Tulificha siri kuiokoa serikali

Sungurampole

JF-Expert Member
Nov 17, 2007
984
205
Maneno haya manne yamekua maarufu kwa siku za karibuni. Leo nimeyasikia kutoka kwa Mh Lembeli, akiwa mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Ardhi, Mazingira (Fahamu 12.6.12)

Tumeyasikia kwa Mwakyembe na huenda hata Hosea angeulizwa angesema aliwasafisha Richmond ili kuiokoa serikali. Mh Lowassa amekua akisema aliwajibika ili kuiokoa serikali. Majuzi Waziri wetu 'mpya' wa Nishati alisema alipoenda TANESCO amekuta madudu ya kutisha ila hakutuambia ni yapi, naye huenda ni ili 'kuiokoa serikali'

Watanzania hii serikali wanayoiokoa ndio tuliweka madarakani na ndiyo tunayoipa mamlaka ya kutawala.

Tujiulize na tutafakari:

  • Je, ni sawa serikali yetu kutegemea kulindwa kwa viongozi wake kudanganya?
  • Hivi inakuaje kiongozi anadiriki kutuambia alificha ukweli?
  • Hivi ni kweli watanzania tumekufa ganzi au tumepofuka?
  • Na hao wanaosimamia maadili ya viongozi wanajisikiaji juu ya haya?
 
Ni kweli mkuu wa kaya anahusika kwa kiasi kikubwa sana, hilo linajulikana! Kama ingewekwa wazi Jk angetakiwa awe jela! Ndo maana wanaichafua chadema kwa sababu kama chadema wakikamata nchi Jk na Mkapa na Lowasa watapelekwa jela.
 
Ni kweli mkuu wa kaya anahusika kwa kiasi kikubwa sana, hilo linajulikana! Kama ingewekwa wazi Jk angetakiwa awe jela! Ndo maana wanaichafua chadema kwa sababu kama chadema wakikamata nchi Jk na Mkapa na Lowasa watapelekwa jela.

mi nataka waanze na KINANA
 
Dawa ni moja 2 nayo nikuipiga chini ccm, yote yatakua hadharani na wakamalizie maisha segerea. CHADEMA kaza buti, imebaki mkia 2 wameanza kutapatapa ccm
Tulishawapiga chini wakachachua, kote bara na visiwani, ushahidi tunao. Tuendelee kufanya maigizo haya?

Dawa ni 1 tu: TAHRIR SQUARE; full stop! Watanzania kama hamko tayari kukabiliana na hilo acheni kulalamika.
 
Dawa hapa tuhamasishe vijana kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kuru endapo likiletwa tukate ngebe za magamba wanavyosema vijana hawapigagi kura maana hawana zile kadi za kupigia kura.
 
Dawa hapa tuhamasishe vijana kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kuru endapo likiletwa tukate ngebe za magamba wanavyosema vijana hawapigagi kura maana hawana zile kadi za kupigia kura.

Wazo zuri sana. Wakati ukifika, tunatakiwa tuanze kuhamasisha kwenye familia, jirani, ofisini, jumuia hadi taifa. Halafu tunaringa sana wakati wa kampeni tukiwa na vitambulisho vyetu!
 
WAWEZA KUWADANGANYA WATU WOTE KWA WAKATI FULANI,ukafanikiwa hata kuwadanganya baadhi ya watu kwa wakati wote,lakini huwezi kuwadanganya watu wote wakati wote!
 
wanajidaganya watatawala milele! kiongozi wa ngazi za juu anadhani utawala ni wa chama kimoja mpaka aseme wapo milele! how dummy he is to say that? hakuna utawa unaodumu milele. hawa viongozi waongo watatia akili muda utakapofika.
 
Wazo zuri sana. Wakati ukifika, tunatakiwa tuanze kuhamasisha kwenye familia, jirani, ofisini, jumuia hadi taifa. Halafu tunaringa sana wakati wa kampeni tukiwa na vitambulisho vyetu!

Wakati uliokubalika ni sasa.
 
Hata serikali za mataifa makubwa yana siri ambazo zikijulikana zinaweza kuziangusha. Km. Uingereza na Marekani wangekuwa wanatoa idadi kamili ya wanajeshi wao waliokufa katika vita ambavyo havikuwa na umuhimu huko Iraq (kulikotokana na taarifa zisizo sahihi za kiintelejinsia), Afganistan, nk. Au matumizi/manunuzi yo yote ya kijeshi, Nina uhakika hata CDM au CUF au NCCR- zikitwaa madaraka kuna maeneo yatafanyika madudu ambayo yatakuwa ni hatari kwa serikali zao kama yatajulikana wazi. Hata vyama vya siasa vina siri ambazo zikijulikana, wanachama wangekosa imani navyo. HIVI NDIVYO ILIVYO.
 
Hakuna mtu muongo na mnafiki kama Lembeli, nishakutana naye mikutanoni kama mara mbili naamini ni aina ya watu ambao hawatufai katika Tanzania ijayo

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Umeunganisha unganisha ili upate ku "propagate" chuki. Unachoshindwa kuelewa kuwa kila waziri anapokula kiapo huwa anaapa kuwa atalinda siri za baraza la mawaziri ambayo ni serikali. Serikali ina siri nyingi sana na usitake kuwaaminisha watu vinginevyo.
 
Hata serikali za mataifa makubwa yana siri ambazo zikijulikana zinaweza kuziangusha. Km. Uingereza na Marekani wangekuwa wanatoa idadi kamili ya wanajeshi wao waliokufa katika vita ambavyo havikuwa na umuhimu huko Iraq (kulikotokana na taarifa zisizo sahihi za kiintelejinsia), Afganistan, nk. Au matumizi/manunuzi yo yote ya kijeshi, Nina uhakika hata CDM au CUF au NCCR- zikitwaa madaraka kuna maeneo yatafanyika madudu ambayo yatakuwa ni hatari kwa serikali zao kama yatajulikana wazi. Hata vyama vya siasa vina siri ambazo zikijulikana, wanachama wangekosa imani navyo. HIVI NDIVYO ILIVYO.
Asante Mkuu!
Kuna watoto humu wanafikiri kuendesha serikali ni kama kuendesha boda boda.

Toa siri zako at the expense of stability and tranquility.
 
Hivi Takukuru wanazisikia mawaziri hawa? na Polisi je, vipi mkuu wa nchi anashituka na haya maneno?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom