Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,755
Nikianza na Muziki,kwa kipindi cha nyuma muziki wa Dansi(ya ukweli) ulikuwa umeshamiri sana nchini kwetu kiasi kwamba enzi hizo redioni ilikuwa ni mwendo wa muziki wa Dansi tu.
Kuna baadhi ya wanamuziki ambao kwangu mimi huwa ni vigumu sana kuwasahau kutokana na mchango wao katika kuufanya muziki wetu (enzi hizo) uwe maarufu. Binafsi siwazungumzii wanamuziki wa miaka ya 60 na 70 bali nawazungumzia wanamuziki wa miaka ya 80 mwanzoni mpaka miaka ya 90 ambao daima walinivutia na abado wananivutia kutokana na uzuri wa miziki yao,wanamuziki hawa kwa sasa ni marehemu,hivyo nimeona ni bora niitumie nafasi hii japo kwa uchache kuwashirikisha katika kuwakumbuka mashujaa wangu hawa wa muziki.
Kila mtu anajua kwamba kuna wanamuziki ambao huwezi kuacha kuwataja mara tu uanzapo kuuzungumzia muziki wa Tanzania,wanamuziki hawa ni kama akina Salum Abdallah,Mbaraka Mwinyshehe Mwaruka,Marijani Rajabu n.k(Mungu awarehemu). Mimi leo nimeguswa kuwakumbuka wanamuziki hawa wafuatao:-
1. Hemed Maneti Ulaya:-Mzee mzima mwenyewe wa Vijana Jazz Air Pambamoto, huyu
mkulu kwa kweli alikuwa ananikosha mnoo kwa utunzi na uimbaji wake kiasi kwamba
alipachikwa jina la Chiriku. Baadhi ya nyimbo(ninazozijua) ninazozipenda mpaka leo ni
kama Maria,Tambiko la Pambamoto,Bujumbura,Penzi haligawanyiki sehemu ya 1 na
ya 2 na nyingine nyingi tu.Huyu bwana alikuwa na kipaji kwa kweli.
2.Eddy Sheggy:- Huyu bwana naye alikuwa na kipaji,ukisikiliza nyimbo zake kama
Milima ya kwetu (akiwa na Super Rainbow), Penzi haligawanyiki, Ogopa Tapeli, Mwisho
wa mwezi nk (akiwa na Vijana Jazz), Nelson Mandela, Shakaza(akiwa na Washirika
Tanzania Stars, wimbo wa Shakaza aliurudia pia alipohamia Bima Lee Orchestra) au
Nyimbo za Baba Jenny na Gondoigwe (akiwa na Bantu Group) uatona ni jinsi gani naye
Alikuwa na kipaji cha kuimba.
3. Jerry Nashon Dudumizi:- Mtaalamu mwingine wa Vijana Jazz ambaye daima mimi
namkumbuka kwa nyimbo zake tamu alizotunga na kuimba akiwa na Vijana Jazz,
nyimbo kama VIP,Shoga,Theresa na nyingine nyingi tu…..
4. Suleiman Mbwembwe:- Huyu namkumbuka kwa nyimbo yake tamu ya Mama Chichi
(akiwa Vijana Jazz) na nyingine nyingi akiwa na Juwata/Ottu Jazz/Msondo Ngoma.
5. Francis(Nassir) Lubua, mtaalamu mwenyewe wa Nginde Ngoma ya Ukae
6.Tino Masinge "Arawa"….Sina la kusema hapa jamani…R.I.P
7. Ali Kishiwa Mhoja "TX Moshi William"…Aaargh,kifo jamani.Ukisikia mtu ana kipaji TX alijaliwa hasa, sina haja ya kutaja kazi yake, inajulikana.
8. Athuman Momba:- Kifaa kingine hiki cha Vijana Jazz na Msondo Ngoma…R.I.P
9. Le supreme Fredy Ndala Kasheba:- Mzee wa ZAITA MUSICA wana ZUKE ZUKE
Muselebende,nani atavishau vibao vyake vitamu kama Marashi ya Pemba,Dezodezo
(Tshala Muana aliununua huu wimbo) ama ule wimbo mtamu wa Kesi ya Khanga
(mama nipe nauli nikamfuate Monica,amekimbilia Zambia na Treni ya mizigo, kisa cha
kukimbia madeni yamemzidi, Doti kumi za Khanga alizokopa hajalipa)….dah
10. Suleiman Mwanyiro "Computer": Mtaalamu huy wa gitaa zito (besi) wa Nginde
11. Kalala Mbwembwe:- Huyu bwana alikuwa Tancut Almas baadaye akaanzisha bendi
ya Ruaha International,namkumbuka kwa nyimbo zake kama Lutandila,Safari n.k
12. Kyanga Songa:- Huyu bwana alikuwa na pacha wake tangu Sambulumaa,Tancut na
baadae Ruaha International
Wakuu kwangu mimi hizi ni Hazina zilizotoweka ghafla tukiwa bado twazihitaji.Tuendelee kuwataja wengine ambao nimewasahau…Sasa hivi muziki wa Dansi Bongo ni kama umejifia tu,hakuna kitu,kila kitu vijana wanakopi muziki wa Kikongo tuuuuuuuuu…..Pa1
Kuna baadhi ya wanamuziki ambao kwangu mimi huwa ni vigumu sana kuwasahau kutokana na mchango wao katika kuufanya muziki wetu (enzi hizo) uwe maarufu. Binafsi siwazungumzii wanamuziki wa miaka ya 60 na 70 bali nawazungumzia wanamuziki wa miaka ya 80 mwanzoni mpaka miaka ya 90 ambao daima walinivutia na abado wananivutia kutokana na uzuri wa miziki yao,wanamuziki hawa kwa sasa ni marehemu,hivyo nimeona ni bora niitumie nafasi hii japo kwa uchache kuwashirikisha katika kuwakumbuka mashujaa wangu hawa wa muziki.
Kila mtu anajua kwamba kuna wanamuziki ambao huwezi kuacha kuwataja mara tu uanzapo kuuzungumzia muziki wa Tanzania,wanamuziki hawa ni kama akina Salum Abdallah,Mbaraka Mwinyshehe Mwaruka,Marijani Rajabu n.k(Mungu awarehemu). Mimi leo nimeguswa kuwakumbuka wanamuziki hawa wafuatao:-
1. Hemed Maneti Ulaya:-Mzee mzima mwenyewe wa Vijana Jazz Air Pambamoto, huyu
mkulu kwa kweli alikuwa ananikosha mnoo kwa utunzi na uimbaji wake kiasi kwamba
alipachikwa jina la Chiriku. Baadhi ya nyimbo(ninazozijua) ninazozipenda mpaka leo ni
kama Maria,Tambiko la Pambamoto,Bujumbura,Penzi haligawanyiki sehemu ya 1 na
ya 2 na nyingine nyingi tu.Huyu bwana alikuwa na kipaji kwa kweli.
2.Eddy Sheggy:- Huyu bwana naye alikuwa na kipaji,ukisikiliza nyimbo zake kama
Milima ya kwetu (akiwa na Super Rainbow), Penzi haligawanyiki, Ogopa Tapeli, Mwisho
wa mwezi nk (akiwa na Vijana Jazz), Nelson Mandela, Shakaza(akiwa na Washirika
Tanzania Stars, wimbo wa Shakaza aliurudia pia alipohamia Bima Lee Orchestra) au
Nyimbo za Baba Jenny na Gondoigwe (akiwa na Bantu Group) uatona ni jinsi gani naye
Alikuwa na kipaji cha kuimba.
3. Jerry Nashon Dudumizi:- Mtaalamu mwingine wa Vijana Jazz ambaye daima mimi
namkumbuka kwa nyimbo zake tamu alizotunga na kuimba akiwa na Vijana Jazz,
nyimbo kama VIP,Shoga,Theresa na nyingine nyingi tu…..
4. Suleiman Mbwembwe:- Huyu namkumbuka kwa nyimbo yake tamu ya Mama Chichi
(akiwa Vijana Jazz) na nyingine nyingi akiwa na Juwata/Ottu Jazz/Msondo Ngoma.
5. Francis(Nassir) Lubua, mtaalamu mwenyewe wa Nginde Ngoma ya Ukae
6.Tino Masinge "Arawa"….Sina la kusema hapa jamani…R.I.P
7. Ali Kishiwa Mhoja "TX Moshi William"…Aaargh,kifo jamani.Ukisikia mtu ana kipaji TX alijaliwa hasa, sina haja ya kutaja kazi yake, inajulikana.
8. Athuman Momba:- Kifaa kingine hiki cha Vijana Jazz na Msondo Ngoma…R.I.P
9. Le supreme Fredy Ndala Kasheba:- Mzee wa ZAITA MUSICA wana ZUKE ZUKE
Muselebende,nani atavishau vibao vyake vitamu kama Marashi ya Pemba,Dezodezo
(Tshala Muana aliununua huu wimbo) ama ule wimbo mtamu wa Kesi ya Khanga
(mama nipe nauli nikamfuate Monica,amekimbilia Zambia na Treni ya mizigo, kisa cha
kukimbia madeni yamemzidi, Doti kumi za Khanga alizokopa hajalipa)….dah
10. Suleiman Mwanyiro "Computer": Mtaalamu huy wa gitaa zito (besi) wa Nginde
11. Kalala Mbwembwe:- Huyu bwana alikuwa Tancut Almas baadaye akaanzisha bendi
ya Ruaha International,namkumbuka kwa nyimbo zake kama Lutandila,Safari n.k
12. Kyanga Songa:- Huyu bwana alikuwa na pacha wake tangu Sambulumaa,Tancut na
baadae Ruaha International
Wakuu kwangu mimi hizi ni Hazina zilizotoweka ghafla tukiwa bado twazihitaji.Tuendelee kuwataja wengine ambao nimewasahau…Sasa hivi muziki wa Dansi Bongo ni kama umejifia tu,hakuna kitu,kila kitu vijana wanakopi muziki wa Kikongo tuuuuuuuuu…..Pa1