EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
HUKU CCM ikiwa imefungua milango kwa wanachama wake kujitokeza kuchukua fomu juzi za kurithi ‘viatu' Rostam Aziz, wanachama watatu wa Chadema wamejitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo kwenye uchaguzi mdogo Jimbo la Igunga, mkoani Tabora.
Mkurugenzi wa Sera na Utafiti wa Chadema, Waitara Mwikabwe, alisema kuna kila dalili wanachama wengi zaidi watajitokeza kabla ya siku ya mwisho ambayo ni Agosti 16, saa 10:00 jioni.
Waitara alisema wanachama waliojitokeza jana ni Gideon Kwandu, Anwari Luhumbiza Kashaga na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chadema, Erasto Tumbo.
Alisema milango bado ipo wazi kwa mwanachama yeyote mwenye nia ya kugombea na kwamba, gharama ya fomu ni Sh50,000.
Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Erasto Tumbo, ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Kisesa, wilayani Meatu, kwa tiketi ya UDP, alisema ameguswa na msukumo wa wananchi wa Igunga waliomwomba kugombea nafasi hiyo.
Kwa upande wa CCM, ikiwa ni siku ya pili tangu kuanza zoezi hilo, wanachama wanne wamejitokeza kuchukua fomu.Katibu wa CCM Wilaya ya Igunga, Neema Adamu, alisema licha ya Amina Said Fundikira aliyechukua fomu juzi, wengine waliojitokeza ni Shamshu Ibrahim, Adam Kamange na Ngasa George.
Adam alisema mwisho wa wanachama wanaotaka kuchukua fomu ni Jumamosi ijayo, hivyo aliwataka wenye nia ya kufanya hivyo kujitokeza mapema.
Kwa upande wa CUF, taarifa zilizopatikana mjini Igunga zinadai aliyejitokeza ni aliyewahi kuwania ubunge na kushindwa na Rostam kwenye uchaguzi uliopita. "Ni kweli nagombea tena chama changu kimenipendekeza, mwisho wa wiki baraza kuu watatoa taarifa," alisema Lucas Mahona.
Source: Mwananchi
Mkurugenzi wa Sera na Utafiti wa Chadema, Waitara Mwikabwe, alisema kuna kila dalili wanachama wengi zaidi watajitokeza kabla ya siku ya mwisho ambayo ni Agosti 16, saa 10:00 jioni.
Waitara alisema wanachama waliojitokeza jana ni Gideon Kwandu, Anwari Luhumbiza Kashaga na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chadema, Erasto Tumbo.
Alisema milango bado ipo wazi kwa mwanachama yeyote mwenye nia ya kugombea na kwamba, gharama ya fomu ni Sh50,000.
Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Erasto Tumbo, ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Kisesa, wilayani Meatu, kwa tiketi ya UDP, alisema ameguswa na msukumo wa wananchi wa Igunga waliomwomba kugombea nafasi hiyo.
Kwa upande wa CCM, ikiwa ni siku ya pili tangu kuanza zoezi hilo, wanachama wanne wamejitokeza kuchukua fomu.Katibu wa CCM Wilaya ya Igunga, Neema Adamu, alisema licha ya Amina Said Fundikira aliyechukua fomu juzi, wengine waliojitokeza ni Shamshu Ibrahim, Adam Kamange na Ngasa George.
Adam alisema mwisho wa wanachama wanaotaka kuchukua fomu ni Jumamosi ijayo, hivyo aliwataka wenye nia ya kufanya hivyo kujitokeza mapema.
Kwa upande wa CUF, taarifa zilizopatikana mjini Igunga zinadai aliyejitokeza ni aliyewahi kuwania ubunge na kushindwa na Rostam kwenye uchaguzi uliopita. "Ni kweli nagombea tena chama changu kimenipendekeza, mwisho wa wiki baraza kuu watatoa taarifa," alisema Lucas Mahona.
Source: Mwananchi