Lord Denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 23,494
- 57,869
Heri ya Mwaka Mpya kwenu wadau!
Natumai wote tu salama na tunaendelea vyema na majukumu yetu.
Mwaka 2020 umeshaingia. Na kila mtu anajua kuwa mwaka huu ni wa Uchaguzi Mkuu ambapo Watanzania wanaenda kuchagua viongozi wao Wakuu kwa ajili ya kuwaongoza.
Lakini pamoja na kuwa ni mwaka wa uchaguzi , tumekaribishwa na ripoti nzito ya IMF inayoelezea hali ya ukuaji wa kiuchumi hapa Tanzania.
Kwa watu wenye akili na wanaotafakari vizuri hiki ndiyo kilikuwa kipindi murua kwa Watanzania kujadili kwa kina bila kificho juu ya kwa nini tumefika hapa na nini kifanyike ili tutoke hapa.
Imenisikitisha sana kuona jukwaa hili limeanza kuwa mfu kiasi hiki kiasi kwamba pamoja na ripoti hii kuonesha hali si shwari hapa kwetu kwenye ukuaji wa uchumi still watu hawajadili jambo hili la msingi na wamekalia vijembe vya CCM na CHADEMA pamoja na nyimbo za kusifu na kuabudu
Nchi haishtuki, viongozi hawashtuki, Wananchi ndio wamelala usingizi wa pono pamoja na hali ya uchumi kuwa mbaya sana na dalili zote kuwa wazi.
Wiki hii kuna habari za kiwanda cha tiles Chalinze kufungwa kutokana na Kukosa biashara, Vilevile kwa kipindi kirefu kuna Habari nyingi za biashara mbalimbali kufungwa, watu kupunguzwa kazini na mambo mengi yanayoonesha uchumi wetu hauko sawa ila watu wamelala kila siku kuimba nyimbo za kusifu na kuabudu pamoja na vijembe vya vyama.
Kwa hali inayoendelea sasa kiuchumi Tanzania ilipaswa kila siku watu kutafakari na kujadili hali ya kiuchumi kiasi kwamba hata watawala watashtuka ila wapi watu wamekalia vijembe na kusifu na kuabudu.
Simshangai aliyesema Africa is a dark continent.
Tanzania tulisharogwa kitambo sana.
Natumai wote tu salama na tunaendelea vyema na majukumu yetu.
Mwaka 2020 umeshaingia. Na kila mtu anajua kuwa mwaka huu ni wa Uchaguzi Mkuu ambapo Watanzania wanaenda kuchagua viongozi wao Wakuu kwa ajili ya kuwaongoza.
Lakini pamoja na kuwa ni mwaka wa uchaguzi , tumekaribishwa na ripoti nzito ya IMF inayoelezea hali ya ukuaji wa kiuchumi hapa Tanzania.
Kwa watu wenye akili na wanaotafakari vizuri hiki ndiyo kilikuwa kipindi murua kwa Watanzania kujadili kwa kina bila kificho juu ya kwa nini tumefika hapa na nini kifanyike ili tutoke hapa.
Imenisikitisha sana kuona jukwaa hili limeanza kuwa mfu kiasi hiki kiasi kwamba pamoja na ripoti hii kuonesha hali si shwari hapa kwetu kwenye ukuaji wa uchumi still watu hawajadili jambo hili la msingi na wamekalia vijembe vya CCM na CHADEMA pamoja na nyimbo za kusifu na kuabudu
Nchi haishtuki, viongozi hawashtuki, Wananchi ndio wamelala usingizi wa pono pamoja na hali ya uchumi kuwa mbaya sana na dalili zote kuwa wazi.
Wiki hii kuna habari za kiwanda cha tiles Chalinze kufungwa kutokana na Kukosa biashara, Vilevile kwa kipindi kirefu kuna Habari nyingi za biashara mbalimbali kufungwa, watu kupunguzwa kazini na mambo mengi yanayoonesha uchumi wetu hauko sawa ila watu wamelala kila siku kuimba nyimbo za kusifu na kuabudu pamoja na vijembe vya vyama.
Kwa hali inayoendelea sasa kiuchumi Tanzania ilipaswa kila siku watu kutafakari na kujadili hali ya kiuchumi kiasi kwamba hata watawala watashtuka ila wapi watu wamekalia vijembe na kusifu na kuabudu.
Simshangai aliyesema Africa is a dark continent.
Tanzania tulisharogwa kitambo sana.

