Tundu Lissu avurugwa.

Bado najiuliza kama anayeandika hapa ni FaizaFoxy ninayemsomaga humu, au aliacha computer bila ku-log out sasa kuna mtu anaitumia!
Kweli huu muungano batili umewagawa CCM kwa wengine wakitetea maslahi ya nchi kama FaizaFoxy na wengine wakitetea matumbo yao kama MwanaDiwani ambaye cheo alichonacho CCM hapo kabla hakikuwepo, hivyo akitumia akili kuhusu huu muungano kwa kudai Tanganyika yetu, huenda cheo chake kikafutiliwa mbali kwenye uso wa sisiem.
So inamlazimu aendelee kutumia tumbo kufikiri kwenye masuala nyeti kama haya.
 
Last edited by a moderator:

Masuala ya Hanga kwa sasa ni ya kifamilia zaidi na wala sio ya serikali kujibu.

Kama utakuwa muelewa, serikali iliyopo madarakani, ina wajibu wa kulinda raia na mali zao, na sio kuwafanya hayo mambo ambayo wewe na watu wa aina yako mnakisia.

Kwa akili ya kawaida tu, hivi kama kweli Nyerere au Karume wangekuwa na nia mbaya dhidi ya Hanga, unadhani wangemuweka hadharani!? Si wangefanya mambo kimya kimya tu..

Ila hadi kumuona Hanga mikononi mwa sheria, basi ujue kwamba suala lake lilikuwa mahakamani na kama CHADEMA au Kambi ya upinzani inataka majibu tofauti na ambayo mtoto wa marehemu ameyatoa, basi bila shaka hawana budi kulithibitishia taifa juu ya madai yao.
 
MwanaDiwani,

Mbona hujagusia hoja za akina Kassim Hanga na wenzake aliowataja Tundu Lissu kwa majina? wako wapi?
Hilo si lingeulizwa Baraza La Wawakilishi, au kule kwa Karume.
Amani si bado yupo.
Lissu hana akili sana na ukimfuata unaonekana sawa naye.
Kwanini haulizi Dedan Kimathi kaburi lake liko wapi?
 
Ndugu, Kama ni swala la maandiko tu, mbona kuna maandiko ya fiction mengi tu.

Hoja hapa siyo maandiko bali mantiki iliyoko ndani ya maandiko halafu cha kushangaza, anayedaiwa kutenda ndiyo tena anaulizwa kama ametenda.
 
Kiukweli Lissu amewashika penyewe,na hapana shaka serikali imeamua kumkodi mtoto bandia wa Hanga ajaribu kufunika uozo.Hovyoo kabisa,
 
Miaka 50 ya Muungano, mnzazibar mmoja ameshakuwa Waziri wa Mambo ya nje (Masele, 2014) safi sana muungano wa kipekee duniani (Mizengo, 2014) udumu milele.
Miaka karibu 240 ya uhuru wa USA kuna majimbo hayajawahi kutoa Rais na husikii wamarekni kuifanya hii ni hoja, Kiongozi achaguliwe kwa uwezo wa kuongoza Taifa sio dini yake au pande gani ya nchi anatokea, siku tukijitenga hawa hawa watatuambia Wanyiramba au wanyakyusa hawajawahi kuongoza nchi kwa hiyo Mbeya wajitenge. na siyo kila mpinga hoja za Lissu ni CCM , wengi hatupendi CCM ila hoja za kizushi hizi we'r sick and tired of them
 
Hilo si lingeulizwa Baraza La Wawakilishi, au kule kwa Karume.
Amani si bado yupo.
Lissu hana akili sana na ukimfuata unaonekana sawa naye.
Kwanini haulizi Dedan Kimathi kaburi lake liko wapi?
Ndugu, swali lako ni zuri sana.

Hiyo hotuba tunafahamu imeandikwa na CUF na akapewa Tundu Lissu aisome kwa sababu yeye kwa sasa ndiyo mwenye "akili kubwa' ndani ya UKAWA.

CUF nia yao ni kupandikiza mbegu za utengano kwa kumshambulia Mwl. Nyerere wakitegemea kushusha heshima yake katika taifa ili hata hoja zao za Muungano zipate wafuasi.
 
Ndugu, tunaelewa vizuri ajenda zao. Kila Kile wanachokifikiria, sisi tunakuwa tumeishakifahamu.

Kwa sasa hawataki hata maelezo ya familia inayohusika, eti wanataka maelezo ya serikali ambayo tayari wameishatoa hukumu.
 
Lisu anasema ukweli!

Taabu kubwa hapa ni CCM kuendeshwa kwa mazoea kwa miaka 50 bila kupenda kuusikia ukweli!
Ndugu, Lissu amesema ukweli upi?.

Unafahamu yaliko mahandaki ambako anadai wamezikwa marehemu?. Kama hufahamu, unaupataje ukweli wa hoja zake bila proof.
 
Hahahahahahaaaaaaa! Serikali haiwezi kupeleka suala hilo mahakamani, tena suala lenyewe linalotokana na TL kwa sababu wanamfahamu kuliko vitanda vyao wanavyovifahamu. Anachokisema TL anakijua na kumpeleka mahakamani ni sawa na kujionyesha utupu njia panda pale Kariakoo. Kama ina majibu na impeleke, lakini wawe tayari kuumbuliwa. Ndo maana wanaongea kwa kujihami wakinyoosha vidole kwa TL na visingizio kibao, oooh anamtukana muasisi...., ooh anachonganisha wananchi na serikali.....ooh flofloflofloflofloflooo! Chezea Tundu Lisu weye.
 
Kwa nini miaka 50 ya muungano waziri mkuu hajatoka zanzibar..raisi usiseme, jaji mkuu usiseme nk nk..
 
Ndugu, Lissu amesema ukweli upi?.

Unafahamu yaliko mahandaki ambako anadai wamezikwa marehemu?. Kama hufahamu, unaupataje ukweli wa hoja zake bila proof.
Tuelezee walivyokufa ili tujue upi uongo pamoja na picha za makaburi yao! otherwise you are bluffing!
 
Kwaiyo hata we ukifa leo watu wa keshoo wasihoji? Kwakuwa wamezaliwa baaada ya wewe kufa?aisee kama ndo una akili hizi basi we zaidi ya Janga
 
 
Kwa nini miaka 50 ya muungano waziri mkuu hajatoka zanzibar..raisi usiseme, jaji mkuu usiseme nk nk..

Salim Ahmed Salim? Anyway, hata hivyo haijaandikwa popote kwamba Waziri Mkuu lazima atoke eneo fulani!
 
Tuelezee walivyokufa ili tujue upi uongo pamoja na picha za makaburi yao! otherwise you are bluffing!
Ndugu, sikufahamu lakini hoja zako ni kama za vijana wa darasa la nne.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…