Tuna cha kujifunza kutoka CHADEMA

Tuna cha kujifunza kutoka CHADEMA

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Hata kama ni wapinzani wetu,mazuri yao tutayachukua.Ima kwa kuwaomba au kuyafanya tu na wao wagutuke baadaye. Kwenye chaguzi za CHADEMA zinazoendelea katika Ukumbi wa Mlimani City, CHADEMA inatufunza mambo mbalimbali ya kidemokrasia. Wametulia;wamejipanga na wanapendeza. Kuanzia maandalizi ya nje ya ukumbi;ukumbini na luningani. Na hata fulana na kofia zao. Tutajifunza kwa maboresho yetu.

Kuanzia Baraza la Wazee; BAVICHA na leo hii BAWACHA,CHADEMA wamejipanga na wakapangika. Intelijensia huru imeshindwa kuona mikutano mbalimbali ya kificho nje ya Ukumbi rasmi inayolenga kupanga takrima au mshikemshike wa hapa na pale. Mbabe wa sera na sura huonekana Ukumbini (Ukumbi rasmi wa mikutano). Kambi za wagombea mbalimbali huishia mlangoni ili kuwapa wasio na kambi muda wa kutafakari sera na sura za wagombea wao.

Hadi kufikia leo, hakuna hata mgombea aliyekimbilia kwa waandishi wa habari kulalamikia ukiukwaji wa sheria na kanuni za kichama. Kila mmoja anamuamini aliyeshinda na kuapa kupambana naye kwa hoja uchaguzi ujao. Mipango ya CHADEMA isitutishe wapinzani wao ila itufunze. Tukubali kuchukua angalau utulivu na umeremetaji wa ukumbi na wanaukumbi katika vyama vyetu. CCM yangu isibaki tena nyuma. Ichote mema ya CHADEMA.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Hongera zako tupatupa chama kinaendeshwa kisomi kuna watu wanajua kupanga itifaki,mzee tulia tukutane mwakani utafurahi na roho yako cdm hoyeeeee....
 
Hata kama ni wapinzani wetu,mazuri yao tutayachukua.Ima kwa kuwaomba au kuyafanya tu na wao wagutuke baadaye. Kwenye chaguzi za CHADEMA zinazoendelea katika Ukumbi wa Mlimani City, CHADEMA inatufunza mambo mbalimbali ya kidemokrasia. Wametulia;wamejipanga na wanapendeza. Kuanzia maandalizi ya nje ya ukumbi;ukumbini na luningani. Na hata fulana na kofia zao. Tutajifunza kwa maboresho yetu.

Kuanzia Baraza la Wazee; BAVICHA na leo hii BAWACHA,CHADEMA wamejipanga na wakapangika. Intelijensia huru imeshindwa kuona mikutano mbalimbali ya kificho nje ya Ukumbi rasmi inayolenga kupanga takrima au mshikemshike wa hapa na pale. Mbabe wa sera na sura huonekana Ukumbini (Ukumbi rasmi wa mikutano). Kambi za wagombea mbalimbali huishia mlangoni ili kuwapa wasio na kambi muda wa kutafakari sera na sura za wagombea wao.

Hadi kufikia leo, hakuna hata mgombea aliyekimbilia kwa waandishi wa habari kulalamikia ukiukwaji wa sheria na kanuni za kichama. Kila mmoja anamuamini aliyeshinda na kuapa kupambana naye kwa hoja uchaguzi ujao. Mipango ya CHADEMA isitutishe wapinzani wao ila itufunze. Tukubali kuchukua angalau utulivu na umeremetaji wa ukumbi na wanaukumbi katika vyama vyetu. CCM yangu isibaki tena nyuma. Ichote mema ya CHADEMA.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

mzee tupatupa umeniwahi kuwapa magamba somo,,kiukweli cdm wako vizuri
zile propaganda kuwa cdm bado,,mara wako kihuharakati zaidi,,ZIMEISHA

TUWE WAUNGWANA KUKUBALI VITU
CHADEMA WAMEIVA
 
Umoja ni nguvu mzee tupa tupa....makundi mliyoyaona ndani ya chadema mliyatengeneza nyie wenyewe na leo yamewarudianeni wenyewe sina imani kama chaguzi zenu za ndani zitawaacha salama shekhe

Kama kuna mazuri kwetu ruksa choteni tu kwani hiki ni kisima cha fikra bora na huru
 
Unajua ndugu yangu tumekuwa humu jf kudanganya watu ila mmjionea wenyewe,hongera kwakutambua hili.
 
Angalau wewe umekuwa mzalendo wa kusema ukweli. Hongera.
 
Chadema ina support kubwa sana kutoka watu wenye busara na wasomi..hiyo fursa haipo Kwenye chama chetu Mzee Tupa Tupana Hongera zao...ndo safari yao naona imeiva..sisi tumeishia kubinafsisha chama kwa watu wachache na familia zao..angalia mama salma na wanawe walivokuwa wanamgombania Mh. Membe...so sad...
 
Hata kama ni wapinzani wetu,mazuri yao tutayachukua.Ima kwa kuwaomba au kuyafanya tu na wao wagutuke baadaye. Kwenye chaguzi za CHADEMA zinazoendelea katika Ukumbi wa Mlimani City, CHADEMA inatufunza mambo mbalimbali ya kidemokrasia. Wametulia;wamejipanga na wanapendeza. Kuanzia maandalizi ya nje ya ukumbi;ukumbini na luningani. Na hata fulana na kofia zao. Tutajifunza kwa maboresho yetu.

Kuanzia Baraza la Wazee; BAVICHA na leo hii BAWACHA,CHADEMA wamejipanga na wakapangika. Intelijensia huru imeshindwa kuona mikutano mbalimbali ya kificho nje ya Ukumbi rasmi inayolenga kupanga takrima au mshikemshike wa hapa na pale. Mbabe wa sera na sura huonekana Ukumbini (Ukumbi rasmi wa mikutano). Kambi za wagombea mbalimbali huishia mlangoni ili kuwapa wasio na kambi muda wa kutafakari sera na sura za wagombea wao.

Hadi kufikia leo, hakuna hata mgombea aliyekimbilia kwa waandishi wa habari kulalamikia ukiukwaji wa sheria na kanuni za kichama. Kila mmoja anamuamini aliyeshinda na kuapa kupambana naye kwa hoja uchaguzi ujao. Mipango ya CHADEMA isitutishe wapinzani wao ila itufunze. Tukubali kuchukua angalau utulivu na umeremetaji wa ukumbi na wanaukumbi katika vyama vyetu. CCM yangu isibaki tena nyuma. Ichote mema ya CHADEMA.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Umeshindwa kuficha mapenzi uliyonayo juu ya CHADEMA.
 
Wewe ni Mwana chadema uliye CCM! Ni kweli chadema hawana cha kujifunza kutoka CCM? Ulishawai kuwaona wanasifia hata jambo moja?
Vuta ni kuvute umevutwa hadi chadema!
 
Hiyo yote tisa, kumi ni Jpili mkutano mkuu. Tuko kambini tunauandaa, mwenyekiti wetu aliwaambia tunataka kuinyesha dunia chama hiki ni imara na makini kiasi gani. Karibu sana, Wassira hajathibitisha mpaka tunataka akiri kwa moyo na kinywa chake.
 
Wewe ni Mwana chadema uliye CCM! Ni kweli chadema hawana cha kujifunza kutoka CCM? Ulishawai kuwaona wanasifia hata jambo moja?
Vuta ni kuvute umevutwa hadi chadema!

Acha wivu wewe mbona mmekopi mengi? Kuanzia chopa hadi sasa kina Nape wanavaa magwanda!
 
Wewe ni Mwana chadema uliye CCM! Ni kweli chadema hawana cha kujifunza kutoka CCM? Ulishawai kuwaona wanasifia hata jambo moja?
Vuta ni kuvute umevutwa hadi chadema!

Dikteta wao Mbowe yupo meza kuu hawana uhuru kabisa! Amesema lazima waangalie mgombea eneo analotoka
 
Sijaona cha kujifunza kutoaka chadema zaidi ya ukabila ,ukanda na kufanya vurugu ambazo siyo za lazima.
 
Back
Top Bottom