Tunalaani kitendo hiki, hakivumiliki!

Tunalaani kitendo hiki, hakivumiliki!

Naungana na wengine wote kulaani kitendo hiki. Lakini na tofautiana na wengi wanaosema polisi wachukue hatua. Nina imani kubwa kwamba polisi wenyewe ndiyo wahusika wa jambo hili, na si ajabu ni polisi kadhaa walivaa nguo za kiraia na kuvamia eneo hilo. Naamini kwamba nia yao ilikuwa kumuua ili wasingizie majambazi. Maana ni kawaida yao, tukisema serikali ya CCM inaongozwa kidikteta dhidi ya yeyote anayoipinga tunaonekana wanafiki, wakorofi na tusiyeitakia mema nchi yetu. Ndugu zangu lets not depend on polisi, pale tunapoweza kufanya kazi wenyewe, basi tutekeleze wajibu wetu, manake to some significant measures serikali ilishashindwa siku nyingi katika vita ya kupambana na majambazi, na zaidi sana na yenyewe inashiriki katika ujambazi huo. Sasa ukitaka polisi akusaidie si ni sawa na kumwajiri chui akulindie mbuzi?
 
hivi kweli tanzania imefikia hapa......sitaki kuamini.............
Huamini nini wakati ulimsikia kiranja mkuu wa viranja akisema kuwa atawashughulikia wote wanaomsema vibaya na wengine ameshawashughulikia?
 
Vitu kama hivi vikiachwa viendelee vitabomoa uhuru na ustawi wa taifa letu. Tutajenga taifa la watu wahuni wahuni kama Italy.
 
Naona nchi inaenda Kikagame kagame vile...hatari jamani hakuna atakayesalilmika...nalaani washenzi wa tabia hawa wanaouwa wasomi wetu, wataalamu wetu dhulma yao haitadumu ipo siku Mungu atawaumbuwa.
 
Naungana na Invisible kulaani kwa nguvu zangu zote hizi mbinu chafu zilizopitwa na wakati za kujaribu kunyamazisha sauti ya wananchi. Nataka nimhakikishie Kiranja Mkuu kuwa kachelewa na njama kama hizi hazitafanikiwa kamwe - sana sana ndio anazidi kujiwashia petroli. Najua vitendo kama hivi tutavishuhudia sana tunavyokaribia uchaguzi lakini atambue kuwa safari hii hakuna tena mtelemko, yeye na genge lake wasubiri tu kuwajibishwa kwa kuliweka taifa letu rehani. Kutapatapa kama mfa maji hakutaisadia CCM kwani sikio la kufa halina dawa na kwa kukurupuka namna hii ndio wananchi watakavyozidi kukasirika.

Tunajua the guilty are always afraid kama alivyowahi kuandika mwandishi mashuhuri wa riwaya, James Hadley Chase lakini kama mapema hivi woga tayari umewaingia mpaka wanachanganyikiwa, mbona mbele ya safari watakuwa vichaa kabisa ! Kwa jinsi wanavyotafunana wenyewe kwa wenyewe kama tunavyoshuhudia, hata kipofu sasa anaweza kuhisi uroho na ulafi wao unavyowaendesha. Tokea tupate uhuru sijawahi kuwa na tumaini kama nililonalo hivi sasa - hivi sas natafuta tu popcorn halafu nikae niwe mtazamaji kwenye hii sinema ya bure starring manyang'au ya CCM yakimalizana - then we pick the spoils.
 
Naungana na Invisible kulaani kwa nguvu zangu zote hizi mbinu chafu zilizopitwa na wakati za kujaribu kunyamazisha sauti ya wananchi. Nataka nimhakikishie Kiranja Mkuu kuwa kachelewa na njama kama hizi hazitafanikiwa kamwe - sana sana ndio anazidi kujiwashia petroli. Najua vitendo kama hivi tutavishuhudia sana tunavyokaribia uchaguzi lakini atambue kuwa safari hii hakuna tena mtelemko, yeye na genge lake wasubiri tu kuwajibishwa kwa kuliweka taifa letu rehani. Kutapatapa kama mfa maji hakutaisadia CCM kwani sikio la kufa halina dawa na kwa kukurupuka namna hii ndio wananchi watakavyozidi kukasirika.

Tunajua the guilty are always afraid kama alivyowahi kuandika mwandishi mashuhuri wa riwaya, James Hadley Chase lakini kama mapema hivi woga tayari umewaingia mpaka wanachanganyikiwa, mbona mbele ya safari watakuwa vichaa kabisa ! Kwa jinsi wanavyotafunana wenyewe kwa wenyewe kama tunavyoshuhudia, hata kipofu sasa anaweza kuhisi uroho na ulafi wao unavyowaendesha. Tokea tupate uhuru sijawahi kuwa na tumaini kama nililonalo hivi sasa - hivi sas natafuta tu popcorn halafu nikae niwe mtazamaji kwenye hii sinema ya bure starring manyang'au ya CCM yakimalizana - then we pick the spoils.

Nitashangaa kusikia CCM kuna chagua la Mungu. Chama cha CCM sana kinaongozwa kwa nguvu za shetani.
 
Kubenea kumbuka gazeti lenu lilisema nini kuhusu kiongozi wa usalama wa NCHI!! ohooo... Inasikitisha kuona UMAFIA uko nje nje bongo na serikali haina inalosema. Nalaani pia kitendo hicho...
 
Poleni Vijana; haya ndio madhara inayojenga amani kwa maneno majukwaani; wakati haina mkakati maalumu; RAIS NA MAFISADI WENZAKE GO AWAY;I'M ON THE WAY TO RECLAIM MY COUNTRY. Haijawa covered mahala popote? badala yake wanakava mafisadi; je kuna waandishi wapi ni mafisadi pamoja na vyombo vipi vina sera za kifisadi? why not putting this in Black pen?
 
..............nimekaa chini nikiangalia mbele yangu: nilikotoka ni mbali siwezi kurudi, na ninapokwenda sipajui. Hapa nina njaa na kiu kali sana; sijui nitakula nini na wala sijui nitakunywa nini. Ninahitaji kujilaza nipate usingizi ili nipumzishe mwili na akili lakini kuna baridi kali sana na wala sina chochote cha kujifunika.

Ninabaki kushangaa kuwa imekuwaje nikajikuta mahali hapa panapotishia kuchukua uhai wangu?...............................
 
Pasipo na haki siku zote usalama huwa mashakani. Kwa wale ambao hawakuwahi kujua au kutokea nyanyaso za dola basi waelewe kwamba Tanzania tayari ni nchi ya hatari kwa wananchi wengi; hakuna dhamana (guarantee) ya haki za binadamu. Mali yako inaweza kuchukuliwa na wewe ukawekwa ndani na kuambulia kibano ilihali wenye nafasi zao wameamua. Nilikuwa nikisikia tangu miaka ya 1990 kuwa kuna malodi wakiamua wanatoa mshiko wizara ya mambo ya ndani au polisi ili "mkorofi wao" awekwe ndani na kushughulikiwa ipasavyo - it is common knowledge. Na hatari inazidi kuongezeka kwa kadiri utawala wa nchi unavyozidi kudhibitiwa na mafisadi/mafia. This country will surely explode one day.
 
Kuna baadi ya wanachi na wakazi maeneo fulani miji tofauti tofauti tanzania wakisikia matukio kama yametokea kwa kina Kubenea, wakufunzi wa vyuo viongozi wanafurahi.

Sio kuwa wananchi wanafurahia kitendo ila wanafurahi sababu wanahisi labda wahusika wanaweza kuamka usingizini sababu maafa yamewakumba wanaosikika.

Naungana kukemea sio tu tukio hili la kuvamia nyumba ya kubenea bali matukio yote yanayofanana na hayo.

Nahisi jeshi letu la polisi linaitaji kumegewa % fulani ya bajeti ya JWTZ. Tanzania ina real problem kwenye policing kuliko kwenye military.
 
Hivi yule Sheikh wao aliposema hakutakuwa na uchaguzi mwaka huu, mbona kama naanza kuona dalili za kukwamisha uchaguzi kwa makusudi?.
Maana kama watu hawatakuwa huru kutoa maoni yao ni dhahiri kuwa hakutafanyika kampeni zilizo salama na huenda tukapoteza contestants muhimu sana, na kulazimika mchakato wa kutafuta mgombea/wagombea kuanza upya na uchaguzi kuahirishwa.
 
Hawa majambazi pamoja na kuiba mabilioni ya fedha za wavuja jasho wanataka kuwa CIA na kutengeza elimination squads. Wanatakiwa wakumbuke tu kuwa kila nafsi itaonja mauti na madhila yote wanayoyasababisha watayalipa na riba.
 
haya wale wanaopinga kuwa prof. mwakyusa na yule polisi wa kike wameuwawa na CCM watasemaje? maana walikuwa wanasema Baadhi yetu humu tunatoa hukumu kabla ya mahakama. Kutaka kumuua Kubenea inathibitisha kuwa uongozi uliyopo sasa serikalini ni chinja chinja
Kweli nimeamini ukweli huwezi kuuficha kamwe ana kama ukiuficha na kuuzika utachipua na kumea tena KIGUMU CHAMA CHA MAFISADI NINGUMU FIKRA ZA MWENYEKITI WA MAFISADI NINGUMU
 
mtu unakuwa mkimbizi kwenye nchi yako mwenyewe? this is real bad, wako wapi wakina mama wanaojua kulia na kuomboleza waiombee nchi yetu? maana naona Mungu keshaghairi na amani imepotea kabisa.
babu yangu aliwahi niambia kuwa Tz now ni kama shamba lenye nyasi zilizokauka, siku likitiwa moto linalipuka lote. siombei tufike huko but where are we going?
 
mmh.. hata maneno miye yamenitoka na huwa sina kawaida ya kuishiwa maneno. Na mimi nalaani vile vile.
Tutalaaani sana mwaka huu, lakini suluhisho ni kubadilisha utawala. Huu wa sasa Lowassa et al washauweka mfukoni. Na kwa tukio la leo utasikia polisi wakipiga blah blah tu hakuna kitakachofanyika
 
TANGAZO TOKA WIZARA YA MAMBO YA NDANI
Tanzania si salama tena na kila mkaaji raia/mwenyeji anapaswa kujilinda mwenyewe, kwani kwasasa geshi la polisi linawalinda baadhi tu ya wagombea wa CCM. Hivyo basi raia na wageni toka nje ya nchi ni jukumu lenu kujilinda wenyewe. Jeshi la polisi/UT na hata JWTZ halitahusika na lolote kwasasa na wala lisilaumiwe. Kubenea na wenzako ambao hamko kwenye pay-roll ya Mafisi-maji, no Mafisadi Kaeni chonjo.
MSEMAJI WA WIZARA
 
tena laana hii iwashukie CCM na serikali yake, maana hawa ndiyo wadhamini wakuu
wa uhuni na uvinjifu wa amani na ujambazi wa kuvamia watu na kuwaua,
hii ni tabia yao hawa tangu asili, Mungu awalaani tena awashushie pigo la
kuwataarifu kuwa hapendezewi na mambo yao ya kifirauni na kighafidhuna wayafanyayo
 
Hao walifahamu fika kuwa kubenea amehama eneo hilo ndio maana walikwenda kutesa watu,wanavunga tuu kwani hao jamaa wanajua kila litendekalo!
 
Back
Top Bottom