Tumshukuru Hayati Magufuli - Rais Samia

Tumshukuru Hayati Magufuli - Rais Samia

Umejichanganya wewe Catholic Goat!
Na hapo umejibu hoja gani zaidi ya kujaza server....

Ngoja nikurudishe kwenye hoja; In the Hindsight haijalishi kama JPM alikuwa sahihi au vinginevyo..., hatari ya kwamba mtu mmoja anaweza kuamulia watu / taasisi na jamii kwa ujumla ni hatari kubwa sana...

Ofcourse lockdown was impossible kwa nchi kama Tanzania watu wangekufa kwa njaa na fujo kutokea..., Ila hatari kubwa zaidi ni Mtawala aliyepo sasa na watawaliwa kuona kwamba ni sahihi kwa mtu mmoja kuweza kuamua issue kama hii pekee; sababu inaweza ikatokea janga kama hili tena tukamsikiliza aliyepo pale juu na sio wataalamu wa hilo jambo.....
 
Kutosimamisha shughuli za kiuchumi, marehemu Magufuli alikuwa sahihi.

Lakini alistahili kuweka mwongozo wa kujikinga na maradhi hayo kwa watu waliokuwa kwenye hatari zaidi, ikiwa ni pamoja na yeye mwenyewe.

Kosa alilofanya ni kuyapuuza maradhi ambayo yalikuwa ni tishio kubwa.
 
Kutosimamisha shughuli za kiuchumi, marehemu Magufuli alikuwa sahihi.

Lakini alistahili kuweka mwongozo wa kujikinga na maradhi hayo kwa watu waliokuwa kwenye hatari zaidi, ikiwa ni pamoja na yeye mwenyewe.

Kosa alilofanya ni kuyapuuza maradhi ambayo yalikuwa ni tishio kubwa.
Aliyapuuza wapi wakati na shule zilifungwa, akawa anawatahadharisha wananchi kutotumia barakoa za misaada isipokuwa kila mtu ashone ya kwake na kufuata taratibu zote za kujikinga na korona semeni ukweli msimsingizie
 
Na hapo umejibu hoja gani zaidi ya kujaza server....

Ngoja nikurudishe kwenye hoja; In the Hindsight haijalishi kama JPM alikuwa sahihi au vinginevyo..., hatari ya kwamba mtu mmoja anaweza kuamulia watu / taasisi na jamii kwa ujumla ni hatari kubwa sana...

Ofcourse lockdown was impossible kwa nchi kama Tanzania watu wangekufa kwa njaa na fujo kutokea..., Ila hatari kubwa zaidi ni Mtawala aliyepo sasa na watawaliwa kuona kwamba ni sahihi kwa mtu mmoja kuweza kuamua issue kama hii pekee; sababu inaweza ikatokea janga kama hili tena tukamsikiliza aliyepo pale juu na sio wataalamu wa hilo jambo.....
Ulivyo punguani wa kiwango cha fisi maji, aliamuaje peke yake wakati alikaa na baraza la mawaziri? Au ulitaka aamue na nani? Au ulitaka aamue na mbwa koko kama wewe ndo uamini kaamua na mtu?

Afu ulivyo na vichogo vinne unasema lockdown was impossible kwa nchi kama Tanzania, kisha unampinga Rais Samia kwa kumsifu Magufuli kutokufanya lockdown!

Ndiomaana nilikuwa napinga nyie vyeti feki kutokulipwa!
 
Kutosimamisha shughuli za kiuchumi, marehemu Magufuli alikuwa sahihi.

Lakini alistahili kuweka mwongozo wa kujikinga na maradhi hayo kwa watu waliokuwa kwenye hatari zaidi, ikiwa ni pamoja na yeye mwenyewe.
Alifanya hivyo. Ila mnajiondoa ufahamu kwa sababu zenu za kutaka kudumaza jamii.

Kinawauma sana wazungu kukataliwa mashauri yao....na hicho ndicho kinawapeleka kusambaza uwongo.
Kosa alilofanya ni kuyapuuza maradhi ambayo yalikuwa ni tishio kubwa.
Hakupuuza maradhi, alitoa tahadhari, alitaka kuona Jamii inatengeneza barakoa zao wenyewe, aliwasii kutumia mbinu zingine badala ya kuwa n a utegemezi wa vifaa kutoka nje, kwa maan nyingine wawe wabunifu katika kutatua matatizo yaliyojitokeza wakati wa Janga.

Hakuwa na kosa lolote lile kutaka madawa ya kinga, madawa ya kupunguza makali ya corona, yabuniwe Tanzania

Kosa kubwa ni la wazungu kutaka kutusokomeza na kila kitu kutoka kwao. Kwa Tanzania yetu hilo liwe mwiko.

Tundu Lissu ndie aliyeanzisha hii kampeni. Yeye na vibaraka vyake ndio waliokuwa wanadai Hayati alipuuza maradhi. Ni waongo wa kushuturiwa, na akemewe kwa nguvu zote kuendeleza kampeni hiyo ya kudumaza.
 
Ulivyo punguani wa kiwango cha fisi maji, aliamuaje peke yake wakati alikaa na baraza la mawaziri? Au ulitaka aamue na nani? Au ulitaka aamue na mbwa koko kama wewe ndo uamini kaamua na mtu?

Afu ulivyo na vichogo vinne unasema lockdown was impossible kwa nchi kama Tanzania, kisha unampinga Rais Samia kwa kumsifu Magufuli kutokufanya lockdown!

Ndiomaana nilikuwa napinga nyie vyeti feki kutokulipwa!
Hivi unajua hata unachoandika au hata huelewi unachoandika Moja kama waliamua wote kwanini asifiwe mmoja ?

Pili wote waliosema kufuata ushauri wa wataalamu walikuwa wana-support lockdown ? Issue kubwa hapa ni kwamba life is priceless huwezi ukapima maisha na kukua au kushuka kwa uchumi...

Kwenye masuala ya Afya uamuzi inabidi utoke kwa wataalamu wa Afya period; hata kama tulitoboa kwenye hili ila haipaswi hii ndio iwe system yaani tufuate ushauri wa mwanasiasa....

Kwahio kwa kiongozi kusifia uvunjaji wa protokali hususan hata kabla hatujajua hatari / athari ya huo uamuzi ni kufanya betting na maisha ya watu
 
Hivi unajua hata unachoandika au hata huelewi unachoandika Moja kama waliamua wote kwanini asifiwe mmoja ?

Pili wote waliosema kufuata ushauri wa wataalamu walikuwa wana-support lockdown ? Issue kubwa hapa ni kwamba life is priceless huwezi ukapima maisha na kukua au kushuka kwa uchumi...

Kwenye masuala ya Afya uamuzi inabidi utoke kwa wataalamu wa Afya period; hata kama tulitoboa kwenye hili ila haipaswi hii ndio iwe system yaani tufuate ushauri wa mwanasiasa....

Kwahio kwa kiongozi kusifia uvunjaji wa protokali hususan hata kabla hatujajua hatari / athari ya huo uamuzi ni kufanya betting na maisha ya watu
Hapa safi ndo umeandika point ya msingi. Umezungumzia suala la wataalamu. Mwanzoni ilikuwa unaandika blabla braza ila hapa umeset good ground.

Safi braza, inapaswa kuwa set with technical principles siyo betting. Nashukuru pia nashukuru kwa uvumilivu wako, you seem to be a good civics-teacher!
 
Aliyapuuza wapi wakati na shule zilifungwa, akawa anawatahadharisha wananchi kutotumia barakoa za misaada isipokuwa kila mtu ashone ya kwake na kufuata taratibu zote za kujikinga na korona semeni ukweli msimsingizie
Yaani nimsingizie marehemu Maguguli ili nipate nini. Uliyoyasema kuwa aliyasema, ni kweli aliyasema lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa aliupuuza huu ugonjwa. Hakuupa uzito mkubwa kwa uhalisia wake.

Fikiria maisha yake binafsi, alikuwa anafanya nini? Aliyokuwa anafanya yalikuwa yanaendana na hayo uliyoyasema? Aliwahi kutamka kuwa corona ni mafua tu. Yule mdudu ni futa tu, likipata joto linayeyuka tu. Siku moja alipokuwa kanisani alipopewa nafasi ya kuwasalimia waumini, akawadhihaki waliovaa barakoa kanisani, specifically akamtaja jaji mstaafu Mihayo kuwa yeye na mkewe wamevaa barakoa mpaka zinawafanya wasitambulike. Akawasifu ambao hawakuvaa barakoa.

Fikiria kuwa, marehemu Rais Magufuli, waliokuwa wamemzunguka, katibu wake mkuu akafariki, Waziri wake wa Fedha akaugua hasa, waziri wake wa masuala ya nje akafariki, na wengine kadhaa kuugua, lakini yeye akaendelea na mikutano yake inayomchanganya na kundi kubwa la watu bila ya tahadhari ya wazi tuliyokuwa tunaiona.

Mimi binafsi siamini kama barakoa zina msaada mkubwa katika kuzuia maambukizi. Lakini naamini njia waliyoichukua Waisrael ilikiwa nzuri zaidi. Yaani kuwa na vituo vingi vya kuoimia ili wenye maambukizi waanze kupata tiba mapema. Wayahudi waligundua kuwa mtu anayeweza kupata matibabu kabla hajaanza kuumwa lakini tayari ana maambukizi, kulikuwa ma uwezekano karibia na zero wa kupoteza maisha.

Marehemu baada ya wanaomzunguka kuugua, alistahili kuanzishiwa matibabu, lakini sijui kama ilifanyika. Kuna watu ambao watu wao wa karibu waliugua, wao hawakuugua, walipopimwa walionekana wana maambukizi, walianzishiwa matibabu kabla ya kuanza kuugua, walipona bila ya kuugua hata kidogo. Na baadhi ninaowafahamu walikuwa above 75 years old.

Kama unaona alichukua jitihada zote, tukubaliane kutokukubaliana.

Lakini tunakubaliana kuwa uamuzi wake wa kutowafungia watu alikuwa sahihi, lakini ilitakiwa kuambatana na juhudi nyingine ili kuwasaidia wale ambao walikuwa kwenye hatari kubwa kama wangeambukizwa.
 
View attachment 2513786

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Tanzania amemshukuru Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kutosimamisha shughuli za kiuchumi wakati wa janga la Covid 19 na kusema hatua hizo zimesaidia uchumi wa Tanzania kutoshuka kwa sana ukilinganisha na Mataifa mengine.

Rais Samia amesema hayo leo wakati akizungumza na Wawakilishi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) na Zanzibar (TAHLIFE) leo February 11,2023 Ikulu Chamwino Dodoma “Dunia imekumbukwa na mambo matatu makubwa, Uviko- 19, miaka miwili Dunia kama ilisimama hakukuwa na uzalishaji viwandani wala shughuli za maendeleo, baada ya maradhi kuondoka Dunia kama imeanza upya, viwanda vimeanza upya, chumi zimeanza kujengwa upya”

“Nataka hapa kwa pamoja tumshukuru Marehemu John Pombe Magufuli yeye alisema sisi hatusimamishi kitu kwasababu hatuna uwezo wa kulisha Watu wote hawa kila Mtu atoke akajitafutie riziki lakini tuchukue tahadhari, kwa maana hiyo uchumi wetu haukushuka sana kama ulivyoshuka kwa wenzetu Nchi za jirani ndio maana hatukutetereka sana”

“Uchumi wetu ulikuwa unakua kwa 7% lakini yalipoingia maradhi tumeshuka mpaka 4% lakini kuna Nchi za jirani walishuka hadi 2% hadi 3% kwahiyo sisi tulikwenda vizuri, kwahiyo Dunia imekumbwa na maradhi, mabadiliko ya Tabia Nchi na sasa sio mabadiliko ya Tabia Nchi ni mabadiliko ya Tabia Dunia”
#MillardAyoUPDATES

huyu mama huyu jamani dah!
 
View attachment 2513786

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Tanzania amemshukuru Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kutosimamisha shughuli za kiuchumi wakati wa janga la Covid 19 na kusema hatua hizo zimesaidia uchumi wa Tanzania kutoshuka kwa sana ukilinganisha na Mataifa mengine.

Rais Samia amesema hayo leo wakati akizungumza na Wawakilishi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) na Zanzibar (TAHLIFE) leo February 11,2023 Ikulu Chamwino Dodoma “Dunia imekumbukwa na mambo matatu makubwa, Uviko- 19, miaka miwili Dunia kama ilisimama hakukuwa na uzalishaji viwandani wala shughuli za maendeleo, baada ya maradhi kuondoka Dunia kama imeanza upya, viwanda vimeanza upya, chumi zimeanza kujengwa upya”

“Nataka hapa kwa pamoja tumshukuru Marehemu John Pombe Magufuli yeye alisema sisi hatusimamishi kitu kwasababu hatuna uwezo wa kulisha Watu wote hawa kila Mtu atoke akajitafutie riziki lakini tuchukue tahadhari, kwa maana hiyo uchumi wetu haukushuka sana kama ulivyoshuka kwa wenzetu Nchi za jirani ndio maana hatukutetereka sana”

“Uchumi wetu ulikuwa unakua kwa 7% lakini yalipoingia maradhi tumeshuka mpaka 4% lakini kuna Nchi za jirani walishuka hadi 2% hadi 3% kwahiyo sisi tulikwenda vizuri, kwahiyo Dunia imekumbwa na maradhi, mabadiliko ya Tabia Nchi na sasa sio mabadiliko ya Tabia Nchi ni mabadiliko ya Tabia Dunia”
#MillardAyoUPDATES
Maneno ya kweli kabisa. Mama ashikilie mtazamo huu na aachane na wapambe ambao wanadhani kumsifia yeye ni lazima wamponde JPM. Anayoyasema Mama kuhusu COVID19 ndio ukweli wenyewe, pamoja na kwamba JPM alikuwa akichekwa kwa maamuzi yake. Linganisha vifo vilivyotokea kati ya Kenya, waliochukua hatua ya kufunga nchi, na sisi tulioiacha wazi, JPM akisema nchi itabakia wazi lakini tahadhari za kinga zichukuliwe na watu tusali. Vifo vya Tanzania havikuwa vingi kama vya Kenya.
Kauli ya Mama ni nzuri na itamsaidia katika uchaguzi ujao akitambua hadharani mazuri ya JPM kuliko wapambe wanaojikita katika kumlaumu JPM tu kwa kila dosari iliyopo nchini. Hatusemi JPM alikuwa malaika. Lakini ni ukweli usiopingika JPM alifanya mazuri mengi tu, zaidi ya mabaya. Hata kumpata Rais mwanamke kulikuwa ni kwa uzuri wa JPM kumchagua Mama kuwa mgombea mwenza. Bila hivyo Mama asingekuwa Rais hii leo.
Tupongeze mazuri yaliyofanyika na hii pekee ndiyo itamfagilia Mama na kuwarudisha kundini washabiki wa JPM ambao ni muhimu sana kwa CCM katika uchaguzi ujao. La sivyo CCM inagawanyika na ushindi kwao utakuwa wa kubahatisha sana wakijitenga wafuasi wa JPM.
 
Aliyapuuza wapi wakati na shule zilifungwa, akawa anawatahadharisha wananchi kutotumia barakoa za misaada isipokuwa kila mtu ashone ya kwake na kufuata taratibu zote za kujikinga na korona semeni ukweli msimsingizie
Pia hata public transport ilikua ni level seat hamna kubanana
 
Na hapo umejibu hoja gani zaidi ya kujaza server....

Ngoja nikurudishe kwenye hoja; In the Hindsight haijalishi kama JPM alikuwa sahihi au vinginevyo..., hatari ya kwamba mtu mmoja anaweza kuamulia watu / taasisi na jamii kwa ujumla ni hatari kubwa sana...

Ofcourse lockdown was impossible kwa nchi kama Tanzania watu wangekufa kwa njaa na fujo kutokea..., Ila hatari kubwa zaidi ni Mtawala aliyepo sasa na watawaliwa kuona kwamba ni sahihi kwa mtu mmoja kuweza kuamua issue kama hii pekee; sababu inaweza ikatokea janga kama hili tena tukamsikiliza aliyepo pale juu na sio wataalamu wa hilo jambo.....
Ulitaka tupige kura? Mbona CHADEMA wKishapiga kura wabunge wao wakatika Bungeni na kina zittokabwe? Uchaguzi uliofuata 2020 wananji wenye hasira wakawanyima kura sasa siyo wabunge tena.
 
Ulitaka tupige kura? Mbona CHADEMA wKishapiga kura wabunge wao wakatika Bungeni na kina zittokabwe? Uchaguzi uliofuata 2020 wananji wenye hasira wakawanyima kura sasa siyo wabunge tena.
Aisee hivi hata umecheki ninaongelea nini narudia tena kujiqoute ulichoniqoute.......
Ngoja nikurudishe kwenye hoja; In the Hindsight haijalishi kama JPM alikuwa sahihi au vinginevyo..., hatari ya kwamba mtu mmoja anaweza kuamulia watu / taasisi na jamii kwa ujumla ni hatari kubwa sana...

Ofcourse lockdown was impossible kwa nchi kama Tanzania watu wangekufa kwa njaa na fujo kutokea..., Ila hatari kubwa zaidi ni Mtawala aliyepo sasa na watawaliwa kuona kwamba ni sahihi kwa mtu mmoja kuweza kuamua issue kama hii pekee; sababu inaweza ikatokea janga kama hili tena tukamsikiliza aliyepo pale juu na sio wataalamu wa hilo jambo.....

Hapo Keyword ni wataalamu..., jamba la hatari na janga ambalo halijulikani sio sahihi kulifanyia siasa au dhihaka ni vema to tread carefully kwa kuwashirikisha wataalama na wataalamu kwenye hili ni watu wa afya.....
 
Back
Top Bottom