Kweli utaratibu mnaotumia una hali ya kutokuwa na uaminifu, maana nimetuma binti na kaka wakaenda huko walipo hawa watu wakaambiwa watoe 3,000 za form, wametoa hizo hela na wakawaona hao waajiri matokeo yake wanaambiwa kazi zipo lakini mnatakiwa mtoe hela kama 70,000, na mwingine kaambiwa 80,000/ ndipo waunganishwe na waajiri. Jamani hivi kweli mtu hajapata kazi atapata wapi hiyo hela? Na kisha mfano mtu anatoa hiyo hela akienda kwa mwajiri akakuta kazi hakuna je atarudishiwa hela na dalali?
Naomba muache tabia hii ya kuchukuwa kila anayekwenda hapo kumwambia atoe hela 3000/= si vyema na mtu anatoka hajapata kazi na form ni photocopy tu?