa kutokutimiza wajibu wenu. Hivi Lameck ulitubu ile dhambi ya kufanya Ugaidi dhidi ya binadamu wenzako?
Kama utafuata ile kanuni ya anayefanya zaidi alipwe zaidi bila shaka utakubaliana nami kwamba ule mshahara unaosemekana mkubwa sana anaoweza kuwa analipwa rais basi angetakiwa apewe Tundu Lissu
Kwa maoni yangu sioni kama kuna amejitoa kutetea wanyonge kama Tundu Lissu,huyu anaziwasilisha hasira za Watanzania mbele ya uso wa Tanzania. Jinsi Tundu Lissu anavyozungumza kwa hisia akikemea uonevu na udikteta ndiyo wa Tanzania wanavyozungumza huku sites.
Najua uzalendo wako kwa Tanza ia hauna bei na hata kusema kwangu unastahili upatiwe mshahara wa rais sio kwamba ujazwe mapesa la hasha,bali ni appreciation ya jambo kubwa unalofanyia nchi yako.
Ni zaidi ya jembe mkuu.Lissu ni Jembe
Ni moja ya nne wewe wala huwezi kusumbua watu wenye akili zaoLakini mpigania wanyonge huwa haweki fedha mbele, ukiona mtu anaweka fedha mbele kama malipo ya kazi yake ujue huyo ni shetani na mwizi tu, kama Tundu Lisu!
Hujui hata nchi inako elekea una andika andika tu!Huko ndani siyo kuzuri =Tundu Lissu (lakini lema anamwezi wa tatu hata kumuona ameshindwa)