OCC Doctors
Senior Member
- Jul 20, 2018
- 104
- 151
Mafuta ya ziada kwenye tumbo (Obesity) husababisha mshipa unaoleta damu ndani ya ini (Portal vein) kujaa mafuta ya asidi yasiyo na kazi (free fatty acids), na kuongeza mkusanyiko wa mafuta kwenye ini.
Mafuta pia hujilimbikiza kwenye seli za misuli. Ambapo sasa kunaanzishwa ukinzani dhidi ya homoni inayo dhibiti sukari mwilini (Insulin resistance), na hatimae homoni ya insulin kuzagaa kwenye damu kuliko kawaida (hyperinsulinemia), na hapo ndipo uratibu wa sukari mwilini unaharibika, ugonjwa wa kisukari unaanza.
Baada ya mafuta kuzagaa kwenye misuli, hatua inayofuata ni ongezeko la mafuta kuanza kuenea kwenye damu (dyslipidemias) na hapo sasa shinikizo la juu la damu (hypertension) hujitokeza.
Hali hiyo hupelekea viwango vya sumu-taka (uric acid) kuongezeka katika damu, na hapo ndipo hali ya kuganda kwa damu huanza (prothrombotic state) ambayo huongeza viwango vya protini ya kugandisha damu 'fibrinogen' na kuzuia-vizuizi vya kuyeyusha damu "plasminogen inhibitor I'' kufikia hapo sasa damu itaanza kuganda ambapo uvimbe wa kizazi (Fibroid) utajiunda mfano wa nyama ya maini kwenye kizazi cha mwanamke.
Wagonjwa hao wenye ongezeko la tumbo (obesity) wana hatari ya kupatwa na ongezeko la kukosa pumzi wakati wa kulala kutokana na sehemu ya kupitisha hewa kuziba ambapo huanza kukoroma wakilala (obstructive sleep apnea) ni kutokana na uhaba wa kupita kwa pumzi kwenye bomba la hewa.
Hatari zingine ni pamoja na hatua ya juu ya ugonjwa wa ini usiohusiana na pombe (nonalcoholic steatohepatitis), kutokana na mwili kuhifadhi mafuta mengi kwenye ini.
Pia ugonjwa sugu wa figo, ugonjwa wa vimbe kwenye vifuko vya mayai (polycystic ovary syndrome) kwa wanawake.
Uwepo wa tumbo kubwa na mafuta ya ziada hushusha homoni ya kiume kua chini, hupelekea kiwango cha chini cha homoni ya kiume kwa wanaume (low serum testosterone), ambapo sasa huleta shida ya kusimamisha uume au upungufu wa nguvu za kiume au vyote kwa pamoja.
Mafuta pia hujilimbikiza kwenye seli za misuli. Ambapo sasa kunaanzishwa ukinzani dhidi ya homoni inayo dhibiti sukari mwilini (Insulin resistance), na hatimae homoni ya insulin kuzagaa kwenye damu kuliko kawaida (hyperinsulinemia), na hapo ndipo uratibu wa sukari mwilini unaharibika, ugonjwa wa kisukari unaanza.
Baada ya mafuta kuzagaa kwenye misuli, hatua inayofuata ni ongezeko la mafuta kuanza kuenea kwenye damu (dyslipidemias) na hapo sasa shinikizo la juu la damu (hypertension) hujitokeza.
Hali hiyo hupelekea viwango vya sumu-taka (uric acid) kuongezeka katika damu, na hapo ndipo hali ya kuganda kwa damu huanza (prothrombotic state) ambayo huongeza viwango vya protini ya kugandisha damu 'fibrinogen' na kuzuia-vizuizi vya kuyeyusha damu "plasminogen inhibitor I'' kufikia hapo sasa damu itaanza kuganda ambapo uvimbe wa kizazi (Fibroid) utajiunda mfano wa nyama ya maini kwenye kizazi cha mwanamke.
Wagonjwa hao wenye ongezeko la tumbo (obesity) wana hatari ya kupatwa na ongezeko la kukosa pumzi wakati wa kulala kutokana na sehemu ya kupitisha hewa kuziba ambapo huanza kukoroma wakilala (obstructive sleep apnea) ni kutokana na uhaba wa kupita kwa pumzi kwenye bomba la hewa.
Hatari zingine ni pamoja na hatua ya juu ya ugonjwa wa ini usiohusiana na pombe (nonalcoholic steatohepatitis), kutokana na mwili kuhifadhi mafuta mengi kwenye ini.
Pia ugonjwa sugu wa figo, ugonjwa wa vimbe kwenye vifuko vya mayai (polycystic ovary syndrome) kwa wanawake.
Uwepo wa tumbo kubwa na mafuta ya ziada hushusha homoni ya kiume kua chini, hupelekea kiwango cha chini cha homoni ya kiume kwa wanaume (low serum testosterone), ambapo sasa huleta shida ya kusimamisha uume au upungufu wa nguvu za kiume au vyote kwa pamoja.