tumetoka mbali!...

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,844
barua.jpg

...ushawahi kumbwa na dhahma ya kuitafutia barua marashi kuipulizia, halafu ukakumbana na tabasamu na vicheko ukikatiza mbele ya mashoga zake walosoma 'gazeti' uloandika?

those days boarding school :D!!!!!!!! ...hamna cha sms wala email...ha haa..

...wikiendi hii share nasi experience zako miaka hiyo
 
Yes enzi hizo boarding ni barua tu hamna simu za mkononi. Ukipata barua imetoka kwa bf unajisikia kweli.Ukiandika wewe unapulizia unyunyu wako,nilikuwa napenda seduction perfume baada ya kutumia sana cobra!
ilikuwa lazima nimkumbushie kwenye barua huu msemo
Love start with a smile
Grow with a kiss
and end with tears!
Ukikosa barua,siku ukitoka nje ya shule kama kwenda kuswali/kusali najitumia barua nionekane nakumbukwa..
Kuna siku nikakosea kutuma baruaz, ya mdingi nikamtumia bf halafu ya bf nikamtumia baba,niligundua wakati zimeshawafikia! Huwa sisahau hiki kitu,baruaz mambo ya boarding we acha tu!
 
...
ilikuwa lazima nimkumbushie kwenye barua huu msemo
Love start with a smile
Grow with a kiss
and end with tears!

...ha -ha -haaa! inaonekana BelindaJacob ulikuwa na AUTOGRAPH enzi za primary school,...

mnazikumbuka Autograph jamani? mnazungusha darasani ma best wana sign

nyimbo wanazopenda;
chakula wanachopenda;
(kazi) career unayoipenda;
nk nk....?

kisha unamalizia na Quote! ha ha haaaa...

leo hii mambo ya AUTOGRAPH yamehamishiwa kwenye FACEBOOK, HI5 nk.... tekinolojia bwana!!!
 

...ushawahi kumbwa na dhahma ya kuitafutia barua marashi kuipulizia, halafu ukakumbana na tabasamu na vicheko ukikatiza mbele ya mashoga zake walosoma 'gazeti' uloandika?

those days boarding school :D!!!!!!!! ...hamna cha sms wala email...ha haa..

...wikiendi hii share nasi experience zako miaka hiyo

Yakhe umenikumbusha mbali, hawa wanasemema unyunyu, wengine hatukuwa na uwezo wa kumiliki kobra. Barua ikishaandikwa inachorwa maua kwa kutumia poda nyekundu na nyeupe (tibeti na bint el sudan) zilikuwa zinanukia hizooo. Ama kweli watu wa posta walikuwa na kazi enzi hizo.

Nakumbuka nikiwa form one siku moja jamaa bwenini kwetu alitumiwa nguo iliyovaliwa. Baada ya parcel kufunguliwa bwenini pakawa hapakaliki. Cha kushangaza jamaa wakawa wanaigombania kama mpira wa kona.
 
Ni kweli aise teknolojia imetubadilisha sana. Nakumbuka nilisaini autograph ya mdada mmoja mshkaji wangu...yaani lilikuwa daftari nikabandika na picha..sijui sasa hivi..nikiletewa ile picha na yale niliyoaandika how will I feel!

Life, bana ni safari ya ajabu sana. Ndo maana ni vyema kila sekunde ukaiishi kwa ukamilifu wake. Maana kila kinachotokea katika maisha yako leo..hakitajirudia..
 
...ha -ha -haaa! inaonekana BelindaJacob ulikuwa na AUTOGRAPH enzi za primary school,...

mnazikumbuka Autograph jamani? mnazungusha darasani ma best wana sign

nyimbo wanazopenda;
chakula wanachopenda;
(kazi) career unayoipenda;
nk nk....?

kisha unamalizia na Quote! ha ha haaaa...

leo hii mambo ya AUTOGRAPH yamehamishiwa kwenye FACEBOOK, HI5 nk.... tekinolojia bwana!!!

Yes autography nilikuwa nayo tena kuna moja mpaka leo ninayo,nikiisoma sasa naishia kucheka na kukumbuka enzi hizo.
kweli teknolojia imekuwa sana siku hizi ni mambo ya social networks kama hizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom