Tumeshasema hatuna Corona, mabeberu mnatufuata fuata nini?

Tumeshasema hatuna Corona, mabeberu mnatufuata fuata nini?

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
10,509
Reaction score
16,734
Tanzania tangu mwanzo imekuwa ikifuata tahadhari za kujikinga na corona huku yenyewe ikiziangalia tahadhari hizo kwa umakini sana.

Kwa kiasi kikubwa Tanzania imeibuka shujaa katika vita hivi hata kama bado hakujatolewa tangazo rasmi ya kwisha kwa janga hili.

Hata Trump wa Marekani na mganga wake mkuu wa maradhi ya maambukizi Dkt Fauci jana walitoa tamko la kukoma kuwafungia watu ndani tena kama kinga ya corona.

Kwa msimamo huu Tanzania haiko peke yake japokuwa imekuwa mbele kueleza msimamo wake.La kushangaza ni kuwa kila siku ukifuatilia vyombo vya habari vya nje utakuta hawachoki kutilia shaka maelezo ya Tanzania na kama kwamba wanahamu kusikia watanzania wengi wanakufa kwa corona.

Sisi mitaani na mahospitalini kwetu hatujaiona korona na tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutukinga na janga hili,kwanini mabeberu wanashangilia majanga ya wenzao.
 
Mlijua kuwa hakuna korona kwa vipimo vipi? Vile feki mlivyopimia mapapai
 
Mlijua kuwa hakuna korona kwa vipimo vipi? Vile feki mlivyopimia mapapai
 
Mlijua kuwa hakuna korona kwa vipimo vipi? Vile feki mlivyopimia mapapai

Hata waziri wa elimu juzi aliposema hakuna mwanafunzi au mwana chuo aliyeambukizwa hadi sasa tangia vilivyofunguliwa vifunguliwe hakuna ajuaye takwimu hizo alizipata je.

Labda tuna namna ya kupima kivyetu vyetu.
 
Kwa kweli wanaopaswa kumwomba Mungu na kisha kumshukuru kwa kuwanusuru hatuko peke yetu. Wenzetu wengine hawa hapa:

Bad News For South Africans
Watu 94 wanaotajjwa kufa kwa siku Afrika kusini kwa corona walijulikanaje.Kuna ajabu gani watu 94 kufa kwa siku katika nchi yenye watu zaidi ya mil 50.
 
Watu 94 wanaotajjwa kufa kwa siku Afrika kusini kwa corona walikulikanaje.Kuna ajabu gani watu 94 kufa kwa siku katika nchi yenye watu zaidi ya mil 50.

Inahitaji kubarikiwa kuwa na moyo wa ajabu kweli kweli kuona ni sawa tu kwa watu kufa madhali mfaji si wewe wala anayekuhusu.

Hongera mkuu kwani hicho nacho ni kipaji.
 
Naona mnabadilisha ID lkn mada zake zile zile,endeleni pigeni ramli ................lkn maisha lazima yaendelee.
 
Ila kuna ubabya gani kumshukuru Mungu ikiwa ww unaepinga hili upo hai???
 
Hizo ni propaganda za jiwe corona ipo na inaumiza watanzania kimya kimya.
 
Wacha tuwaimbie hii _wacha waisome namba eeeeh![emoji445][emoji445]wasituzowee kabisa.
 
Ama hakika kwa hili mabeberu sasa wanaonesha upumbavu wao...
 
Wewe ni tabibu au mkunga wa hospitali gani?
 
Beberu jinga sana, wakisaidiana na beberu saidiz tanzania, wanatupangia maisha sisi....mtasema sana this time..na Magu tunamtengenezea zengwe abadili katiba....aendelee kuwa madarakan...mtatutafuta sana....mkileta yenu...tunafanya yetu...to hell
 
Hayo mambo ya Corona bila kuangalia na kumuelekea Mwenyezi Mungu sana basi mataifa tajiri yataporomoka vibaya sana.Hilo raisi Trump aliliona zamani isipokuwa mabeberu walionyuma yake hawamuachii akatoa maamuzi yake kama raisi.Mwenyewe amesema hata iweje hawezi kuvaa barakoa kwanza inaharibu sura wasije mapaparazi wakapata picha yake.
Kuna mataifa ambayo corona kwao ni kama damu na hawataki kusikia kifo.Akifa mtu mmoja tu inakuwa nongwa wanazidi kukaza kamba kuwafungia watu ndani.Wasubiri njaa na maandamano vitakapowaumbua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom