Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 339
- 677
TUMUOMBEE RAIS AU TUMHURUMIE?
Na Elius Ndabila
0768239284
Juzi Mh Rais akiwa mkoani Kagera alitoa maagizo kwa mkoa wa Dar es salaam juu ya video iliyokuwa mitandaoni ikionyesha moja ya shule iliyopo Ubungo wanafunzi wake wakisomea nje na kukaa chini. Akizungumza kwa uchungu mkubwa Mh Rais aliwaagiza viongozi wa Manispaa ya Ubungo na RC wa Mkoa kushughulikia tatizo hilo haraka.
Baada ya kauli ya Mh Rais, yametolewa maelekezo ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo kwenye moja ya Chombo cha habari ambacho kinajulikana kwa jina la NJOMBE PRESS TV. Mkurugenzi huyo amesema "Awali ya yote niyapokea maelekezo ya Mh r Rais, Sisi tangu tulipoona hiyo clip hatukukaa kimya kila mtu alishangaa kwa sababu ni taarifa ambazo hazikuwahi kufika ofisini kwangu":- Beatrice Dominic Mkurugenzi wa Manisipaa ya Ubungo.
Anasema kila mtu alishangaa kwa kuwa hizo taarifa hazikuwa kufika ofisini. Wakati Mkurugenzi anazungumza hayo mimi nimeifikiria kuwa yaani Mkurugenzi anashangaa! Yaani taarifa hazijafika ofisini? Hivi gari za Wakurugenzi zina kazi gani? Mkurugenzi anataka taarifa zifike ofisini? Nani amfikishie ofisini? Wilaya ya Ubungo kwa ukubwa wake ni ndogo kuliko kata yetu ya Ibaba Wilayani Ileje. Ni Wilaya ambayo Mkurugenzi anaweza kutembelea shule zake zote za msingi na sekondari kwa masaa matatu akamaliza Wilaya nzima. Lakini nimejiuliza Kama Mkurugenzi wa Ubungo, wilaya yenye kila aina ya rasilimali, wilaya ndogo kiasi hiki hawezi kujua changamoto za wilaya yake hadi yeye na wenzake wote WANASHANGAA! Vipi Wilaya ambazo ni kubwa kuliko mkoa wa Dar es salaam wote, Wilaya ambazo hazina rasilimali kama za Ubungo, ambazo tu hata barabara kwa msimu huu wa mvua hali ikoje? Ninazungumza Wilaya kama Namtumbo, Kalambo, Newala, Kiteto, Matela, Makete, Ileje, Chunya n.k huko hali ikoje? Hali ni mbaya. Dar es salaam ndo sura ya nchi kuko hivi, vipi huko kwenu?
Hali hii umenifanya nifikirie kazi ya kumuombea Rais iendelee, lakini wasio weza kuomba waendelee kumhurumia kwani baadhi ya Wasaidizi wake hawamsaidii bali wanamuongeza stress. Badala ya Mh Rais kupambana na ujenzi wa Taifa kwa kushughulikia mambo makubwa, lakini wakati mwingi amekuwa anapambana na mambo ambayo yangesimamiwa na hata mtendaji wa mtaa. Kutokana na uzembe mkubwa wa baadhi ya watu ambao Mh Rais aliwaamini kushindwa kuendana na kasi yake ndiyo maana mara kadhaa tumemuona Mh Rais anafanya kazi za VEO, WEO, DEO, DMO, DED, DC n.k
Watanzania wangejua ni channel ipi Mh Rais anafuatilia na wangeamua kutuma kila mtu clip ya matatizo hasa kwa upande wa Elimu tu kwa kila mtu sehemu alipo Mh Rais angeshaa kuwa hii ni Tanzania au ni Malawi? Mh Rais ukitaka kujua haya undaa kikosi independent cha watu hata 50 kwa nchi nzima ili wazunguke huko mitaani kama mazingira ya baadhi ya shule yanafanana na Tanzania mpya. Yapo maeneo ambayo hali ni mbaya kuliko hata Ubungo, lakini sidhani kama unajua. Zipo Wilaya zenye miti lakini utakuta watoto wanakaa chini.
Kuna tetesi nimesikia baada ya kauli yako ya juzi kuna baadhi ya maeneo toka jana viongozi hawajalala. Hawa unajiuliza wakisubiri Rais atoe tamko? Wao kazi zao ni zipi?
Kila mtu achague upande wake, Kumuombea au kumhurumia kwa kuwa na watu ambao si msaada kwake?
Na Elius Ndabila
0768239284
Juzi Mh Rais akiwa mkoani Kagera alitoa maagizo kwa mkoa wa Dar es salaam juu ya video iliyokuwa mitandaoni ikionyesha moja ya shule iliyopo Ubungo wanafunzi wake wakisomea nje na kukaa chini. Akizungumza kwa uchungu mkubwa Mh Rais aliwaagiza viongozi wa Manispaa ya Ubungo na RC wa Mkoa kushughulikia tatizo hilo haraka.
Baada ya kauli ya Mh Rais, yametolewa maelekezo ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo kwenye moja ya Chombo cha habari ambacho kinajulikana kwa jina la NJOMBE PRESS TV. Mkurugenzi huyo amesema "Awali ya yote niyapokea maelekezo ya Mh r Rais, Sisi tangu tulipoona hiyo clip hatukukaa kimya kila mtu alishangaa kwa sababu ni taarifa ambazo hazikuwahi kufika ofisini kwangu":- Beatrice Dominic Mkurugenzi wa Manisipaa ya Ubungo.
Anasema kila mtu alishangaa kwa kuwa hizo taarifa hazikuwa kufika ofisini. Wakati Mkurugenzi anazungumza hayo mimi nimeifikiria kuwa yaani Mkurugenzi anashangaa! Yaani taarifa hazijafika ofisini? Hivi gari za Wakurugenzi zina kazi gani? Mkurugenzi anataka taarifa zifike ofisini? Nani amfikishie ofisini? Wilaya ya Ubungo kwa ukubwa wake ni ndogo kuliko kata yetu ya Ibaba Wilayani Ileje. Ni Wilaya ambayo Mkurugenzi anaweza kutembelea shule zake zote za msingi na sekondari kwa masaa matatu akamaliza Wilaya nzima. Lakini nimejiuliza Kama Mkurugenzi wa Ubungo, wilaya yenye kila aina ya rasilimali, wilaya ndogo kiasi hiki hawezi kujua changamoto za wilaya yake hadi yeye na wenzake wote WANASHANGAA! Vipi Wilaya ambazo ni kubwa kuliko mkoa wa Dar es salaam wote, Wilaya ambazo hazina rasilimali kama za Ubungo, ambazo tu hata barabara kwa msimu huu wa mvua hali ikoje? Ninazungumza Wilaya kama Namtumbo, Kalambo, Newala, Kiteto, Matela, Makete, Ileje, Chunya n.k huko hali ikoje? Hali ni mbaya. Dar es salaam ndo sura ya nchi kuko hivi, vipi huko kwenu?
Hali hii umenifanya nifikirie kazi ya kumuombea Rais iendelee, lakini wasio weza kuomba waendelee kumhurumia kwani baadhi ya Wasaidizi wake hawamsaidii bali wanamuongeza stress. Badala ya Mh Rais kupambana na ujenzi wa Taifa kwa kushughulikia mambo makubwa, lakini wakati mwingi amekuwa anapambana na mambo ambayo yangesimamiwa na hata mtendaji wa mtaa. Kutokana na uzembe mkubwa wa baadhi ya watu ambao Mh Rais aliwaamini kushindwa kuendana na kasi yake ndiyo maana mara kadhaa tumemuona Mh Rais anafanya kazi za VEO, WEO, DEO, DMO, DED, DC n.k
Watanzania wangejua ni channel ipi Mh Rais anafuatilia na wangeamua kutuma kila mtu clip ya matatizo hasa kwa upande wa Elimu tu kwa kila mtu sehemu alipo Mh Rais angeshaa kuwa hii ni Tanzania au ni Malawi? Mh Rais ukitaka kujua haya undaa kikosi independent cha watu hata 50 kwa nchi nzima ili wazunguke huko mitaani kama mazingira ya baadhi ya shule yanafanana na Tanzania mpya. Yapo maeneo ambayo hali ni mbaya kuliko hata Ubungo, lakini sidhani kama unajua. Zipo Wilaya zenye miti lakini utakuta watoto wanakaa chini.
Kuna tetesi nimesikia baada ya kauli yako ya juzi kuna baadhi ya maeneo toka jana viongozi hawajalala. Hawa unajiuliza wakisubiri Rais atoe tamko? Wao kazi zao ni zipi?
Kila mtu achague upande wake, Kumuombea au kumhurumia kwa kuwa na watu ambao si msaada kwake?