Kwa bahati mbaya hao watalii hawasomi hizo propaganda za ccm dhidi ya Lema, pia ujue hakuna mtalii anayekuja kumuona Lema bali kuona wanyama Serengeti, Manyara, Ngorongoro nk. Sisi tunaoishi kwa kutegemea utalii kwa taarifa yako ndio kada ya watu wenye maisha mazuri hapa Arusha kuliko kada nyingine. Propaganda kama hizi wanaziamini wazee waliojaa umaskini kwa kisingizio cha amani, niwaambie ccm pia mnaruhusiwa kushinda jimbo la arusha ila kwa kura halali vinginevyo kitendo cha nyinyi kulazimisha kulitwaa jimbo la arusha kwa kutumia hila na jeshi kutawafanya kuwa na kesi ya kujibu kwenye mahakama za kimataifa.