Tunaofuatilia mafao NSSF tunateseka

Tunaofuatilia mafao NSSF tunateseka

Bozi

Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
92
Reaction score
144
Unaweza kusema aidha shirika halina hela kulipa mafao au haipo nia ya kulipa watu stahili zao.

Ukifika ofisi za NSSF wafanyakazi wanachojua ni kukupiga tarehe tuu, wakidai kila kitu kinashughulikiwa makao makuu ya NSSF, ukisikia jambo lako linashughulikiwa DSM basi ni kama umeambiwa haulipwi.

Hawajali kabisa kwamba pesa unayoidai ndio mbadala wa mshahara wako baada ya kupoteza kazi, ndio ada ya watoto na ndio chakula cha kwa familia.

Inafika wakati mtu unaanza kuuza samani na asset mbalimbali ulizonazo kulipa ada za watoto huku pesa yako iko NSSF inaudhi sana.

Tuliopoteza ajira Tanzania ni kundi la jamii tuonateseka sana kipindi hiki, inafika wakati hata nauli ya kwenda kufuatilia malipo kidogo inakosekana.

NSSF TULIPENI PESA ZETU, ACHENI KUTUTESA.
 
Pesa zinatekeleza miradi mikubwa, acha tufeee...
 
Serikali imekopa mahela huko na inazifanyia kazi nje na bajeti ya bunge😣😰
 
Magufuli ana roho mbaya sana Shetani afadhali. Pure SADDIST furaha yake kuona wengine wanateseka. Huwezi kabisa kuchezea hela za watu. Yote haya kasababisha yeye.
 
Vumilieni,Nchi inajengwa na Wananchi,wewe ni mmoja wapo.
 
Kama fao la uzazi ni kama wamelifuta, mpaka ulipate huo mlolongo wake ni aibu tupu!! Hawana ushindani tena
 
Unaweza kusema aidha shirika halina hela kulipa mafao au haipo nia ya kulipa watu stahili zao. Ukifika ofisi za NSSF wafanyakazi wanachojua ni kukupiga tarehe tuu, wakidai kila kitu kinashughulikiwa makao makuu ya NSSF, ukisikia jambo lako linashughulikiwa DSM basi ni kama umeambiwa haulipwi.
Hawajali kabisa kwamba pesa unayoidai ndio mbadala wa mshahara wako baada ya kupoteza kazi, ndio ada ya watoto na ndio chakula cha kwa familia.
Inafika wakati mtu unaanza kuuza thamani na asset mbalimbali ulizonazo kulipa ada za watoto huku pesa yako iko NSSF inaudhi sana.
Tuliopoteza ajira Tanzania ni kundi la jamii tuonateseka sana kipindi hiki, inafika wakati hata nauli ya kwenda kufuatilia malipo kidogo inakosekana.
NSSF TULIPENI PESA ZETU, ACHENI KUTUTESA.
Pesa zipo ila tunazitumia kwenye kutembea na dege kubwa Airbus kwenda mapumzikoni.
 
hivi kama hawawezi kulipa si wasikate hela za watu!!yani kikwelii inauzi na inaumiza sana,ila watanzania wengi tunandimi mbili,tulidanganywa tukaandamana kumpongeza.mamaaeeee wacha tuisome wote
 
Wanaojiita Viongozi wa Wanyonge wako wapi kusaidia hili jambo baya sana kwa watu ?
Wapi makondakta wa daladala ?
Wapi maufunguo ya ofisi za umma ?
 
Watu wanateseka sana, NSSF inatesa watu jamani. Kazi huna, umezunguka kila mahali kutafuta kazi umekosa, hakuna kazi, umechoka ukaona acha nifikirie kufanya jambo lingine. Unaomba pesa zako unanyimwa, unasumbuliwa, unazungushwa,familia inateseka, watoto wanakosa shule, unakosa mwelekeo, unazidiwa na msongo, unapata mshtuko na magonjwa mengineyo pia unaweza hata kufa. Walitutungia hii sheria bila kujali kuwa inatuumiza jamani, kweli serikali yetu haioni kuwa tunaumizwa....!!??.
 
Watu wanateseka sana, NSSF inatesa watu jamani. Kazi huna, umezunguka kila mahali kutafuta kazi umekosa, hakuna kazi, umechoka ukaona acha nifikirie kufanya jambo lingine. Unaomba pesa zako unanyimwa, unasumbuliwa, unazungushwa,familia inateseka, watoto wanakosa shule, unakosa mwelekeo, unazidiwa na msongo, unapata mshtuko na magonjwa mengineyo pia unaweza hata kufa. Walitutungia hii sheria bila kujali kuwa inatuumiza jamani, kweli serikali yetu haioni kuwa tunaumizwa....!!??.
Maamuzi magumu yanahitajika
 
Back
Top Bottom