Tuliowahi kufukuzwa kazi tukutane tupeane experience

Kuna wafanyakazi airport wamefukuzwa Kazi baada ya kupokea asante kwa kuhudumia abiria vizuri.Unamfukuza Kazi mtu kisha kapewa elf 5 kama Asante.Uonevu mtupu halafu kuna mijizi inapiga mamilioni inahamishwa tu wizara au halmashauri
 
Mkuu uko sahihi sana, usipojipanga unaweza fanya nini vile.............
 

We are hiring
 

Kweli wewe mkaruka Mkaruka
 
Amemaanisha hiyo ultavet haikuwa mtego? Iliishaje hii ishu yako pale Lead?
Utravet haikuwa mtego,mm sikwenda kwa kuwa tayari nilikuwa na mkataba na LEAD PROJECT,na Niko govt tayr,so nikaamua nimwambie ukweli Yule manager wa utravet ,nakumbuka email yake ilianza kwa jina la laagie.somethin hiv,so nikaamua kum connect jamaa angu aliitwa somebody msoka,from tanga.manager wa utravet akaniambia jamaa yuko vizur nikamwambia yes,akasema mwambie atume maombi kwa email,Ila huyu tutampiga interview tukiona anafaa basi tutampa offer,nikampa contact jamaa angu awasiliane nae,ofcoz jamaa alienda wakampiga interview baadae ,akaenda Nairobi Kenya kwa 2weeks seminar.alipiga nao kazi.
 
Niliacha kazi mwaka 2018 mpaka leo najuta Kwa kweli naona bora nisinge acha kazi.Sijui wenzangu mnatumia mbinu gan kupata kazi Kwa haraka
hakikisha unaongea vizuri na walinzi wa hiyo kampuni/ofisi wakukonnect na HR, then ukipata chance ipambanie.
 
Huyo boss ni kama boss wangu wa sasa...

Nipo namlia timing tuu sku akijichanganya lazima nimtie hasara...
 
miaka kumi na ushee iliyopita....
Nilikiwa kwenye ajira kwenye kampuni niliyufanyia kazi kwa zaidi ya miaka nane katika vitengo tofauti tofauti kwa ufanisi mzuri tuu,sasa nikiwa mkoani tukaitwa Makao makuu kwa ajili ya kujifunza system mpya ya kazi, tulivyomaliza wakati narudi kituo changu wakati tunakabidhiana kazi na msaidizi wangu nikagundua upotevu wa vifaa ambavyo thamani yake ilikuwa ni kama milioni 2 hivi,nilikuwa na uwezo wa kulificha hili au kulimaliza kichinichini ila baada ya kugundua upotevu ule haukumhusisha msaidizi wangu nikaamua kuliripoti makao makuu kwa hatua za ziada,ikiwa ni pamoja na kuwaelezea ninavyohisi upotevu umetokea na vielelezo ambavyo wangevitumia ilikuwa rahisi kubaini upotevu huu,baada ya muda alitumwa mkaguzi wa ambae alikuja kuangalia lilivyotoea,(mbwa sana yule mhindi)..alinilazimisha kuandika kuwa kosa amelitenda msaidizi wangu ili achukuliwe hatua,nilimwambia siko tayari kuchuma hiyo dhambi na kama anadhani kosa lipo basi nitalibeba mimi,story ni ndefu ila baadae nlikuja kuitwa kwa mahojiano yaliyochukua zaidi ya siku tatu na waliokuwa wanasimamia wakanikandamiza kuwa kosa limetendeka chini yangu hivyo ni kosa langu, (wapuuzi wale walikuwa wanafanya kazi kwa kulamba lamba makalio ya wazungu ili waonekane wanajua wanachokifanya)baada ya kuona mwelekeo niliamua kufuatilia upotevu huo kivyangu bila kushirikisha ofisi ambapo nilifanikiwa kuwanasha waliofanya uhalifu huo na kuwafikisha mahakamani na wakahukumiwa kifungo,hili nililifanya bila kutoa taarifa ofisini,hatimae baada ya muda nilipewa barua ya kufukuzwa kazi bila ya kujua kuwa nilishalifanyia kazi na kufanikiwa kuwakamata wahalifu waliohusika, niliipokea barua kwa furaha kiasi kwamba hata walioniletea barua walibaki wananishangaa,niliwakabidhi pesa ya ofisi kama milioni 35 ambayo ningeweza kupotea nayo,nilivyomalizana nao nikaenda kufungua kesi CMA,kule wakaniwahi wakamrubuni wakili wangu akawa hahudhurii mahakamani mwishoe nikashindwa,nikatafuta wakili mwingine nika appeal,huyu walimfuata kumhonga wakashindwa, mlolongo ulikuwa mrefu lakini hatimae nilishinda na walinilipa stahiki yangu tosha kabisa,nashukuru wakati kesi inaendelea nilianza kujishughulisha na biashara ndogo ndogo na zilifanikiwa kwa kiasi kizuri tuu, wale wapuuzi walionikandamiza kuna wengine nakutana nao mitaani wamepauka hadi meno, niliifanya kazi kwa moyo sana lakini baada ya tukio hili nilichana vyeti vyangu vyotena kuvitia moto ili nisikumbuke tena kutafuta ajira... ...
 
Mkuu hongera khaaa!

We kabila gani?
 
K ikakuchoma
 
Sasa alikutupia jini la wizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…