Tumepata wapi upofu kutoona aliyofanya Maswi?

Tumepata wapi upofu kutoona aliyofanya Maswi?

Labda aseme mwingine lakini na sio Huyu,Balile ni Kweli watanzania tunasahau lakini sio kiasi hicho. Bado tuna kumbuka Kuwa wewe ni raisi wa na editor makanjanja na huu ndio msimu wenu wea Biashara, tunakumbuka article ya namna hii 2010 iliyoongelea lipstick ya mke wa Lowassa na namna viatu vya bwana mkubwa vinavyongaa kwa kiu. Wewe na hai kinda Maswi mnatofauti gani? How cheap unatia kinyaa ndugu yangu Kwani wameshaingiza zote ama nusu baada ya kazi? Ni pay role tu hata Kuwa Mhariri wea gazeti la kamala haujakusaidie kupata akii. Keep your opinions to yourself, hivi bado unaendeleaje Ile freelancer ya Rostam yenye engine ya RAV4?
 
Ninaamini pesa inanguvu na inabadiri watu. Balile!!! Maswi katika mradi wa REA Siye anayestahili misifa na kupambwa kote huko! fuatilia project za REA zilianzishwa na nani ? on which kama ktibu mkuu ni laazima zitamgusa si kwa sababu ni Maswi hata ungekuwa wewe! nahisi ungejisifia
 
Balile sidhani ujio wa REA ni ujio ambao umekuja kwa kuwa initiated na Maswi au Muhongo.

Ni juhudi ya watu wengine ambayo wao wameyakuta na kuya implement kama ambavyo wewebuna implement matunda ya uhuru wa vyombo vya habari kwa kupotosha jamii.

Hii ina maana kuwa hata bila maswi pengine hata wewe katika position yako kama ungekuwa katibu mkuu wa wizara hiyo ungefanya tu kqa sbb ni majukumu yako.

Hata hvyo kufanya mazuri mengi kwa kutimiza wajibu hakuhalalishi muhusika kufanya madudu kwa kuwa eti mabaya hayo yatafunikwa na mazuri uliyoyafanya, it elements stands its own.

Kwa hiyo mazuri ya Maswi kama Balile usemavyo haya justify yeye kufanya mabaya, alikuwa pale kwa maana ya kutenda yaliyo mazuri kwa manufaa ya umma.

Uandishi wa namba hiyo ni ukosefu wa weredi au uzumbu wa kutaka kutetea hata yasiyo mayai!

Bakile badirika usiwe mwaandishi njaa usiyeweza kutenganisha nyekundu na njano kwa upofu wa mapesa ambayo pia ni jasho la nduguzo wa Kagera ambao miaka mingi wamekatwa kodi pasipo kupata huduma kwa sababu ya watu wenye akili kama zako kutetea wizi na upokaji wa mali za wananchi.
 
Last edited by a moderator:
Kumbe hata waandishi wa habari ni vilaza wa kufikiri na kuchambua mambo. Tulitegemea wewe kama muhandisi wa habari uchambue vizuri kati ya utendaje mzuri wa kazi na Kashfa ya ESCROW (Ufisadi). Kama waandishi wetu ndiyo mnafikiria namna hii kweli tumekwisha kama Taifa

Pengine uandishi wa namna hii ndo wa wale wanaitwa uchwara. Ebu wewe mwandishi tueleze kiasi cha fedha alichotumia Maswi kutoka kwenye mfuko wake. Yote aliyoyasimamia alifanya hivyo kutokana na bajeti iliuokuwa imepitishwa na bunge. Acheni uandishi wa upotoshaji.
 
Maswi ni mwizi. Kumbuka alisema Kafulila na Zitto wakutane mitaani awatwange. Haya si maneno ya kutamkwa na katibu mkuu wa serikali. Kwa maneno hayo tu, alitakiwa kufukuzwa kazi.

Ni vema mwandishi akumbuke kuwa Maswi is not infallible. Wapo watz wengi waaminifu na wachapa kazi hata kuliko Maswi wako.
Unamtetea mwizi? Wewe mtu wa ajabu kweli2.
 
Wana Jamii,

Huwa inafika mahali nasoma mawazo ya baadhi ya wachangiaji au watoa mada nashindwa kabisa kuelewa kuwa ni nini kinawapelekea kujifanya hawaoni/kupindisha ukweli.

Ni jambo lililodhahari kuwa ukifanya mazuri mia moja (100) hayahalalishi kufanya moja baya! Na kama ingekuwa inaruhusiwa hivyo, basi tungeshuhudia mambo ya ajabu kabisa yakifanyika hapa duniani na kuachwa tu, kisa aliyefanya uovu ni kiongozi ambae amefanya mazuri mengi.

Labda nimuulize ndugu Balille kwa nia nzuri tu, hivi itokee mtu afanye mambo makubwa/mazuri kama unavyotaka kutuaminisha, halafu afumaniwe na mke wa mtu, na bahati mbaya mke huyo awe ni wako, utasema aachwe tu kwa kuwa mtuhumiwa katusambazia umeme hadi kijijini kwetu?

Najua kuna watakaosema mifano hii haiendani, lakini kwangu, dhambi ni dhambi tu iwe umeiba, umeua au umetembea na mke wa mtu na kwamba mazuri mengi hayafuti mabaya machache kama inavyofanyika kwenye nadharia ya hesabu! (100 -1=99 Kwamba mazuri 100 yamefuta 1 baya na kubakia mazuri 99)

Nafikiri, ifike mahali tuwe wakweli ili pale mtu anapokosea awajibike kwa makosa yake.
 
Huyo Maswi ndio kama Kalemani wa leo?
 
Back
Top Bottom