Tumepoteza shillingi moja, tunaomba msaada wa kuitafuta

Tumepoteza shillingi moja, tunaomba msaada wa kuitafuta

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
40,799
Reaction score
46,917
Mathematical Riddle ; Fumbo la Hisabati

Marafiki watatu, Gwajima, Wambura na CCM walienda hotelini kwa Tulia, wakalipia room shs.30/= , ambapo kila mtu alichangia shs.10/=.

Baadae Tulia akagundua kwamba gharama ya chumba ilikuwa shs.25/= tu, hivyo akamkabidhi mlinzi Mafwela shs.5/= ili awarudishie wageni pesa iliyozidi.

Kwa kuwa mlinzi allikuwa kilaza, na hakujua jinsi ya kugawanya shs.5/= baina ya watu watatu, akaamua kumpa kila mmoja shs.1/= , na yeye akabaki na shs.2/=.

Kwahiyo sasa, kila mgeni anakuwa amelipa shs.9/= ( sababu kila mmoja amerudishiwa shs.1/= katika ile shs.10 aliyolipa awali), hivyo jumla wamelipa shs.27/=.
Na Mlinzi Mafwela amebaki na shs.2/=, ambapo jumla inakuwa shs.29/=.

Je, Shs. 1/= iliyopotea , imeenda wapi?
===========================

View: https://www.instagram.com/reel/DH_smPPMr7U/?igsh=dHBrZHFuOHl1MTIy
 
Hii ni logical fallacy kwa sababu unajaribu kujumlisha kile ambacho tayari kimo ndani ya hicho kiasi i.e Tshs 2 ya mlinzi tayari IPO ndani ya Tshs 27.

Hivyo, mgawanyo sahihi ni:
  • Tulia/gharama ya chumba: Tshs 25
  • Gwajima, Wambura, CCM: Tshs 3
  • Mlinzi: Tshs 2

Jumla: Tshs 30.
 
Hii ni logical fallacy kwa sababu unajaribu kujumlisha kile ambacho tayari kimo ndani ya hicho kiasi i.e Tshs 2 ya mlinzi tayari IPO ndani ya Tshs 27.

Hivyo, mgawanyo sahihi ni:
  • Tulia/gharama ya chumba: Tshs 25
  • Gwajima, Wambura, CCM: Tshs 3
  • Mlinzi: Tshs 2

Jumla: Tshs 30.
Kwahiyo shilling 1 ipo wapi 😂
 
Tafsiri

Mwaka 2025 utawala wa Gwajima (upinzani wa ndani wa chama), CCM (chama tawala), na Wambura (vyombo vya dola) unamalizika kwa njia ya kisiasa. “Shilingi iliyopotea” haiwakilishi pengo la kifedha bali ni imani ya wananchi iliyopotea Sio hasara ya pesa, bali ni ishara kuwa mfumo unajisambaratisha kutoka ndani, na mamlaka yasiporudishwa kwa wananchi kwa dhati, mwaka 2025 hautakuwa tu uchaguzi bali ni mwisho wa enzi ya kisiasa. Hawataweza kutawala mpaka 2030.
 
Tafsiri

Mwaka 2025 utawala wa Gwajima (upinzani wa ndani wa chama), CCM (chama tawala), na Wambura (vyombo vya dola) unamalizika kwa njia ya kisiasa. “Shilingi iliyopotea” haiwakilishi pengo la kifedha bali ni imani ya wananchi iliyopotea Sio hasara ya pesa, bali ni ishara kuwa mfumo unajisambaratisha kutoka ndani, na mamlaka yasiporudishwa kwa wananchi kwa dhati, mwaka 2025 hautakuwa tu uchaguzi bali ni mwisho wa enzi ya kisiasa. Hawataweza kutawala mpaka 2030.
Mmeambiwa muache Gwajimanisation 😂
 
Tafsiri

Mwaka 2025 utawala wa Gwajima (upinzani wa ndani wa chama), CCM (chama tawala), na Wambura (vyombo vya dola) unamalizika kwa njia ya kisiasa. “Shilingi iliyopotea” haiwakilishi pengo la kifedha bali ni imani ya wananchi iliyopotea Sio hasara ya pesa, bali ni ishara kuwa mfumo unajisambaratisha kutoka ndani, na mamlaka yasiporudishwa kwa wananchi kwa dhati, mwaka 2025 hautakuwa tu uchaguzi bali ni mwisho wa enzi ya kisiasa. Hawataweza kutawala mpaka 2030.

Narudia, shilingi moja imeenda wapi?!
 

Narudia, shilingi moja imeenda wapi?!
Wamechukua wananchi
 
Tafsiri

Mwaka 2025 utawala wa Gwajima (upinzani wa ndani wa chama), CCM (chama tawala), na Wambura (vyombo vya dola) unamalizika kwa njia ya kisiasa. “Shilingi iliyopotea” haiwakilishi pengo la kifedha bali ni imani ya wananchi iliyopotea Sio hasara ya pesa, bali ni ishara kuwa mfumo unajisambaratisha kutoka ndani, na mamlaka yasiporudishwa kwa wananchi kwa dhati, mwaka 2025 hautakuwa tu uchaguzi bali ni mwisho wa enzi ya kisiasa. Hawataweza kutawala mpaka 2030.
Amina!!! , Aminaaaa!!
 
Back
Top Bottom