#COVID19 Covid-19: Serikali iache kucheza na akili za Watanzania

Mzalendo39

JF-Expert Member
Apr 17, 2015
882
1,029
Hivi karibuni Serikali ya awamu ya sita imetangaza kuwepo kwa mlipuko wa Corona na kuuarifu umma kuchukua taahadhari ya kujikinga na ugonjwa.

Kinachoshangaza serikari hiyo hiyo inayotangaza kuchukua tahadhari dhidi ya Corona ndiyo inayoongoza kuvunja Taratibu za kujikinga na Corona kwa kuruhusu mikusanyiko.

Mfano:
1. Rais Samia alimpigia Simu Nandy simu akiwa Dodoma kwenye #Nandyfestival ilihali akujua kuwa mkusanyiko huo ni kichocheo cha kusambaa virusi vinavyosababisha #Corona
2. Huko Mtwara jana wamehitimisha Michezo ya #umitashumita na viongozi wakuu wa serikali wakahudhuria na katika video inaonesha uwanja ukiwa umefurika kupita kiasi.
3. Maonyesho ya sabasaba# Unawezaje ukatangaza uwepo wa mlipuko wa Corona na ukaruhusu maonyesho yanayoendelea ya sabasaba.
4. Mechi ya simba na yanga ilitakiwa leo mechi ya simba na yanga ichezwe bila mashabiki kutoka na mlipuko wa wimbi la tatu la Corona, lakini bado Serikali hiyo hiyo inaruhusu mashabiki kuingia uwanjan

5. Kumbi za starehe Ukitembea kwenye majiji makubwa ambayo ni #Dar es salaam #Mwanza #Arusha #Dodoma msongamano ni mkubwa mno kwenye kumbi za starehe, lakini bado Serikali inashindwa kuchukua hatua na tahadhari ya kupambana na Covid licha ya kiongozi mkubwa wa nchi kutangaza

Nchi jirani na Tanzania tayari nimechukua hatua ya kujikinga na ugonjwa huu kwa
1. Kudhibiti mikusanyiko
2. Kufunga mashule
3. Kufunga Mabaa
4. Kudhibiti watu(lockdown) kwa mchana na usiku

Serikali yangu ya Tanzania imekuwa ikijivuta kama jongoo/Konokono katika kushughulikia na kudhibiti janga hili la Corona. Serikali kama haiwezi kupambana na ugonjwa huu iachie wananchi uhuru kama ilivyokuwa kwa #Mwendazake kuliko kutangaza ugonjwa covid upo na hatua zinachukuliwa kujikinga sifuri.
 
Aisee hii nchi inawatu wa lawama sana, sasa unataka serikali awavalishe watu barakoa na kuwanawisha mikono, serikali imeshatoa tamko la kuchukua tahadhari sasa kama mtashindwa kusikia shauri zenu.
 
Magufuli bus terminal kuanzia j3 auingii bila barakoa lakini kwenye Darby ya Simba Vs Yanga unazama tu bila barakoa.
Mpaka Corona yenyewe inashangaa.
 
Sikiliza ndugi yangu. Hata rais SSH haamini kama kuna corona. Ila anachofanya ni kuwafurahisha wapinzani ambao wamekuwa wakiimba corona,corona ili apendwe na pande zote. Ukweli ni kwamba corona iko kwenye smartphone na tv ila mtaani haimo. Hata rais anaamini hivyo. Si tunaenda hivyohivyo mpaka corona mwenyewe ajihudhuru.

Maana kushinda vita haimaanishi kwamba kwako hawajafa bali wamekufa wachache kuliko kwa adui. Hivyo corona tutaishinda japo wakufa watakuwepo.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Serikali ishakutangazia janga lipo, wananchi mchukue tahadhari, ni wewe tu kujiongeza uvae/usivae barakoa, ukakusanyike ama usikusanyike, unawe maji tiririka bila kusahau matumizi ya santaiza😋 ni wewe tu na akili yako, kaa ukiilaumu serikali sasa
 
Sikiliza ndugi yangu. Hata rais SSH haamini kama kuna corona. Ila anachofanya ni kuwafurahisha wapinzani ambao wamekuwa wakiimba corona,corona ili apendwe na pande zote. Ukweli ni kwamba corona iko kwenye smartphone na tv ila mtaani haimo. Hata rais anaamini hivyo. Si tunaenda hivyohivyo mpaka corona mwenyewe ajihudhuru. Maana kushinda vita haimaanishi kwamba kwako hawajafa bali wamekufa wachache kuliko kwa adui. Hivyo corona tutaishinda japo wakufa watakuwepo.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Ni kweli Corona haipo maana hata wodi wanazolazwa hao wagonjwa ktk hospital wanasema ni watu wenye changamoto ya upumuaji
 
Hatuna corona tuna changamoto za upumuaji

Corona Tanzania ni maigizo, leo tuna barakoa kesho hatuna

Hata wanaolilia uwepo wa corona fatilia mikutano yao wamevaa barakoa ila wanashikana mikono na hakuna kupeana nafasi wamesongamana balaa
 
Kwetu Vs Dunia!
 

Attachments

  • ud83dude2dud83dude02ud83eudd23_https___t.co_pnni5JaT7P.mp4
    720.4 KB
Back
Top Bottom