Tumepata wapi upofu kutoona aliyofanya Maswi?

Tumepata wapi upofu kutoona aliyofanya Maswi?

Maswi ameonewa sana. Yale aliyotekeleza Maswi ni Maagizo kutokana na barua ya Werema. Maswi ni JEMBE. Aliyoyafanya Maswi mmeyaona na mtazidi kuyaona, ni vyema akarudishwa kwenye madaraka yake mara moja.
Acheni Mpare amalize kazi yake kwanza, kwa yule no fear, no favour. Tutapata lililo la ukweli
 
Kaka mengi anavuruga nchi kwa ulafi wake nataman Tanzania ipate rais makini amnyooshe huyu babu anayebaka vtoto kna kylne....maswi na muhongo wamefanya kazi kubwa sana ila mengi dalali wa vtalu vyetu vya madini na anayetumia watoto yatima kukwepa kodi anawachafua kupitia vbaraka wake waganga njaa..akawalipe kwanza wafanyakazi wake vizuri huyu mkwepa kodi mengi.
. Mengi anaingiaje hapo? una elimu ya level gan ww?kila kitu bungeni kilikua waz,analyse na fanya decision! kina profesa na watu wake wametukosea sana watz..watu wa musoma vijiji (majita ku....yo) mnamwona ka Mungu kwavile hamna maprofesa .
 
toka Balile na mwenzio [MENTION]Jackton Manyerere[/MENTION], mlipokubali kufadhiliwa na lowasa pesa ya kuanzisha gazeti MLIPOTEZA credibility ya kukemea Ufisadi.

Kwa iyo umeme kufik kwenu inafuta makosa ya makusudi ya kitendaji waliyofanya Maswi na Muhongo??

kwaiyo utekelezaji wa mradi wa REA ni ushahidi kuwa maswi hausiki ESCRAW?? iyo sheria unayosoma haikusaidii
 
Last edited by a moderator:
Bwana Balile. Ukitaka kuwa msafi katika utumishi wowote ule, pale bosi wako anapofanya makosa, wewe unatakiwa kunawa mikono kwa kujiuzulu, ili usiunganishwe na huo uamuzi. Bwana Maswi aliposhauri vizuri, wenzake na mabosi wake walipoenda mrama, alitakiwa ajiuzulu ili kunawa mikono, abaki msafi. Kwa kubaki kwakwe ofisini, mambo yameenda vibaya ofisini kwake yeye akiwa mtendaji mkuu. Nani awajibike? Huwezi kubaki ofisini ukiwa na kosa kubwa, ukaendelea kudai huo uamuzi ulifanywa na wakubwa, wewe huhusiki, wakati taasisi yako ndio imeyumba na kuporomoka. Unakosa uhalali wa kuwepo ofisini kama mtendaji mkuu na mfanya maamuzi mkuu. Tena pale ushauri wake ulipotupiliwa mbali na Ikulu na CAG, tayari alishadharaulika, alitakiwa aombe kuachia ofisi. Tunawaomba watumishi wote wa umma kuwa imara katika ofisi zao, kufanya kazi kwa misingi ya sheria, na kujiamini kitaaluma na kiuweledi. Hii itapunguza kuingiliwa na wanasiasa na watendaji wengine waganga njaa na mafisadi. Tanzania ya leo inahitaji watumishi imara katika maamuzi, kujiamini, uwazi na weledi.
 
nikiona mada nitaharibu sichangii maana watu wandhani nchi hii haina wachapakazi waadilifu
 
Maswi amefanya mengi sana nchi hii, bila shaka tutakosea sana kama Maswi ataondolewa kwenye wadhifa huo, ni mchapakazi hodari asiyependwa na mafisadi hadi kufikia kumuundia zengwe.
 
Kaka mengi anavuruga nchi kwa ulafi wake nataman Tanzania ipate rais makini amnyooshe huyu babu anayebaka vtoto kna kylne....maswi na muhongo wamefanya kazi kubwa sana ila mengi dalali wa vtalu vyetu vya madini na anayetumia watoto yatima kukwepa kodi anawachafua kupitia vbaraka wake waganga njaa..akawalipe kwanza wafanyakazi wake vizuri huyu mkwepa kodi mengi.

Yaani wewe sijui uliachwaje uraiani usipelekwe lupango na panya road wenzio. Mengi anahusishwaje kwenye uzi huu?
 
Kwani kuna mtu kasema Maswi hakuwa anatimiza wajibu wake kwenye maeneo mengine?
Mkuu hii ndio inaonyesha kwamba kwa Tanzania mtu akipiga kazi sana hata achakachue vipi kuna watu lazima watamtetea simply because amefanya kitu flani positively yaani ni sawa na mtu ambae alikufadhiri alafu anakuporomoshea matusi unashindwa kuchukua hatua kisa aliwahi kukufadhiri. Ifike mahali watu waelewe kwamba hawa watumishi wa umma wateule wa raisi au vinginevyo na viongozi wa kisiasa wapo kwa ajili ya kuleta maendeleo hivyo anapofanya kitu chochote kizuri shukurani ni kwetu wote watz (kwa kulipa kodi) maana nashangaa watu wanavyotoa shukrani utasema hao jamaa walifanya kazi pasipo mshahara.

Ni sawa na polisi kakamata jambazi tunaanza aisee inabidi tumshukuru sana (kwani aliajiriwa ili afanye nini)

Nimeandika mengi lakini geraldkowero1 amemaliza yote kwenye post #30
 
Last edited by a moderator:
Maswi amefanya mengi sana nchi hii, bila shaka tutakosea sana kama Maswi ataondolewa kwenye wadhifa huo, ni mchapakazi hodari asiyependwa na mafisadi hadi kufikia kumuundia zengwe.

Msichokijua ni kuwa utumishi wa umma unahitaji uaminifu na uadilifu100% Mbona kichwa kinachoitwa Ruta kilimaliza mwendo salama? Alikataa maagizo yooooote ya kifisadi toka jumbajeupe. akalazimishwa kustaafu at 55.
Balile, Hata ukiwa Mchapakazi vipi, ndo ukiambiwa ujinyonge unajinyonga? Haya sasa ameshajinyonga!! utafanyaje?

c.c Balile, nyamemba na watwanga debe wengine
 
Nadhani Balile aniombe radhi kwa kujaribu kunishawishi kwamba Maswi kaonewa na Kikwete.
 
Balile kalipwa kiasi gani kumtetea Maswi?

Maswi angejiuzulu kuliko kukubali kutenda mambo ambayo aliona hayana tija kwa taifa. AWAJIBISHWE!
 
kumsifia Maswi khs mradi wa rea ni kumpa sifa nje ya uwezo wake.

cjakuskia ukimtaja prof. mhongo ?.
 
Mimi nakubaliana na Balile katika maeneo yafuatayo;

Mosi,ni ukweli uliowazi kuwa mwizi wa hizi pesa zetu ni Rais wetu huyuhuyu anayeitwa Jakaya Kikwete ,familia yake na marafiki zake.

Pili, ofisi ya mwanasheria mkuu kwa maana ya Jaji Werema kama mshauri mkuu wa kisheria wa nchi/Rais ilitumika tu kama "cover" dhidi ya Rais ambaye anajua kabisa kuwa ana kinga ya kikatiba dhidi ya jinai yoyote akiwa madarakani na hata aachapo madaraka ya Urais ( kwa makosa yote aliyoyatenda akiwa Rais). Na hili si kosa lake bali ni udhaifu wa katiba yetu ya JMT ya mwaka 1977. Na baba wa taifa Mwl J.K. Nyerere (Mungu amrehemu huko aliko) aliwahi kuonya juu ya "udhaifu wa katiba" ambayo inampa Rais madaraka na kinga kubwa kupita kiasi hata ya kuua mtu na asishtakiwe popote na wakati wowote, kuwa kwa katiba hii siku nchi hii ikipata Rais kichaa, basi ni lazima atatumia mwanya huo wa kikatiba kuuvaa " udikteta"!

"Labda" Jakaya Kikwete si dikteta lakini anautumia udhaifu wa kikatiba inayompa kinga kuwa mwizi na kuwaibia wananchi wake mwenyewe na hili ni tatizo baya kuliko hata udikteta wa kuamuru wapinzani wake wanyongwe au waswekwe gerezani!!

Kwa hiyo hoja ya Balile hapa ni kuwa "fedha za Escrow Account" toka BoT kwenda kwa kina PAP na VIP ya James Rugemarila zilitoka kwa agizo la Rais huyu aliyezungukwa na kuta za kinga za kikatiba pande zote na kwa hiyo kina Maswi, Mhongo and others si lolote, si chochote ni kuukumbatia mbuyu tu badala ya kuudondosha!!.

Hata ivyo katiba ibatoa njia ya kumwajibisha Rais aliyetenda jinai kwa kuptia Bunge kwa kum - impeach.......kushtakiwa kibunge jambo ambalo mtoa hoja amekiri kuwa kwa mfumo wa sasa ambapo kwa zaidi ya 80% ya bunge inahodhiwa na chama kimoja atokacho Rais na aina ya wabunge wenyewe tulionao, mashtaka dhidi ya "Rais wao "yataishia getini tu!!

Swali kubwa na muhimu hili; kwamba, Rais kama ataumiza wangapi ndipo tuseme inatosha?...Nauliza hili kwa sababu whether Balile na wenzako mnapenda au hampendi, mnataka au hamtaki kina Maswi, Prp. Mhongo and the others lazima waondoke kwa sababu ndiyo rahisi kwetu, ndiyo halali yetu!!

Hawa kama walikuwa wanataka kutunza heshima zao, rekodi ya utendaji kazi wao uliotukuka kwa kutandaza nguzo na nyaya za umeme kila kijiji na kitongoji (jambo ambalo si kweli) japo umeme wenyewe ni tatizo (not reliable na ni ghali sana) kwa sbb ya "capacity charges", basi, walikuwa na option moja tu kwa wakati ule nayo ni;

Kujiuzuru nafasi zao walizokuwa wanazishikiria na kumwambia bosi wao kinagaubaga kuwa kwa namna jambo lilivyo sipaswi/hatupaswi kuwa sehemu ya kushiriki wizi huu. Hapo "intergity" ya watumishi hao inayotetewa na kina Balile ingetetewa na kila mtanzania mzalendo leo!!


Lakini kama walikuwa wanatambua kuwa mkubwa wao Rais anakosea na anawaingiza katika uchafu wakidhani na wao wana kinga kikatiba na wakakubaliana naye, hawana namna nyingine zaidi ya kukubaliana na yanayowapata sasa!..

Swali kubwa litaendelea kuwa hili; mpaka lini ataendelea kuumiza wengine?? Alimuumiza rafiki yake wa karibu Lowassa na wenzake (mpaka leo jamaa hasafishiki kwa jiki au sabuni yoyote!!) ktk ile kashfa ya kampuni feki ya ufuaji umeme ya Richmond
 
This is very low Balile, Hivi jambazi anayeitunza vizuri familia na ndugu zake tumuache tu kwakuwa anasaidia sana!!? I'll buy this!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom