Tumefikaje hapa tulipo?

Hawana njia nyingine hawana ushawishi kwa wananchi wanaenda enda tu wamechoka sana aibu kwao ni kubwa na kinachowaweka hadi saivi ni kulinda mali zao za wizi
 
Mkuu wangu mimi nasikiliza sana Hotuba za Viongozi wote. Labda nikeambie tunkwamba wote hutumia neno hao MAADUI ZETU kama ni Upinzani. Huamini nitazieeka hapa.
Umeulizwa swali rahisi tu. Toa mifano ya "matendo ya kikatili", ya kuharibu UTU wa wanaCCM uliofanywa na hao CHADEMA kwa "adui zao" CCM.
"Neno "adui" katika maswala ya kisiasa unalitafsiri vipi kuwa kusigina UTU wa mtu mwingine?
 
Acha upotoshaji usio na tija, bunge maalum la katiba halikuvunjika bali lilienda hadi mwisho, ikapatikana katiba pendekezwa iliyokuwa inasubiri kura ya maoni. Ila alipoingia Magufuli akasema hakuahidi katiba mpya kwenye kampeni zake. Sema kundi la Ukawa liligomea kuendelea na bunge lile, baada ya kuona wabunge wa ccm wakichezea maoni ya wananchi yaliyokuwa kwenye rasimu ya Warioba.
 
Mada hii ni swali:
"Tumefikaje Hapa tulipo".

Kama wewe siyo mtu unayependa majibu ya mizunguko mingi na unafiki chungu nzima ndani yake, swali hili ni rahisi tu.

Kwamba wakati uliwadia, na fursa ikajitengeneza kwa kundi ambalo siku zote limekuwepo likiwa na madai yake maalum, limetumia fursa hiyo (seized the moment) kujinyanyua.

Sasa kuna ugumu gani hapo kuelewa!
 
Hivi ilikuwaje Zanzibar wakaandika katiba yao 1984 yenye kuifanya Zanzibar huru bila Tanganyika kupewa Uhuru,na wasomi pamoja na Mwalimu Nyerere wakaangalia na kuacha hiyo katiba ifanye kazi wakati Tanzania bado ipo?
 
Magufuli aliandaa ukumbi bila kujuwa sherehe itakuwa vipi, Samia kaleta sherehe iliyosheheni burudani ambazo waTanzania walijisahaulisha kuwa zilikuwepo chinichini miongoni mwao tokea uhuru.
 
Hivi ilikuwaje Zanzibar wakaandika katiba yao 1984 yenye kuifanya Zanzibar huru bila Tanganyika kupewa Uhuru,na wasomi pamoja na Mwalimu Nyerere wakaangalia na kuacha hiyo katiba ifanye kazi wakati Tanzania bado ipo?
Hapana. Utakuwa umechanganya mwaka wa hiyo Katiba ya Zanzibar, na mabadiliko mengine yaliyofuata wakati huo

Haya ya Katiba yalikuja baadae sana wakati wa Kikwete.
 
Shukran saana, kwa hoja hii ya msingi kabisa ambayo hata mimi yanipa shida kusema kwa uhakika tunawezaje kutoka hapa.

Hatuwezi kurudisha UTU wetu kwa maandishi kwa sababu hata Katiba hii mnayosema mbovu haifuatwi katika maswala ya msingi kabisa.

Ninewahi tolea mfano HAKI ambayo ipo ndani ya Katika Sura ya kwanza sehemu ya 3 lakini imekiukwa wazi wazi kabisa mpaka tumefikia mauaji ya Watu wasokuwa na hatia na hata walikuwa na hatia utawala ulishindwa kufuata taratibu za Kisheria. Hii yote ni kutokana na kupoteza Heshima na thamani ya UTU wetu badala yake tumeishi kwa Mazoea...

Ukiniuliza mimi nitasema hivi. Hatuwezi kuwa na siku ya maombolezi, siku ya Maridhiano wala Katika Mpya/Mpito pasipo kuwa na - SERIKALI YA MPITO. Tunaipataje?

Sina maana rais apinduliwe au aondolewe kwa nguvu madarakani kwa sababu hatutaki kumwaga zaidi damu za Watanzania na kusababisha uadui mkubwa zaidi isipokuwa dhahiri hatuwezi kifikia muafaka wa aina yeyote Rais akiendelea kuwepo madarakani.

Ataondokaje Madarakani?
- Rais akubali kuwa Bangusilo kwa kulinusuri Taifa hili na manufaa ya wote - AJIUZURU yeye mwenyewe kwa hiari yake akithamini UTU wa Watanzania na Katiba itamlinda. Hakuna njia nyingine salama na yenye baraka kwetu nayoiona mimi.

Tukubali sote hatashtakiwa, atalindwa na mafao yake ataendelea kupata kama marais wengine wastaafu walomtangulia. (It's Win win situation on both sides) Tukumbuke rais ana mamlaka makubwa sana na akikataa hakuna kitakacho fanyika iwe maombolezi, maridhiano wala Katiba Mpya/ya Mpito. Huu ndio Ukweli mchungu.

Kustaafu kwake, Kikatiba kutatupa mwanzo mpya, tutaunda Serikali ya Mpito, tutaweza kuomboleza sote kwa pamoja, tutaweza kufanya maridhiano ya pamoja na sii lazima Uchaguzi Mkuu ufanyike 2030. Ni mpaka pale tumeweza kukamilisha maswala yote ya kutuunganisha Wananchi Upya kama jamii moja ya Watanzania.

Nimeandika haya kama mtazamo na maoni yangu naomba sana isitafsiriwe vinginevyo.

Maasalaam
 
Umeulizwa swali rahisi tu. Toa mifano ya "matendo ya kikatili", ya kuharibu UTU wa wanaCCM uliofanywa na hao CHADEMA kwa "adui zao" CCM.
"Neno "adui" katika maswala ya kisiasa unalitafsiri vipi kuwa kusigina UTU wa mtu mwingine?
Marekani katika siasa zake husema wazi Russia ni Adui zao, wamewahi kuuana? Au kwako wewe Uadui ni vita tu! Hata mauaji ya Wana Chadema mimi sina Ushahidi kuwa ni CCM ila nayasoma. Acha mauaji najua Mbowe leo hii ni Adui wa Chadema hii haifichiki.

Ukiniuliza mimi nitoe Ushahidi utakuwa unanionea ila najua fika UADUI upo kubali usikubali haiondoi mtazamo wangu na hatuwezi fikia muafaka wa aina yeyote ikiwa tutakuwa in denial of the facts..
 
Kama mtu umejipachika hakuna atakaye kuheshimu hata ufanyeje!
 
KWANZA KABISA, wafuasi wa CCM watambue na kukubali kuwa chama chao ambacho ni chama dola kimeunda na kulea mfumo wa kiimla (authoritarian) ambao una kasoro za msingi zilizoleta madhara makubwa sana kwa taifa na wananchi kwa ujumla. Ni mfumo ambao umetumika kuongoza nchi hii tangu awamu ya kwanza. Muda wote huo umekuwa ukitegemea utashi wa mtu mmoja, Rais, na kundi lake (inner circle). Mtu mmoja katika kiti cha uRais wa JMT (na uenyekiti wa CCM) amekuwa na mamlaka yote juu la nchi na vyote vilivyomo absolute power.

Ni kukosa uelewa au hila kutaka kulinganisha CCM na vyama huru vya siasa.

Rais (wa CCM) akiwa mwema na mzalendo kwa nchi yake kama alivyokuwa JKN (Nyerere) - benevolent dictator - wananchi wanakuwa na amani na kushiriki shughuli za maendeleo kwa juhudi kubwa. Rais akiruhusu utawala wa sheria na uwazi kama awamu za pili, tatu na nne, angalau watu wanaongea, taasisi zinafanya kazi na taarifa muhimu zinasambaa kiasi chake. Rais akiamua kupuuza katiba, kupuuza utawala wa sheria, kuzuia uwazi na kutawala kwa hofu, vitisho, mateso, udhalilishaji, hata mauaji kwa kutumia vikundi vya mauaji (hit squads), nchi inaingia gizani, unafiki, uchawa, na ujinga (idiocy) vinatamalaki. Hizo ni awamu za 5 & 6.

Endapo, wafuasi wa CCM hawataona hayo kuhusu chama hicho na kukimbilia kujificha kwenye udini, muungano, jinsia, watu fulani fulani (individuals), CHADEMA, n.k., hakika safari itakuwa ndefu sana kuelekea kwenye ufumbuzi.
 
Hakuna sehemu CCM itakwepa hili
Tumefika hapa kwasababu ya CCM
Kila wanayofanya na wanayofikiria kufanya ni kusalia madarakani
Kwasababu tuu inajulikana siku wakikubali mabadiliko ndoutakua mwanzo wa kulipia Yale waliyosababisha ndani ya miaka zaidi ya sitini kwenye nchi ya Tanganyika
 

Nadhani unatazama upande mmoja tu wa sarafu kwa sababu kumbuka Nyerere alipata upinzani mkubwa sana, tena naweza sema ni rais alokoswa koswa sana kupinduliwa kuliko marais wrngine wote. Toka anaapishwa hadi anastaafu ilikuwa sii.shwari.hata kidogo.

Kwa njia za kipekee kabisa Nyerere (dictatorship) aliweza kukomesha Udini na Ukabila ambao ulikuwa ndio Siasa za wakati wake. Aliweza kupambana na walopinga UJAMAA kwa maneno na vitendo toka (1967 - 1984). Haikuwankazi ndogo hata kidogo ilihitaji ujasiri usokuwa na huruma. Baada yake ndio tukashindwa kuendeleza alotuachia. ( Marekebisho ya Katiba 1984) Tukaingizwa shimo la chewa.

2015 Akaja Magufuli ambaye pia alikuwa Dikteta mwema (mtazamo wangu) lakini nae alikutana na Upinzani mkubwa sana mapema tu nje ya chama chake na ndani ya Chama Chake. Sababu kubwa haikuwa Itikadi wala sera zake bali Kiti alichokalia! Mwisho wake sote tunaujua.

Mimi naamini tatizo linaanza na sisi Wenyewe tumepoteza thamani UTU wetu na UZALENDO kwa Taifa. Kumbuka hawa viongozi wote wanatoka miongoni mwetu.

Nina hakika hata wewe unawajua baadhi ya viongozi ambao kablanya madaraka walikuwa karibu na wewe, lakini baada tu ya kupata madaraka hayo walikutenga.

Pengine hata simu yako hapokei tena, umegeuzwa mzigo hata kama kutaki msaada wowote toka kwake. Mimi naamini katika uhalisia huu ( Money and Power) hata akiingia Tundu Lissu madarakani hatatofautiana na viongozi wengine kwa sababu sote NDIVYO TULIVYO.

Nakumbuka Bashite amewahi kusema kitu kama hiki ya kwamba "Hawa wooote wanaopiga kelele ni kwa sababu hawajashika madaraka lakini siku wakiyashika watageuka na wao kama sisi"
Hotuba hiyo ilinipa picha ya Waziri wa ndani alokuwa Chadema leo yupo CCM utadhani sio yule alokuwa Chadema. Tumepoteza UTU kwa kupigania vyeo na maslahi Binafsi.
 
Tumefika hapa baada ya familia kukosa malezi yenye utu na maadili kuanzia nyumbani shuleni hadi makazini
 
Yaani hawa kwa vile wamewaua cdm wanahofu wasije kugeuziwa kibao

..wamewauwa kwanza.

..halafu ndio wameanza kuogopa kugeuziwa kibao.

..sasa jiulize kwanini waliwauwa wenzao?

..Katiba Mpya na bora haitaruhusu kulipiziana visasi, na kuchukua sheria mkononi.
 
Kwa hiyo wewe kujitoa kwa wadau wa UKAWA na taasisi nyingine unaamini Katiba ile Pendekezwa ndio ilipata maamuzi halali kabisa ya Bunge lile?

Umewahi wasikia Mzee Warioba na hata Polepole wakizungumzia Katiba Pendekezwa! Umewahi wasikia Wananchi wakizungumzia Katiba Pendekezwa dhidi ya Rasimu ya Katiba? Mimi naamini Bunge lile halikufikia muafaka na hata jana Prof. Tibaijuka kazungumzia.

Yawezekana mimi nina mitazamo tofauti sana na watu wengi hapa na hainishangazi kwa sababu hata zamani nilipokuwa hapa nilipitia Upinzani mkubwa kwa sababu watu wanazumgumza hoja zao kwa hisia za UCHAMA ilihali mimi natazama Uhalisia.
 
Marekani katika siasa zake husema wazi Russia ni Adui zao, wamewahi kuuana? Au kwako wewe Uadui ni vita tu! Hata
Najuwa wewe ni mtu mbishi.
Basi tutajie nchi yoyote yenye vyama pinzani wanaoitana kuwa ni vyama rafiki.

Mkuu 'Mkandara' wewe unajulikana siku zote msimamo wako upo wapi katika haya maswala ya Tanzania. Huna tofauti kubwa sana na 'zealots' wengi humu kama akina Ritz, BIG SHOWW na wengine.
Tofauti yako ni kuwa huwi bayana kama wao. Unajaribu kila uwezavyo kufunika maana ya maandishi yako uonekane upo balanced.; kama utumiaji wa maneno kama "UTU" niliyoyanyanyua hapo mwanzo kabisa.

Kwa ufupi, watu wa aina yako ndio hatari zaidi ya hao wanaojitokeza waziwazi kama hao niliowataja hapo juu.

Sasa wewe nieleze uhasama huu utatatua vipi hali yetu hii inayotukabili, huku watu kama wewe mnafunikafunika uwazi wenu usijulikane.

Halafu unauliza na swali kabisa: Eti "Tumefikafikaje hapa tulipo"?

Kwani hujui?
 
..wamewauwa kwanza.

..halafu ndio wameanza kuogopa kugeuziwa kibao.

..sasa jiulize kwanini waliwauwa wenzao?

..Katiba Mpya na bora haitaruhusu kulipiziana visasi, na kuchukua sheria mkononi.
Mimi nafikiri tuachane kabisa sasa na hili swala la Katiba, ambalo ni wazi Samia na Genge lake wameamua hawawezi kuruhusu bila ya shurti ambayo inaweza kuwa ni ya kuuana.
Jitihada sasa ziwe kuinyanyua Tanganyika.

Muungano na Zanzibar kwa hali tuliyopitia sasa sioni huo muungano ukiwa tulivu.

Muungano umetufikisha pabaya sana, sioni uhitaji wa huu muungan

Sikumbuki kuwahi kuusema muungano huu kwa haya maneno niliyotumia leo.
Kwa hiyo nitajiwekea kumbukumbu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…