Tumeanza mahusiano...

Tumeanza mahusiano...

sunv

Member
Joined
May 19, 2020
Posts
44
Reaction score
33
Habari za muda huu,

Wapendwa nina mchumba wangu tumeanza mahusiano tangu mwaka 2014, yeye akiwa darasa la saba mimi nikiwa form one mpaka leo hii yeye yupo chuo na mimi nipo chuo kikuu bado tuna mahusiano, lakini siku moja nilijaribu kushika simu yake nikakuta kuna voice note ambazo ametumiwa na mwanaume mwingine.

Alipogundua nimeona alilia sana akaomba nimsamehe, basi nikapotezea lakini juzi kati aliniambia nisajiri kadi ya bank kwaajili ya kutunza hela ambazo zitatusaidia kuanzisha maisha, mpaka sasa ameshaweka kiasi fulan mimi sijaweka nafsi inanituma kuzitumia pesa ambazo ameweka yeye.

Je ni sahihi kufanya hivyo?

Naombeni ushauri wenu
 
Yaani unataka kuzitumia hizo pesa kama kulipa kisasi ama wataka kuzitumia kisha uzirudishe
 
Yaani unataka kuzitumia hizo pesa kama kulipa kisasi ama wataka kuzitumia kisha uzirudishe
Naona kama badae atabadirika tena sasa nataka nizitumie kama kulipa kisasi
 
Naona kama badae atabadirika tena sasa nataka nizitumie kama kulipa kisasi
Inaonesha huna tena mpango nae.... usilipize kisasi, be a man muambie ukweli na umuachie pesa zake zije zimsaidie mwenyewe baadae
 
Kama unaogopa kuwa atabadilika mtunzie zake usiweke zako kama humuamini ila zake pia usitumie kabisa kilio cha mwanamke utalipa siku moja, Pia sikushauri umuamini
 
Inaonesha huna tena mpango nae.... usilipize kisasi, be a man muambie ukweli na umuachie pesa zake zije zimsaidie mwenyewe baadae
Me nampenda sana, make najua ni wapi tumetoka sasa kuna wakati roho fulan inanishawishi nizitumie. Naomba mnishauri jaman
 
Naona kama badae atabadirika tena sasa nataka nizitumie kama kulipa kisasi
Ukitaka kulipa kisasi basi chimba makaburi mawili, lako na la huyo umfanyiae kisasi.

Zaidi ya hapo, kisasi cha mwanamke hakinaga kipimo, yeye akikufanyia hataangalia ni ubaya kiasi gani uliomtendea, kisasi cha buku kitakugharimu milioni.

Sasa usitumie kisasi kama kigezo cha kukidhi njaa ndugu, kama huna hela sema tu.
 
Ukitaka kulipa kisasi basi chimba makaburi mawili, lako na la huyo umfanyiae kisasi.

Zaidi ya hapo, kisasi cha mwanamke hakinaga kipimo, yeye akikufanyia hataangalia ni ubaya kiasi gani uliomtendea, kisasi cha buku kitakugharimu milioni.

Sasa usitumie kisasi kama kigezo cha kukidhi njaa ndugu, kama huna hela sema tu.
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Back
Top Bottom