Mpita Njia
Platinum Member
- Mar 3, 2008
- 6,999
- 1,189
Aaaaa Ndallo unaniangusha sasa... na wewe si ni muzee wa mujinbi? sasa unafanyaje biashara kwa kumuachia mtu mzigo kabla ya kupokea mkwanja!!!!!!Kutokana na kichwa cha habari hapo juu ni kua hapa katika maeneo ya mijini kuna hawa mafundi saa wamekuja kugeukia ufundi wa simu na papo hapo nimeona tangazo kwenye banda la fundi saa likisema - TUNANUNUA SIMU MBOVU! chakunishangaza ni kua mimi ninasimu kama 3 hivi za siku nyingi na ni mbovu, basi nikampelekea huyu bwana fundi saa nikamwambia nimeleta simu mbovu si mnanunua kama mlivyojieleza hapa? basi jamaa akazipokea akaniambia ndio wananunua simu mbovu na nimuachie halafu nimrudie baadae, mimi nikajua nakuja kuchukua michuzi japokua kitu chenyewe ni kibovu potelea mbali anipe hela yoyote, niliporudi huyu fundi akaniambia hawezi kununua nikamuuliza kwanini? akanijibu eti simu zenyewe hazifai kwakua ni mbovu mno!!! Jamani naomba kuwasilisha hii hoja kitu kibovu ni kipi?
We acha tu mkulu kumbe hawa jamaa janja yao wanakwanyua baadhi ya spea halafu wanakwambia eti hii haifai kabisa! Basi bwana wameniweza na imekula kwangu.Aaaaa Ndallo unaniangusha sasa... na wewe si ni muzee wa mujinbi? sasa unafanyaje biashara kwa kumuachia mtu mzigo kabla ya kupokea mkwanja!!!!!!
Hiyo kweli wanafanya lakini usithubutu kuwaachia simu yako hata kwa dakika, utalizwaHalafu nimewashtukia wanadai pia wanaFlash simu!
mjini kuna mambo mengi sana kuna sehemu kwa tandale mtogole wameandika tuna nunua chochote.
sasa nilijiuliza wanawezaje kununua chochote wao wanavipeleka wapi hivyo vyovyote? lakini ndio wameshaandika tangazo.
Halafu nilichokuja kushtuka ni pale wakati nampatia hizo simu eti akaniuliza zina ubovu gani wakati yeye kaandika kua wananunua simu mbovu!!!
Mkulu mimi niko karibu na maeneo ya Naazi wewe njoo na wewe utibiwe hawa jamaa wako hapa!
Kweli mjini Shule!
pole sana!
maana ni ujanja wa kizamamnis ana huo aliotumia!