Mzee unaijua miaka 200? Unajua miaka 70 tu nyuma Marekani weusi walikuwa hawapigi kura? Unajua miaka 40 nyuma mtu hakuweza kuongelea vyama vingi Tz, unajua miaka 50 nyuma Tz kukosoa utawala waziwazi haikuweza hata kufikirika? Unajua miaka si zaidi ya 70 iliyopita Hatukujua hata wakoloni wataondoka? Ramli yako ya miaka 200 kaipige tena. Tupo katika zama tofauti, zama za serikali za Afrika kupoteza ukiritimba wa kusambaza habari kwa umma ambapo sasa mtu binafsi na simu yake tu anaweza wasambazia habari maelfu ya watu ndani ya sekunde moja tu. Miaka 200 ni mingi saaaaana