Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,176
- 25,919
Kuna kauli nyingine ni wana siasa tu wanaweza kuzitoa. Lakini pia niliisikia kwa mume fulani aliua mke kisiri akawa anasema nimeondokewa na mpendwa wangu, baadae akajulikana yeye ndio aliua.
Jaribu kutafakari. Unafanya premeditated murder (uuaji uliokusudiwa) kwa kutoa amri kwamba hawa watu wapigeni risasi za kuua, sio kujeruhi. Na unahakikisha ili amri hiyo itekelezwe ipasavyo ulete askari wa kutoka upande ambao unajua hautakuwa na huruma au wa nje ya nchi.
Na baada ya kufanikisha uuaji uliokusudiwa unatoa kauli kwamba nguvu sahihi ilitumika mlitaka tufanyeje. Unazidi kukanyagia kwamba kama hukutaka mtoto wako auwawe kwa nini hukumzuia kwenda kuandamana. Halafu wanaokuuliza kwa nini umeua raia unawaambia "who are you?"
Halafu unahutubia ukisema tumeondokewa na wapendwa wetu.
Hivi ni mimi tu nahisi kuna kitu hakiko sawa sehemu fulani ya mwili au na nyie pia Wana JF?
Jaribu kutafakari. Unafanya premeditated murder (uuaji uliokusudiwa) kwa kutoa amri kwamba hawa watu wapigeni risasi za kuua, sio kujeruhi. Na unahakikisha ili amri hiyo itekelezwe ipasavyo ulete askari wa kutoka upande ambao unajua hautakuwa na huruma au wa nje ya nchi.
Na baada ya kufanikisha uuaji uliokusudiwa unatoa kauli kwamba nguvu sahihi ilitumika mlitaka tufanyeje. Unazidi kukanyagia kwamba kama hukutaka mtoto wako auwawe kwa nini hukumzuia kwenda kuandamana. Halafu wanaokuuliza kwa nini umeua raia unawaambia "who are you?"
Halafu unahutubia ukisema tumeondokewa na wapendwa wetu.
Hivi ni mimi tu nahisi kuna kitu hakiko sawa sehemu fulani ya mwili au na nyie pia Wana JF?