Tumependana...!!

Tumependana...!!

Tetra

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
1,526
Reaction score
771
::
Tumependana ndiyo!
Tusichukiane kwa makosa yanayopita.
::
Tumependana ndiyo!
Tusionyeshane jeuri hakuna mkubwa katika kupenda.
::
Tumependana ndiyo!
Usisahau niliyofanya ukakumbuka ambayo sikufanya.
::
Tumependana ndiyo!
Usinipe mitego ya kujaribu upendo wangu,naweza kuteleza nisiinuke tena.
::
Tumependana ndiyo!
Usinipe mgongo mapema,huo uamuzi una wakati wake haulazimishwi.
::
Tumependana ndiyo!
USINIVUNJE MOYO,,UKIUVUNJA VUNJA KILA KIPANDE KITAOKOTWA NA MWENZAKO,LAWAMA ZAKO KWAMBA NILIKUTENDA ZITAKOSA BARAKA.
=
 
Naam, chambilecho, Ngabu.
Ujumbe wako kuntu.
Umegonga penyewe ikulu.

Umeandika na umesomeka.
Yakini pasi utata.
Asiyeelewa kwake imekula.
 
::
Tumependana ndiyo!
Tusichukiane kwa makosa yanayopita.
::
Tumependana ndiyo!
Tusionyeshane jeuri hakuna mkubwa katika kupenda.
::
Tumependana ndiyo!
Usisahau niliyofanya ukakumbuka ambayo sikufanya.
::
Tumependana ndiyo!
Usinipe mitego ya kujaribu upendo wangu,naweza kuteleza nisiinuke tena.
::
Tumependana ndiyo!
Usinipe mgongo mapema,huo uamuzi una wakati wake haulazimishwi.
::
Tumependana ndiyo!
USINIVUNJE MOYO,,UKIUVUNJA VUNJA KILA KIPANDE KITAOKOTWA NA MWENZAKO,LAWAMA ZAKO KWAMBA NILIKUTENDA ZITAKOSA BARAKA.
=

Malenga wetu..ndio tukupe hongera au?

Haya mapenzi yanaua ~sosi Muumin Mwinjuma
 
Last edited by a moderator:
Naam, chambilecho, Ngabu.
Ujumbe wako kuntu.
Umegonga penyewe ikulu.

Umeandika na umesomeka.
Yakini pasi utata.
Asiyeelewa kwake imekula.

::
Nyani Ngabu
Umenena pia,sifa zikurudie wewe uliyeng'amua
=
 
Last edited by a moderator:
Tumependana ndio!
Basi nithamini usiponithamini wenzio watanithaminisha

::
Naam,,kuthamini hakuhitaji nguvu,kweli NatJ
Mapenzi ni matunzo
=
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji, kuna malenga wapya huku.
Tetra,
ni kweli tumependana
penzi letu linafana
tena linanoga sana
kwani tunaelewana
zaidi tumeshibana
na hata tukigombana
mbali h'tutafikishana.

ni kweli tumependana
si kama zombie wa Kongosho
kisa shamba la korosho

ni kweli tumependana
si kama mchaga wa lara 1
kutwa kuchwa kibaruani

ni kweli tumependana
si kama King'asti na Paw
ata kitukana apewi poo

ni kweli tumependana
zaidi ya babu Asprini
na wakeze themanini

ni kweli tumependana
zaidi ya ma Ngina na Mtambuzi
kamwe sitoki nje, hata niwe nje ya zizi

ni kweli tumependana mzabzab apate somo
la penzi liso kikomo!!!!:yo:
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji, kuna malenga wapya huku.
Tetra,
ni kweli tumependana
penzi letu linafana
tena linanoga sana
kwani tunaelewana
zaidi tumeshibana
na hata tukigombana
mbali h'tutafikishana.

ni kweli tumependana
si kama zombie wa Kongosho
kisa shamba la korosho

ni kweli tumependana
si kama mchaga wa lara 1
kutwa kuchwa kibaruani

ni kweli tumependana
si kama King'asti na Paw
ata kitukana apewi poo

ni kweli tumependana
zaidi ya babu Asprini
na wakeze themanini

ni kweli tumependana
zaidi ya ma Ngina na Mtambuzi
kamwe sitoki nje, hata niwe nje ya zizi

ni kweli tumependana mzabzab apate somo
la penzi liso kikomo!!!!:yo:

::
Heshima yako Mentor
!!!!
=
 
Last edited by a moderator:
Naam!!

Ni kweli tumependana,
Na tena tunapatana
Mioyo imeshikana
Kama kushika supana
Si penzi la kutegana
Ila kutegemeana!

Daima tunawazana
Umbali si kitu bwana
Huwa tunakumbukana
Kila tunapoagana
Simu tunapigiana
Na meseji zashindana!

Na hamu ikitubana
Ya mambo ya kushikana
Wallahi tunapeana
Ni hekaheka ee bwana!
Tukichoka twabebana
Na maji kumwagiana
Kisha tunarudiana
Hilo ni penzi mwanana!!

Kupenda tunapendana
Nisikieni vijana
Ni muhimu kushibana
Siyo kupigana
Wala hamtachokana
Mwisho mje kupigana
Tungo inaisha bwana
Yu wapi wangu mwanana!?

Na. MMM (Tarumbeta ya Kijiji)
 
Naam!!

Ni kweli tumependana,
Na tena tunapatana
Mioyo imeshikana
Kama kushika supana
Si penzi la kutegana
Ila kutegemeana!

Daima tunawazana
Umbali si kitu bwana
Huwa tunakumbukana
Kila tunapoagana
Simu tunapigiana
Na meseji zashindana!

Na hamu ikitubana
Ya mambo ya kushikana
Wallahi tunapeana
Ni hekaheka ee bwana!
Tukichoka twabebana
Na maji kumwagiana
Kisha tunarudiana
Hilo ni penzi mwanana!!

Kupenda tunapendana
Nisikieni vijana
Ni muhimu kushibana
Siyo kupigana
Wala hamtachokana
Mwisho mje kupigana
Tungo inaisha bwana
Yu wapi wangu mwanana!?

Na. MMM (Tarumbeta ya Kijiji)

::
Ee Tarumbeta ya kijiji
Sauti yako yazidi jiji
We Mzee Mwanakijiji
Kwangu nakupa taji.
::
Mi bado mwanafunzi
Nawe kwangu kurunzi
Kwa sayansi ya utunzi
Hapo umezidi ujuzi.
::
mwana kijiji sikia
JF zidi kuimulikia
Nasi tuoneshe njia
Mbali tupate pafikia
=
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom