Tundu A. M. Lissu hapuuziki

Tundu A. M. Lissu hapuuziki

Mbona mimi Lissu ni mmoja wa wabunge ninaowadharau? Akifuatiwa na LEMA?

Kwa upeo wako wakigamba utamdharau ila kwa hoja zake hamna hata mmoja kutoka Lumumba anaweza akaijibu
 
Mbona mimi Lissu ni mmoja wa wabunge ninaowadharau? Akifuatiwa na LEMA?
Inategemea na namna yako ya kufikiri, kuna watu pia walizidharau sana Almasi hadi wakawa wanachezea BAO, walipoletewa goroli za kuchezea bao wakamdharau zaidi mleta goroli kwamba hana akili kwa kuwapa hizo goroli kwa kubadirishana na Almasi. so binafsi sikushangai kwa mtazamo wako huo!
 
Upumbavu wa ccm na wapuuzi wake kama akina mchemba,kinana msomali na huyu asiye na elimu katibu mwenezi wao Nappe mwisho wenu unafika -------!
 
Mkuu hebu tupige kura hapa hapa JF ili tuone kati yako wewe, Lissu na Lema nani ataongoza kwa kudharauliwa.

usipoteze muda wako kwa kumjadili huyo jamaa, we angalia tu ID yake, vitu vingine jiepushe akili yake watu wanatumia kuwekea uchafu.
 
Hakuna hoja ya msingi ambayo Lissu kaitoa kuhusu muungano. Zaidi zaidi ni kushinikiza wanzazibar kujitenga na kuwaaminisha kuwa wao ni koloni la Tanganyika ambayo ilishakufa miaka tele iliyopita kabla hata mwenyewe Lissu hajazaliwa.
 
Mbona mimi Lissu ni mmoja wa wabunge ninaowadharau? Akifuatiwa na LEMA?
Lissu hahitaji kuheshimiwa na wewe intarahamwe ukiwa na wenzio Msomali kinana eti nae mzalendo.Ndgu yenu mwingine Nape na naibu waziri wa fedha Mchemba sijui hata Rais aliwatoa wapi nyinyi ni mashetani ila mwisho wenu umefika!
 
Tangu kwenye kuanza kwa Bunge hili la kumi,Wakili Msomi Tundu A.M.Lissu (Mbunge wa Singida Mashariki-CHADEMA) amekuwa akizungumzia suala la Muungano mara kwa mara. Amekuwa akitoa wito,kwa nyaraka na shahidi mbalimbali, wa kurekebishwa makosa mbalimbali yaliyopo katika Muungano tulionao ili kusonga mbele kama Taifa. Lissu aliendelea kulichambua suala la Muungano kwenye Bunge Maalum la Katiba na hata leo katika Bunge la Bajeti linaloendelea Dodoma.

Kumekuwa na 'mradi' wa wapinzani wake wa kutaka watanzania wampuuze Lissu.Kwamba eti anayoyaongea ni ya kichochezi na hayana maana na msingi kwa Tanzania tuliyonayo. Mimi naamini kuwa Lissu hapuuziki katika hili. Anavyoonekana, amefanya utafiti wa kutosha katika suala hili. Anachokisema popote awapo anakijua,anakiamini na ana uhakika nacho. Hoja hii kwa Lissu sasa imekuwa nyepesi na anaimudu vyema.

Aitwe mchonganishi na mkorofi lakini ataendelea kusema. Kwakuwa anajua anachosema na kumaanisha. Ifike mahali,Serikali itumie hoja za Lissu katika kuuboresha Muungano huu uliopo kwa kurekebisha kasoro anazozitanabaisha Lissu. Kwa vijembe,kejeli,kelele,makofi na vigelegele hoja za Lissu zitabaki na zitaendelea.

Lissu ni akili kubwa.
 
Nimeshawahi kusoma humu JF kuwa Utafiti unasema yakuwa watanzania wana IQ ndogo. lakini nafikiri Lissu ni exceptional kama mtanzania,nafikiri huyu jamaa si matanzania kwasababu IQ yake iko kubwa ukifananisha IQ za watanzania wengi hasa wale wa CCM 🙂
 
Lissu hajatumia busara kutoa maneno ya kashfa kwa waasisi wa Taifa hili na hilo limemshushia heshima sana.....

mkuu naona wewe ni mtu wa ma integral na differentation kwa hiyo usiingie kichwa kichwa kwenye hilo linaosemwa kukashifu waasisi - wengi wanacheza na emotion zetu wakitaka tusifikiri hivyo tusihojo lolote linalohusu waasisi si kwa vile wanawaenzi bali kwa vile hiyo itadisturb status quo.
mfano hili swali alilokuja nalo sasa kuhusu hawa wengine ambaotunafichwa historia yao - je, hapo anawaendelea kuwakashifu waasisi wale wawili?
 
Lissu hajatumia busara kutoa maneno ya kashfa kwa waasisi wa Taifa hili na hilo limemshushia heshima sana.....
Mkuu, neno gani la kejeli alilotoa dhidi ya waasisi wa muungano. Kama kawaita matapeli na waongo na ndivyo ilivyo hayo si matusi wala kejeli. Ni maneno gani katoa?
 
Mbona mimi Lissu ni mmoja wa wabunge ninaowadharau? Akifuatiwa na LEMA?

utakua na akili ya mwendawazimu kumdharau Tundu Lissu. kajipange.....tatizo lenu mumezoea kupewa sifa zisizostahili.
 
Ungeipenda amani ungependa serikali tatu zilizopendekezwa na tume ya katiba ili kuimalisha mungano. vinginevyo serikali mbili ni kuvunja mungano.
Kwakuwa unatumwa na CHADEMA kufanya uchochezi, unadhani kila mtu ni dizaini yako? Wengine sisi ni wazalendo, tunaipenda nchi yetu, na tunaipenda Amani.
 
Tundu lisu kiboko ya mafisadiiii/ma ccm
 
Mkiulizwa ni maneno yepi hayo mnakimbia........bs kwa vile wewe upo hapa ebu tuwekee kumbu kumbu ya hizo kashfa walizopewa waasisi wetu shekhe wangu?

Labda na sisi tutashawishika na kuungana na uvccm na kinana na nape katika kampeni ya kumwadabisha huyu cha utundu lisu
Wakati wa Bunge la Katiba Ndugu Lissu kabla ya kuanza kuchangia hoja ya ama serikali mbili au tatu alisikika akisema "aliyezoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi" aliporekebishwa na mwenyekiti aliyaondoa maneno hayo na kutumia mengine yanayofanana na hayo kimantiki yaani "aliyezoea kuishi kwa uongo hawezi kuwa mkweli". Mara baada ya utangulizi huo aliendelea kunukuu maandiko ya Dr. Mwakyembe, Prof.Shivji kuthibitisha kauli yake ya awali kwa kuonesha ukigeugeu wao kuhusu muundo muafaka wa muungano. Baadaye akanukuu mahojiano ya Mwl. Nyerere huko nyuma mara baada ya muungano aliposema kuwa Zanzibar walikuwa na uhuru wakuchagua ama kuendelea na muungano au la na Tanzania isingewalazimisha kwa mabomu na akalinganisha na maamuzi yaliyofanyika baadaye kumuondoa madarakani Ndg. Aboud Jumbe kama mfano wa ukigeugeu wa Mwalimu. Nadhani hili la mwisho ndio wapinzani wa Lissu wanalitumia kujenga hoja kuwa alimkosea heshima Hayati Baba wa Taifa.
 
Back
Top Bottom