Sasa wewe unaona hii mada inafaa kujadiliwa hapa JF kweli? embu soma mada za JF ya mwaka 2006 na 2007 uone!! Halafu linganisha na mada zinazoletwa hapa 2012!! Utanielewa vizuri.
wee amu weeeee ngoja uolewe utaona.
binafsi huwa naamini katika kuwatembelea wazazi hasa msimu wa sikukuu ili wafurahi, muongee na ndugu zako kwa kina na kisha kuombeana. Ikumbukwe kwamba watoto ndio wanaopaswa kufwata wazazi na si wazazi wafwate watoto.
ni lazima kwangu x-mass na mwaka mpya nile ukweni kwangu ( hapa nnajiandaa tarehe 23 saa 11 alfajiri ngoma inanyuka iringaa)
ni lazima sikuu ya pasaka nile kwetu hivyo alhamis kuu ngoma hunyanyukaa kwetuuuuu nikiwa na kids na baba yao. hiyo ni lazima.
kuna miaka ambayo hupenda kuwaalika watu kwangu, nakumbuka kuna mwaka niliwaita wakwe zangu kula x-mass na new yr kwangu. na hapa niliita mawifi shem na baba na mama pamoja na wajukuu. duh ilikuwa bonge la raha ya ajabu manake utafikiri kuna sherehe lol! inapendeza sana kuona mtu anatoka kwake kuja kwako kukusalimia na familia yake mnakaa pamoja kwa wiki 2 hivi ni kula na kunywa tu. sitokaa nisahau. ilikuwa raha sana sana.
pia kuna pasaka niliwaalika baba na mama yangu kwangu but i was realy disappointed as wazazi wa kichaga huwa hawalali kwa mtoto wa kike hata ardhi ipasuke. sikupenda manake waliniambia tena kwa amri "SISI NI WAZAZI HATUTOKI KWETU KULA SIKUKUU KWA MTOTO BALI MTOTO NDO ATUFWATE SISI " ila nilipouliza kisa nn hasa manake mbona kwa kaka wanaendaga?? nikajibiwa yule ni mtoto wa kiume ila kwako wewe sio kwetu huko ni ukweni hatupaswi kupazoea. ..........arrrrgggggggggghhhhhhhhhh yaani nilimjibu tu hubby twende manake ishakuwa tabu.
watoto mnaruhusiwa kwenda kwa baba zenu kula sikukuu. mimi baba kubebana na mke wangu na wanangu eti naenda kwa baba kula sikukuu si ata watoto wangu wananishangaa. utaratibu wangu ni kwamba watoto wakifunga shule wanaenda kusalimia kwa babu / ujombani n.k; sikukuu zikikaribia wote lazima warudi.
Tatizo lenu mnafikiri kila mwana JF yuko Dar kwenye mji wa mavurugu! Wengine tuko kwenye miji iliyotulia kama vile Mwanza, Arusha etc.Inapendeza ni mzuri kurudi homie na watoto kwenda kujumuika na ndugu kula sikuu unawaonyesha na wanao mto ukitiyirika maji kuwa ukiwa mdogo unasoma ulikua unakuja kuoga hapo na mafrendie wa utoto maisha ni kupanga na kuchagua mwenye kwao aende akawashe kibatari nyama za pori inakua bomba mnaowaiga wazungu nyie kaukeni dar kimpango wenu na vurugu za mji huu heeeeeee.
Kwani walikuruhusu uende kuishi na huyo mwanamume ili iweje? Mi mbona kwangu mama mkwe anakuja na sioni tatizo lolote!
kwa taarifa yako hao hao waliokuwa wanachangia miaka hiyo baadhi yao ndio hao hao wanachangia sasa. istoshe kama za siku hizi huzipend basi ondoka jamvini just like that.
pia unategemea kwa kuandika haya maneno yako ndipo utakapotubadilisha mtazamo wa kufikiri kwetu?? FYI shule haimfanyi mtu kuwa na akili bali humwongezea wigo na upana wa kufikiri tu. akili tulishazaliwa nazo mkuu huna uwezo wa kutufanya tuwe nazo tena.
Sawa mama nimekupata. Endelea kutuelimisha. Tunafarijika sana tunaposoma michango yako yenye busara.
yaani hiyo kwangu mwaka wa 11 huu mama yangu hajawah kuja kwangu akalala. atasalimia na kuondoka.
yaani alale kabisa ama baba si mbingu ingefunguka mkuu.
walijua wanaipeleka nikapigwe mpera sawa lkn sio kwenye upeo wa macho yao atii. nimejikuta kwamba hata nikiwa mjamzito siwez kwenda kwetu naona aibu baba atajua nilifanya so huwa nauchuna na kuonana na maza hadi nijifungue.
Jamani jikwamue kwenye mateso ya kijinsia!
We umekuja na hoja ambayo naweza kukubaliana nayo japo si kwa asilimia 100; kuhesabiwa!!!
Waisrael wanajuana idadi ulimwengu mzima lakini hawalazimishani kwenda kubanana nchini mwao Israel.
yaani ktk kitu ambacho ningeweza kukibadili hiki ni namba moja. hivi Lisa unafikiri wanangu mm hawana hamu ya kumwona bibi ama babu yao hapa nyumbani kwao?? kwann walazimike tu kwenda kwao?? mm natamani siku itokee baba yangu aje alale hapa kwangu acheze na wajukuu nitoke job nimkute tupige story jamani mbona wanatunyanyasa sana na huuuu ukwe??
Ndio maana wao ni Waisrael na sisi sio Waisrael. Hatulazimishwi kufanya wayafanyayo wao ha hakika hatuwalazimishi kufuata ya kwetu.
Karibu mlimani mkuu wangu.
gfsomnwin , hoyo haitakaa ibadilike, mm nimeolewa uchagani , baba na mama mkwe huwa wanakuja na wanakaa kwangu, lakini mm wazazi wangu ni watu wa kanda ya ziwa, hata siku moja hawajawahi kuja kula na kulala kwangu na nina ndoa ya miaka 9 sasa. ila mm napenda msimamo wao, kuja kwako na kukaa, kula, kulala ukweni ni AIBU kubwa, yaani ninamaanisha kwao wameishiwa kiasi wameolewa na mtoto wao. hiyo ndiyo tafsiri yao.
- Ina maana wewe huna haki sawa kaka zako? Aibu gani??
gfsomnwin , hoyo haitakaa ibadilike, mm nimeolewa uchagani , baba na mama mkwe huwa wanakuja na wanakaa kwangu, lakini mm wazazi wangu ni watu wa kanda ya ziwa, hata siku moja hawajawahi kuja kula na kulala kwangu na nina ndoa ya miaka 9 sasa. ila mm napenda msimamo wao, kuja kwako na kukaa, kula, kulala ukweni ni AIBU kubwa, yaani ninamaanisha kwao wameishiwa kiasi wameolewa na mtoto wao. hiyo ndiyo tafsiri yao.
Naona hujanielewa! kwani kama wewe ni mzaliwa wa Bukoba; ukiamua kutembea Arusha au Dar nani anakukataza! Issue ni kubebana msimu wa sikukuu kwenda huko Kiziba / Buyango eti kula sikukuu. Ina maana siku zingine huwa unazuiliwa na nani kupeleka watoto wakapaone kwao.
Atakayewabariki Waisrael atabarikiwa; Atakayewadharau Waisrael atadharauliwa pia.... kwa mwaliko wa kuja kwenu naweza, lakini si kubeba familia nzima.
Wala sijisikii AIBU yoyote ila, kwa sababu hizo ni mila na Desturi zetu a wala hazitokuja kubadilika kamwe. Na nashukuru Mungu katika kugawiwa urith kila mtu kapata sawa na mwenzie haijalishi ni mwanaume au mwanamke. Baba amegawa sawa kwa sawa.