Tunachogombania ni Urithi Wetu! - Ilani ya Maskini

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Wameutwaa urithi wetu wakagawana;

Urithi huo waliogawana wamemegeana vipande vipande na kurithishana wao na watoto wao! Urithi wa taifa letu umekuwa wa kwao peke yao na sisi wengine tumeachiwa tugombanie nyumba iliyotupu ambacho hati miliki yake wao wanayo!

Mgongano unaondelea sasa kwa watu wenye maono madogo ni mgongano wa watu! Watu hao wanaona kinachoendelea sasa ni kati ya Mengi na Manji, Mengi na Rostam, Dr. Slaa na mafisadi, Mwakyembe na Rostam, n.k Wanayaona yanayoendelea kama mgongano kati ya mtu na mtu. Wenye maono haya wanaangalia nani atashinda; na wapo wanaoombea nani ashinde kwani kwa kushinda kwa mtu huyo kwao ni furaha.

Ukiwa unaangalia kutoka mbali utaona kuwa kinachogombaniwa ni urithi wetu. Mara ya kwanza tuliwanyang'anya watu urithi wa taifa letu tulipotangaza Azimio la Arusha. Tulitaka kuhakikisha kuwa wana na watoto wetu huko mbeleni watakuwa na nafasi sawa ya kumiliki na kufurahia utajiri wa nchi yao. Tulipotangaza Azimio lile tulisema kimsingi kuwa nchi hii ni yetu sote na wale watu ambao hawataki wengine wairithi hawa tunawanyang'anya.

Tukaimba wakati ule "mabepari walia, mabepari walia kukatiwa mirija". Tukajaribu kutoa nafasi sawa kwa kila Mtanzania kupata nafasi ya kunufaika badala ya kuacha utajiri wa nchi hii uwe mikononi mwa kikundi cha watu wachache huku mamilioni ya Watanzania wakiishi kama wahamiaji na wapangaji kwenye nchi yao.

Miaka 40 baadaye, waliokatiwa mirija wamerudi kwa nguvu zaidi; wameichomeka mirija yao siyo kwa Watanzania watu wazima tu bali hadi kwenye vichanga vinyonyavyo! Wanatufyonza kama nzi wa "kizungu" ambao wanamereta kwa rangi ya kijani lakini furaha yao iko katika kufyonza uchafu! Mirija yao ya sasa imeunganishwa na kutengeneza pingiri za unyonyaji!

Wanatunyonya kwenye madini, wanatunyonya kwenye fedha, wanatunyonya kwenye elimu na wanatunyonya bila huruma. Ili kuhakikisha hatusikii maumivu ya mijira yao wanatupiga ganzi ya misaada ya kigeni. Bila misaada ya kigeni tungesikia maumivu ya unyonyaji wao. Hili wanalijua.

Hivyo kila kukicha hukika bakuli zao toka kwa mabwana zao ili wamwagiwe ganzi ya misaada ya kigeni. Tukilala wao wanakuja na kutufyonza mpaka karribu tone la mwisho, tukiamka tunajikuta tumenenepa tena na hatusikii maumivu; kumbe walipotunyonya na kuondoka wakarudi na kutujaza misaada ya kigeni! Wenyewe tunawaona wananenepa na kufura kwa utajiri wetu!

Sasa asitokee mtu kuwahoji au kuwapigia kelele; Asitokee mtu awanyonyesheee kidole; Asitokee mtu kuwaambia mbona mnatunyonya? Mtu huyo atakuwa adui na atashukiwa kama na mwewe wa Tanga na kama kuvamiwa na kundi la nyuki atafukuzwa. Kwa sababu amewahoji.

Sisi wengine tuna uamuzi wa kufanya; aidha tukubali yaishe kuwa nchi hii ni ya kwao na tukae pembeni kuangalia nani kati ya "watu" hawa atashinda au kusimama na kusema yule mwenye kutetea urithi wetu yuko upande wetu. Na huyo naye hatuna mkataba naye wa milele kwani yuko upande wetu kwa kadiri ya kwamba anatetea urithi wetu.

Ndugu zangu tunachogombania siyo Benki Kuu, tunachogombania siyo madini, tunachogombania siyo umiliki wa makampuni au kupata kura. Tunachogombania ni Tanzania gani tunataka kuwarithisha watoto wetu na watoto wa watoto wetu. Tunachogombania ni nchi gani tunataka waikute.

Je, tuwarithishe watoto wetu nchi inayotawaliwa kifisadi?
Je, tuwarithishe watoto wetu Benki Kuu ambayo wizi mkubwa umefanyika na unafanyika?
Je, tuwarithishe watoto wetu nchi inayoongozwa na chama kilicholewa ugimbi wa madaraka na kinakwenda kwa kuyumbayumba kama Pombe Sikali?
Je, tuwarithishe watoto wetu Bunge la wabunge waliogawanyika kwa mujibu wa maslahi ya matumbo yao wakitunga sheria za kuuchilia urithi huo kwa bei ya chee?
Je, tuwarithishe watoto wetu mchakato mbovu wa uchaguzi unaochangia kuwachagua wale wale waliotunyonya?
Je, tuwarithishe watoto wetu mfumo mbovu wa elimu ambapo kwa kadiri unavyokwenda juu ndivyo kupasi kunavyoshuka? Angalia wanaopasi kwenye Mtihani wa Bodi ya Wahasibu na mitihani mingine!
Je, tuwaritishe watoto wetu nchi ambayo madini yake yamewekwa chini ya makampuni ya kigeni kama Barrick na kutaka kubadilisha mikataba hiyo inatubidi tuwabembeleze wao?
Je, tuwarithishe nchi yenye viongozi wasiothubutu kutenda lakini wakiwa mahiri wa maneno na mikwara?

Mimi nasema hapana! Ninasema inatosha. Tutawarithisha watoto wetu taifa tulitakalo, taifa lenye nafasi sawa kwa wote na lenye kutawala kwa misingi ya sheria (siyo maneno ya sheria). Tutawarithisha watoto wetu taifa ambalo ndani yake hakuna bwana na mtwana; taifa ambalo Mtanzania mmoja hamnyonyi mwingine kwa sababu tu ya umaskini wake!

Wanaofurahia mgongano wa watu hawa, waendelee kufurahia; lakini tukumbuke kuwa tunachogombania ni kikubwa kuliko Mengi, ni kikubwa kuliko Manji, ni kikubwa kuliko Rostam ni kikubwa kuliko Jeetu Patel na kwa hakika ni kikubwa kuliko Kikwete na wapambe wake! Tunachogombania ni urithi wetu.

Na huo hatuwaachii watu wachache watugawie. Hivyo basi: Tumedhamiria yafuatayo:
 
Nice piece! Ni vyema kuyapigia kelele haya. Lakini kuna haja ya sisi ambayo tunayaona haya kujikita kwenye siasa za nchini kwenu.
Itakuwa vyema kama baadhi yetu humu ndani tukajitokeza kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi ujao. Tutumie uelewa wetu kuleta msukumo wa mabadiliko.
 
Mkijiji hii safi sana, ikiwezekana itoke katika Cheche la wiki hii, nitajitahidi kwa kadri nitakavo barikiwa kuisambaza kama njugu. Iwafikie watu wengi zaidi na zaidi, ina mguso wa kipekee sana,

For sure tunagombea urithi wetu na wanetu wajukuu, vitukuu na vilembwe zetu! Hatuwezi kaa pembeni tuwe watazamaji nchi yetu inatafunwa na kugawiwa kama peremende, wa kiwira wana jichukulia, wakuchota kupitia DOWANS, DEEP GREEN, etc. alimradi kila mtu anaanzisha kachoteo kake na kulala mbele, Nooo.. it is enough!
 
Nice piece! Ni vyema kuyapigia kelele haya. Lakini kuna haja ya sisi ambayo tunayaona haya kujikita kwenye siasa za nchini kwenu.
Itakuwa vyema kama baadhi yetu humu ndani tukajitokeza kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi ujao. Tutumie uelewa wetu kuleta msukumo wa mabadiliko.

Naungana nawe kusupport mtazamo wa Mkjj.

Shida yangu ipo hapo kwenye proposal yako kuwa baadhi (yetu) tukagombee uongozi! Nadhani humu kuna watu wa kila aina kwa hiyo ukifanya statistical prediction utaona tukigombea tutaishia palepale - mkusnyiko wa wasafi na mafisadi - kama ilivyo sasa tu. Sisemi usigombee, gombea lakini ujue kuwa na mafisadi nao watagombea na baadhi watashinda!

Mimi nadhani kubwa ni kila mwenye nia njema na nchi yetu ajaribu popote alipo kujitofautisha na mafisadi kwa ufahari kabisa na tukubali kukumbana na magumu lakini tuwe focused. Pia tuwe tayari hata kwa hatua ya pili ya kuukataa huu unyonyaji kwa vitendo - maandamano, kuandika, kuchangia kwenye forums mbalimbali nk. Na nadhani ni lazima tujipe time frame ili tusijejikuta tunasema tu. Kila mtu aanze kuhubiri uzalendo kuanzia nyumbani, mahali pa kazi, mahali popote. Tutafika.

Haya malumbano ya wakubwa ni hatua nzuri. Joto linazidi kupanda, nyoka wanatoka mapangoni. Sasa tupambane nao mpaka tuwashinde!
 
Naungana nawe kusupport mtazamo wa Mkjj.

Shida yangu ipo hapo kwenye proposal yako kuwa baadhi (yetu) tukagombee uongozi! Nadhani humu kuna watu wa kila aina kwa hiyo ukifanya statistical prediction utaona tukigombea tutaishia palepale - mkusnyiko wa wasafi na mafisadi - kama ilivyo sasa tu. Sisemi usigombee, gombea lakini ujue kuwa na mafisadi nao watagombea na baadhi watashinda!

Mimi nadhani kubwa ni kila mwenye nia njema na nchi yetu ajaribu popote alipo kujitofautisha na mafisadi kwa ufahari kabisa na tukubali kukumbana na magumu lakini tuwe focused. Pia tuwe tayari hata kwa hatua ya pili ya kuukataa huu unyonyaji kwa vitendo - maandamano, kuandika, kuchangia kwenye forums mbalimbali nk. Na nadhani ni lazima tujipe time frame ili tusijejikuta tunasema tu. Kila mtu aanze kuhubiri uzalendo kuanzia nyumbani, mahali pa kazi, mahali popote. Tutafika.

Haya malumbano ya wakubwa ni hatua nzuri. Joto linazidi kupanda, nyoka wanatoka mapangoni. Sasa tupambane nao mpaka tuwashinde!
Njia zote mbili zinaweza kutumika kwa pamoja, ,wenye kuelemisha umma sawa, mwenye kugombea sawa
 
boycott makampuni yenye mahusiano na mafisadi? Kama tulivyofanya dhidi ya makampuni ya Afrika kusini wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi?
 
Petitions/Collect signatures with demands to the government - (e.g prosecution of those implicated/suspected of wrong doing (- Dowans,EPA,etc etc)
 
Nadhani nitaulizwa swali la kipuuzi kabisa, ama swali ambalo wengi mnamajibu nalo, ili kuendeleza mjadala huu wa uporwaji!

Tunaposema tumeporwa, kwa mtanzania wa kawaida kitu ambacho ukimwambia ameporwa akakuelewa ni kipi! Ni wapi ambapo kunahisia za pomoja juu wa matatizo ya watanzania. Kwa mfano, tunapoongelea ufisadi kwa mwananchi wa tanzania unamgusa vipi katika ngazi binafsi? Kwahakika hisira ya ufisadi kwa msomi na mkulima ni tofauti, vile vile kwa walionacho na maskini ni tofauti. Lakini hawa wote wanaweza wakawanachukia ufisadi na wanataka kuupinga, swali hapa je, ingawa hawa watu wanatofauti hizo kinachowaunganisha ni nini? Nachotaka kuelewa hapa ni jinsi gani tunaweza kuongelea ufisadi kwa lugha mbalimbali ili tupata muunganiko mkubwa wa wananchi tofauti.

Ukiangalia hotuba ya Martin Luther King ya I have a dream the central thread of his speech is inequalities and the dream of equality, obama speach focused on change to realize the founding principles of equality as stated in katiba yao.

Sisi ni nini?
 
kwa uelewa wangu, katika thread hii nadhani MKJJ anataka sasa tusogee hatua mbele zaidi kuangalia tuchukue hatua gani kama wananchi.Zipo threads nyingi ambapo tumejadili na kuchambua uporaji huu....na huko bado tunaweza kuendelea kujadili..... tusiondoke kwenye lengo la hii thread
I stand to be corrected.
 
kwa uelewa wangu, katika thread hii nadhani MKJJ anataka sasa tusogee hatua mbele zaidi kuangalia tuchukue hatua gani kama wananchi.Zipo threads nyingi ambapo tumejadili na kuchambua uporaji huu....na huko bado tunaweza kuendelea kujadili..... tusiondoke kwenye lengo la hii thread
I stand to be corrected.

i agree with you. In moving forward we need a shared problem of which now is ufisadi, however, we also need to understand different people will have different response to the matter. As you have seen, the focus has been on people instead of national interest as stated by Mwanakijiji.

Now to get people to see national interest beyond individuals, we need to make majority believe we a common problems. Thus far it is good start, of which mwanakijiji uses sentiments words of "Uporwaji na taifa lijalo". These could be key words in having united front!

All i am asking at this point is basically our communication language which will make use share a common problem to move ahead. In moving ahead, we need people to own a problem and to make them see, visualize it and hate it.
 
Tutaanzaje hiyo boycott,Mkuu? Wakati hata maana ya neno hilo fisadi hatujakubaliana? Leo waliotuletea ndege mbovu, vivuko vibovu, vyakula vibovu, wakatuuzia bidhaa hewa, wakauza fukwe zetu, wameuwa mashirika yetu, wakajenga barabara na mashule hewa n.k.

Leo hii, hao hao, nao wanawanyooshea vidole mafisadi! Mpaka hapo tutakapoamka na kuanza kuwashughulikia hao kunguni waliokuwa kwenye nguo zetu, hatutafika mbali. Mpaka hapo tutakapotambua kuwa tuko complicit kwenye huku kutapanya urithi wetu hatutafika mbali. Mpaka hapo tutakapoangaliana wenyewe na kuambiana kuwa yeyote atakaewafungulia mlango wanaotutakia maovu si mwenzetu, hatutafika mbali.

Hakuna atakaetutoa hapa tulipo bali sisi wenyewe. Tukumbuke kuwa piranha ni hatari kuliko papa. Angalau papa anakubakiza mifupa! Tumekuwa nzige katika nchi yetu, bila haya tunakula na kuharibu hata kile ambacho tulipaswa kuwaachia watakaotufuata!


Amandla.........!
 
Mpaka hapo tutakapoamka na kuanza kuwashughulikia hao kunguni waliokuwa kwenye nguo zetu, hatutafika mbali. Mpaka hapo tutakapotambua kuwa tuko complicit kwenye huku kutapanya urithi wetu hatutafika mbali.

Mpaka hapo tutakapoangaliana wenyewe na kuambiana kuwa yeyote atakaewafungulia mlango wanaotutakia maovu si mwenzetu, hatutafika mbali.

Hakuna atakaetutoa hapa tulipo bali sisi wenyewe.


Amandla.........!

- Ndio maana Mzee Mengi ameanza na sisi tunafutia.

FMES!
 
Kumbe toka Dr. Slaa azungumze Mwembe Yanga tulikuwa tunamngoja Mengi ndiyo tufanye kweli? Iko kazi!

Amandla.....
 
Mzee Mwanakijiji,

Kuna pahala mstari umevukwa, waliouvuka wanajificha kama paka, kichwa chini lakini miili yao inaonekana,hapa ndo pa kupeana tahadhari mapema kuwa kushabikia tu vita ambavyo havitowi jawabu sahihi kwa mustakbali wa taifa hili ni kuvuka mstari na kujificha kama paka. tupeane tahadhari na tuambizane ukweli.

waingereza walimwambia Gandhi " we warn you Mr. Gandhi" naye aliwajibu, "we warn each other".

Mkuu, tushtuane nini hasa kinaendelea nchi hii, watu wasitazame mambo kwa jicho la papo kwa papo.
 
Penye ukweli uongo hujitenga.

Ni ngumu CCM kukubali moja kwa moja mambo hayako sawa. Kwa mfano, hii mikataba ambayo wakuu wanaingia sasa inaiuza nchi pasipo shaka yoyote.Unamsamehe mtu asilipe kodi miaka 99? Uliona wapi kama sio TZ tu.

Na sioni kama ni dhambi watu kusema kuna kasoro. Kama mtu anaamua kufunga masikio basi bahati mbaya halazimishwi.

Ila yanayoendelea sasa hayatatufikisha popote kama nchi. Yanavuruga utaifa, yanaleta chuki na kuzorotesha maendeleo.Lazima yakome kwa nguvu zote
 
We have to own this fight; Fundi amesema kitu ambacho kinaukweli lakini pia kinapaswa kututia shime. Kitu ambacho mzee ES alikisema vile vile siku nyingi kuwa viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe..

Viongozi wetu wako madarakani kwa sababu yetu. Hawajawekwa na shetani hapo au kuteremshwa na Mungu (usiamini maneno ya maaskofu). Hawa wako madarakani kwa sababu ni sisi tumewachagua, tukarudia kuwachagua na labda tutawachagua tena. Bado hatujaweza kuhusisha kura yetu na uongozi wao.

I'll argue that jinsi wanavyochaguliwa ndivyo wanavyoongoza. Ndiyo maana niliyaita haya mapambano ya fikra kwa sababu kabla ya kubadilisha kura ni lazima tubadilishe fikra kwanza. Na katika hili tunajitahidi pole pole sana.

Leo hii watu wa Mbagala ambao wanapokea misaada baadaya milipuko hawahusishi yale yaliyotokea na sera ya ulinzi ya JWTZ au suala la usalama chini ya serikali ya CCM. Wizi wa Benki Kuu hauusishwi na utawala wa serikali iliyoko madarakani; miundombinu mibovu ya maji machafu Dar (na mikoa mingine) haiusishwi na viongozi wa manispaa au serikali waliopo. We see problems in parts.. and hence we don't make a connection of the actual causes of the problems.

Mwisho wake tunashughulikia dalili tu za matatizo na siyo vyanzo!
 
boycott makampuni yenye mahusiano na mafisadi? Kama tulivyofanya dhidi ya makampuni ya Afrika kusini wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi?

Mwanakijiji ndivyo tulivyofanya hivyo kweli kwa mujibu wa historia? Mbona De Beers tuliwaachia 50% share kwenye Mwadui Williamson Diamond Mine?
 
Back
Top Bottom