Tunajadili CHADEMA, tunapitisha muswada wa katiba

Sungurampole

JF-Expert Member
Nov 17, 2007
984
205
Hivi hii ni sawa?

Nafikiri wote tunajua umuhimu wa jambo kama muswada wa kupata katiba kujadiliwa kwa umakini na wabunge na mwisho kupitishwa.

Kwa wote waliosikiliza bunge letu kwa siku za karibuni wakati mjadala huu unaendelea tunajiuliza hivi mjadala ulitosha kuupitisha?

Tunajua Chadema na NCCR walitoka nje, je, hii ilihalalisha kupiga tu juu juu na kupitisha?

Sana nimesikia kila nayesimama analalamika kuhusu kutoa Chadema, anapiga vijembe halafu anaunga hoja. Wako wachache waliobakiza dakika chache za kutoa maoni kidogo kuhusu muswada.

Hakuna anayegusa hata hoja moja ya kambi ya upinzani ni kweli kuwa waliona yote hayafia ?

Hivi tutaarjie nini bungeni bila wabunge wa upinzani?
 
Back
Top Bottom