Tulichagua ovyo na sasa tunatendewa ovyo, Je, tukae kimya?

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Tunachagua kama vipofu, kisha tunalalama kama vichaa. Sasa tuamue: ama tuchague viongozi wetu kwa makini, au tukae kimya wakati wakitunyanyasa. Wachagua hovyo wasiwe wasema hovyo wakitendewa hovyo.
Huyo alikuwa ni Twaha Jenerali Ulimwengu akituasa katika makala yake ndani ya Gazeti la Raia Mwema la Septemba1, 2010 kabla ya uchaguzi. Alituasa kuwa tukichagua hovyo na halafu tukajikuta tunaanza kutendewa hovyo, tusiseme hovyo.

Watanzania kama kawaida yetu tulipuuzia ushauri wake na tukamrudisha madarakani Rais yuleyule, chama kilekile, mafisadi walewale na sasa tunaanza kuonja machungu yale yale ! Kwa kifupi tulichagua hovyo na hivyo tunaendelea kutendewa hovyo, je tukae kimya ?

Ndani ya mwezi moja tayari lile zimwi lisilo na sura tulilokuwa tunapambana nalo ghafla limefufuka na safari hii limeingia kwa staili mpya na ya kutisha. Majeraha tuliyompa yalimfanya akimbilie Ulaya kwa matibabu na sasa kapona na karudi kwa ari na nguvu zaidi.

Hata hivyo linaloogopesha zaidi ni kuwa hii ya Dowans ni rasharasha tu, dhoruba yenyewe ya miaka mitano inatusubiri. Katika hii awamu ya pili, tutashuhudia ambayo yataifanya awamu ya kwanza ionekane kama vile tulikuwa peponi - si tumechagua wenyewe ?
 
Watanzania tuliowengi tulichagua vizuri ila watendaji wa serikali wasio na maadili kama wa NEC na UWT ndio waliotuangusha kwa sababu ya maslahi binafsi. hawakuwa na uzalendo walituuza. Lakini mchuma janga hula na wa kwao, hivyo athari za matendo yao zitawatafuna hata wao na ndugu zao.
 
“Tunachagua kama vipofu, kisha tunalalama kama vichaa. Tuamue, ama tuchague viongozi wetu kwa makini, au tukae kimya wakati wakitunyanyasa. Wachagua ovyo wasiwe wasema ovyo wakitendewa ovyo." - Jenerali Ulimwengu
 
Ulimwengu anasahau hakuna aliyewachagua hao viongozi, na hatuwezi kukaa kimya wakitunyanyasa kwasababu hatukuwachagua sisi, 2020 hapakuwepo na uchaguzi ulikuwepo uchafuzi.
 
“Tunachagua kama vipofu, kisha tunalalama kama vichaa. Tuamue, ama tuchague viongozi wetu kwa makini, au tukae kimya wakati wakitunyanyasa. Wachagua ovyo wasiwe wasema ovyo wakitendewa ovyo." - Jenerali Ulimwengu
Nyumba ni msingi na uongozi ni uchaguzi.
 
Back
Top Bottom