Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Katika moja ya hotuba zake Nyerere alimfananisha mtanzania na bwege mmoja na tumemnukuu alichosema lakini siyo kweli mtanzania ni bwege bali CCM ni pango la wezi wa mali ya umma. Nyerere kwenye hotuba yake alisema yafuatayo na ninamnukuu:-
"Mtanzania ninamfananisha na bwege mmoja ambaye aliokota almasi kubwa lakini chafu chafu. Mjanja mmoja (mwekezaji) alipoona hivyo naye akaokota kichupa akakichonga na kukisafisha na akamfuata bwege (Mtanzania) na kumshawishi wabadilishane. Bwege (Mtanzania) alipoona kichupa mbona kinang'aa akakubali akapewa kichupa tu ili mradi kinang'aa na mwekezaji akaishia na almasi akaenda kuiosha na kuichonga na ikang'aa zaidi ya kile kichupa...bwege alipoona almasi yake imeng'aa akakitupa kile kichupa kikavunjika vunjika na yule mjanja (mwekezaji) akamwambia ukitaka almasi yako itabidi unifidie kwa uwekezaji wangu na gharama ya fidia ni kukuuzia hii almasi kwa bei ya soko.....bwege alipigwa na butwaa....hakuamini alivyotapeliwa." - J.K. NYERERE (Mwisho wa kumnukuu).
Mfano hai.
Mtanzania (bwege) alimwuuzia Kaburu NBC kwa bei ya kutupwa ya dola milioni 300 baadaye bwege akagundua alimwuuzia benki mbili kwa bei ya benki moja. Bwege huyu Mtanzania alipotaka arudishiwe benki ya NMB kaburu (mjanja) akamwambia amerudishie zile dola milioni 300 alizonunulia benki zote mbili ili amwuuzie NMB.
Bwege (Mtanzania) akakubali na hivyo akauziwa benki yake mwenyewe kwa hela aliyouzia benki mbili na hivyo kaburu akawa kajinyakulia NBC bure bila ya kulipa hata senti moja.
Kama hilo halitoshi baada ya miaka nenda rudi kaburu akamwuuzia mwingereza NBC kwa bei ambayo hadi leo haijulikani na kuinyima TRA mapato ya kodi.
Kama hili halitoshi, bwege sasa kauza bandari kwa bei ya kutupwa yaani hata sumni hatalipwa na kuna siku atashtuka kaingizwa mkenge na kwa sababu wako waliohongwa wakachukua hela sasa mwekezaji mwarabu atadai fidia ya mabilioni ya dola sawasawa na bei ya sokoni ya bandari zetu na wengi leo wanaopigia upatu wizi wa mali ya umma watakuwa aidha hawako madarakani au watakuwa wametulizwa kwenye makaburi yao na kuwaachia vizazi vijavyo mgogoro mkubwa wa kimkataba
"Mtanzania ninamfananisha na bwege mmoja ambaye aliokota almasi kubwa lakini chafu chafu. Mjanja mmoja (mwekezaji) alipoona hivyo naye akaokota kichupa akakichonga na kukisafisha na akamfuata bwege (Mtanzania) na kumshawishi wabadilishane. Bwege (Mtanzania) alipoona kichupa mbona kinang'aa akakubali akapewa kichupa tu ili mradi kinang'aa na mwekezaji akaishia na almasi akaenda kuiosha na kuichonga na ikang'aa zaidi ya kile kichupa...bwege alipoona almasi yake imeng'aa akakitupa kile kichupa kikavunjika vunjika na yule mjanja (mwekezaji) akamwambia ukitaka almasi yako itabidi unifidie kwa uwekezaji wangu na gharama ya fidia ni kukuuzia hii almasi kwa bei ya soko.....bwege alipigwa na butwaa....hakuamini alivyotapeliwa." - J.K. NYERERE (Mwisho wa kumnukuu).
Mfano hai.
Mtanzania (bwege) alimwuuzia Kaburu NBC kwa bei ya kutupwa ya dola milioni 300 baadaye bwege akagundua alimwuuzia benki mbili kwa bei ya benki moja. Bwege huyu Mtanzania alipotaka arudishiwe benki ya NMB kaburu (mjanja) akamwambia amerudishie zile dola milioni 300 alizonunulia benki zote mbili ili amwuuzie NMB.
Bwege (Mtanzania) akakubali na hivyo akauziwa benki yake mwenyewe kwa hela aliyouzia benki mbili na hivyo kaburu akawa kajinyakulia NBC bure bila ya kulipa hata senti moja.
Kama hilo halitoshi baada ya miaka nenda rudi kaburu akamwuuzia mwingereza NBC kwa bei ambayo hadi leo haijulikani na kuinyima TRA mapato ya kodi.
Kama hili halitoshi, bwege sasa kauza bandari kwa bei ya kutupwa yaani hata sumni hatalipwa na kuna siku atashtuka kaingizwa mkenge na kwa sababu wako waliohongwa wakachukua hela sasa mwekezaji mwarabu atadai fidia ya mabilioni ya dola sawasawa na bei ya sokoni ya bandari zetu na wengi leo wanaopigia upatu wizi wa mali ya umma watakuwa aidha hawako madarakani au watakuwa wametulizwa kwenye makaburi yao na kuwaachia vizazi vijavyo mgogoro mkubwa wa kimkataba