Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi (NEC), kwanini utaratibu huu usiwaguse pia Wagombea Ubunge na Udiwani?

LESIRIAMU

JF-Expert Member
Feb 12, 2008
8,721
13,959
Kuna maneno nimemsikia katibu akiongea wakati Tundu Lissu anakabidhiwa fomu, nikaona ni busara ya hali ya juu sana ambayo hata Madiwani na watia nia Ubunge wangepewa hiyo fursa.

Nimemsikia akisema wakajaze fomu na wana ruhusiwa kurudi tume siku mbili au tatu kabla ya kuzirudisha ili zikakaguliwe kama zimejazwa sawa au kunahitajika marekebisho.

Hii ni busara maana sioni sababu ya kutegana ili kuenguana kwenye kinyang'anyiro.

Tumezoea wagombea ubunge na udiwani wakitegwa kwenye kukosea kujaza fomu ili waenguluwe. Kwanini hili pia lisiende huko ili fomu za wabunge/ madiwani zilizokosewa nazo zifanyiwe marekebisho? Hii ndiyo tume tunayotaka.
 
Huo ni mtego wa kuengua wagombea. Watasingizia kuwa waliwakaribisha kurekebesha makosa hawakufanya hivyo au walifanya hivyo wakaendelea kukosea. Wanatafuta sababu ya kuhalalisha kitendo hicho. "I smell a very big rat rotting in this statement".
 
Kuna maneno nimemsikia katibu akiongea wakati Tundu Lissu anakabidhiwa fomu, nikaona ni busara ya hali ya juu sana ambayo hata Madiwani na watia nia Ubunge wangepewa hiyo fursa.

Nimemsikia akisema wakajaze fomu na wana ruhusiwa kurudi tume siku mbili au tatu kabla ya kuzirudisha ili zikakaguliwe kama zimejazwa sawa au kunahitajika marekebisho.

Hii ni busara maana sioni sababu ya kutegana ili kuenguana kwenye kinyang'anyiro.

Tumezoea wagombea ubunge na udiwani wakitegwa kwenye kukosea kujaza fomu ili waenguluwe. Kwanini hili pia lisiende huko ili fomu za wabunge/ madiwani zilizokosewa nazo zifanyiwe marekebisho? Hii ndiyo tume tunayotaka.
 
Back
Top Bottom