Bunchari
JF-Expert Member
- Aug 31, 2017
- 695
- 878
Nyakati fulani kitambo nikiwa kijana mdogo niliwai kuwa ktk mahusiano na binti niliempenda kwa dhati mpaka kufikiria kufunga nae pingu za maisha pale ambapo Mwenyezi Mungu akiniimalisha kiuchumi,nilipokua nikiishi na mpenzi wang yule ni kama km 360 tukiwasiliana kwanjia ya simu na mitandao ya kijamii.Kadri siku zilivyokwenda mchumba akaanza kubadilika nikimpigia simu ipo busy anitafuti mpaka nimtafute,siku moja nikaamua kufunga safari kumfata bahati mbaya hatukufanikiwa kuonana baada ya kugoma kupokea simu zangu nikaamua kurudi nilipotoka,siku moja natizama facebook nikakutana na picha ya jamaa na caption kibao "may babe","sweetie","mume" n.k huo ndio ukawa mwisho wetu.