assuredly4
JF-Expert Member
- Nov 7, 2011
- 1,216
- 220
Asante 3squere kwa thread yako!
Hatuna budi kujifunza kuwapa credit wanaostahili credit, na kuwatia moyo kutoa michango yao kwa jamii. Mchango wa Kakobe, unahitajika sana, katika kuikomboa nchi hii!
Ni ukweli ulio dhahiri, kwamba, bila elimu ya uraia aliyoitoa Kakobe, siku chache kabla ya Uchaguzi Mkuu 2010; CCM walikwisha kumpiga bao Dr wa ukweli, Dr Slaa, kwa sakata lile la "mke wa mtu", walilolishupalia kwenye vyombo vyao vya habari. Elimu ya uraia aliyoitoa Kakobe katika TV, kwa somo, "MKRISTO NA UCHAGUZI MKUU", ndiyo iliyomwokoa Dr Slaa! Somo hilo, lilikuwa kama golikipa aliyepangua penati ya hatari! Tukibisha, itakuwa ni arguing, for the sake of argument!
NYONGEZA
Pia hata somo la' RUSHWA ADUI WA HAKI' ambapo Kakobe alitoa mfano kuwa wao waliopokea rushwa wanafananishwa na Kahaba na kiasi walichopokea cha fedha ndio thamani yao hivyo wamemdharau Mungu. Akawasihi watanzania kutubu na kuonesha kumuheshimu Mungu yule aliyewapa rushwa wasimchague, ndiyo maana CCM walikosa kura hata JK hakushinda, yuko madarakani kwa nguvu ya Jeshi, Kama fisadi SHIMBO, aliyemkingia kifua ambaye naye ametoswa baada ya akaunti yake ya Afrika kusini kukutwa ina fedha takribani bilion 3. Elimu yake ya uaraia Chama cha MAgamba haitausahhau milele
Kakobe Baba Askofu, tunakuomba usituache, tunakuomba mwaka 2015 utupatie tena elimu ya uaria ili tuyaondoe magamba na chama cha magamba