Natafuta Ajira
JF-Expert Member
- Mar 25, 2020
- 4,418
- 9,806
Nimekua pamoja na huyu binti kwa miaka miwili na ziada. Marafiki na baadhi ya ndugu kila upande wanajua mahusiano yetu. Kilichopelekea kuachana nae ni hali yangu duni kiuchumi. Kwa kipindi cha takribani mwaka na nusu sasa napitia hali ngumu sana.
Kwa mwanaume ni ngumu kudumisha mahusiano kama haupo stable kiuchumi, sio binti muomba hela akiniomba basi najua kabisa huyu ana shida kweli tatizo hata hizo mara chache anapoomba msaada wangu nakua sina kitu.
Baada ya kujitafakari nimeona ni bora tuachane uenda akakakutana na mwingine mwenye hali nzuri. Sijamuambia sababu nipo broke nimetafuta sababu nyingine. Kama kawaida kaniaga kwa maneno makali kidogo lakini nilishajiandaa kwa ilo.
Vijana wenzangu usiwe commited kwenye mahusiano kama bado uchumi unayumba. Hata kama mwanamke anakupenda kwa hali yako hautakuwa sawa kisaikolojia. Siku ya pili sasa bado najilaumu kwa nilichokifanya lakini maisha lazima yaendelee. Nimelazimika kumuacha kwa sababu nampenda.
Kwa mwanaume ni ngumu kudumisha mahusiano kama haupo stable kiuchumi, sio binti muomba hela akiniomba basi najua kabisa huyu ana shida kweli tatizo hata hizo mara chache anapoomba msaada wangu nakua sina kitu.
Baada ya kujitafakari nimeona ni bora tuachane uenda akakakutana na mwingine mwenye hali nzuri. Sijamuambia sababu nipo broke nimetafuta sababu nyingine. Kama kawaida kaniaga kwa maneno makali kidogo lakini nilishajiandaa kwa ilo.
Vijana wenzangu usiwe commited kwenye mahusiano kama bado uchumi unayumba. Hata kama mwanamke anakupenda kwa hali yako hautakuwa sawa kisaikolojia. Siku ya pili sasa bado najilaumu kwa nilichokifanya lakini maisha lazima yaendelee. Nimelazimika kumuacha kwa sababu nampenda.