Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 69,594
- 123,103
Sio jukumu langu kukuwekea ripoti ya IMF , unaweza itafuta mitandaoni ndugu
Mkuu nimependa sana hii mada yako. Iko hivi, kwa sasa hivi majukwaa rasmi ya kuongea hayo mambo kwa uwazi hayapo, na huku jukwaani mada zinazoanzishwa Ni hizi hizi unazolalamikia. Badala ya kulaumu, anzulisha ww mada yenye msingi, sisi washereheshaji tupo. Toa vifungu kwenye hiyo ripoti vinavyoonyesha hayo matatizo tujadili. Wote tunajua kusoma vitabu vitakatifu, mbona tunaenda kwenye nyumba za ibada na kusubiri viongozi wadadavue?
Mimi bila hata ripoti ya IMF haya yanayotokea niliyajua tu ni lazima yatokee. Nilipoona tu rais anaua mifumo yote ya ushindani na kuanza kuleta mifumo ya ukiritimba wa dola, nilijua fika hatima itakuwa ni ipi. Kibaya zaidi amefanikiwa kuziba midomo vyombo vya habari ili afiche haya yatakayotokokea. Ukiona mtu anajiita msafi lakini hataki kukaa kwenye mwanga, anakimbilia kwenye giza, jua hapo yajayo yanafurahisha. Nyerere pia alitufungia kwenye box tukabaki tunamsifu yeye tu. Siku ametuachia tukatoka ndani ya box, kila mtu alikuwa anatembea na viraka.
