Tuache siasa za Umeme. Je, TANESCO iwafurahishe wanyonge na kuua Viwanda?

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Wanabodi, Viwanda vyetu vikifanya kazi kwa uhakika umeme wetu hautoshi kabisa, Umeme wetu unatosheleza matumizi ya nyumbani tu hapa Tanzania.

Kwa sasa huu umeme kidogo tunagombania matumizi ya nyumbani na Viwandani, Aidha tugawane kidogo kidogo au kukata viwandani na kuacha majumbani, Au tuendelee na ukarabati na kufufua nguvu ya gesi ili tuwe na umeme wa uhakika.

Wakati wa JPM umeme ulikatwa viwandani kwa makusudi ili Raia wanyonge wasiozalisha kitu washangilie na kufurahia huku uchumi ukielekea ukingoni kutoka ukuaji wa asilimia 7% mwaka 2014 mpaka asilimia 4%mwaka 2020.

Leo hii mwaka 2022 mapato ya Tanesco yameongezeka sana hasa kutoka kwa watumiaji wakubwa, Viwanda vina lipa bili inayotakiwa ya umeme kwani wanapelekewa umeme wa uhakika, Kuna viwanda sasa vinalipa kwa mwezi Bilioni mbili za matumizi ya umeme baada ya Mama Samia na January Makamba kuruhusu ukarabati wa mitambo, Hapo awali umeme ulikatwa hovyo viwandani na kusababisha uchumi wa awamu ya tano kuwa hoe hae yaani chakali kwa uzalishaji hafifu

Hakuna mitambo iliyokuwa chakavu kama ya Tanesco, Kuna maeneo umeme ulikuwa unawaka lakini miundombinu yake imeoza kabisa hasa nguzo za umeme, Unaangalia na kujiuliza huu mtaa siku nguzo za umeme zilizooza zikidondoka usiku itakuaje kwa Raia wa maeneo hayo?

Suluhisho letu la umeme lilikuwa ni Kuongeza nguvu umeme wa gesi mwaka 2014 mpaka 2020, Lakini ukabila, chuki na sifa Taifa liliingia hasara la kujenga bomba la gesi, kulipa watu wa Lindi na Mtwara maeneo halafu mtu mmoja akazuia mpango wa Taifa wa umeme wa gesi

Haukufanyika ukarabati wowote kwa miaka mitano yaani 2015 mpaka 2020 kwenye mitambo ya umeme kufurahisha wanyonge na kuhadaa wananchi, Kulikuwa na Tear and wear ya kutosha, Kama uchumi ulivyokuwa unakufa kufurahisha wanyonge ndivyo ilivyo mitambo ya umeme ilikuwa inakufa kufurahisha wanyonge wapate mwanga wa umeme huku viwanda vikipunguza wafanyakazi wake kimya kimya

Hakuna nchi iliyoendelea bila kuwa na Fedha za kigeni ambazo zinapatikana kwa utalii au uzalishaji Mali yaani viwandani ambako umeme ulikatwa hovyo kwa miaka mitano iliyopita ya awamu ya tano kukomesha matajiri

Kwenye utalii huko Ngorongoro bado tunataka tena kufurahisha wanyonge, Tutafurahisha watu wa Ngorongoro wanyonge kwa gharama ya kuharibu utalii na uhifadhi wa Taifa zima hivyo kukosa pesa za kigeni, Kuna siku tena tutakuja hapa kulalamika kwanini Ngorongoro hakuna watalii na wanyama wakati tunataka kufurahisha wanyonge

Nini kifanyike kuondoa tatizo la umeme Tanzania

Mosi, Mpango wa gesi ndio suluhisho mambo ya kutegemea mvua zitanyesha lini yamepitwa na wakati, Tulipoishia kwenye gesi ndio tuendeleze

Pili, Turuhusu kipindi cha mpito cha ukarabati wa nguzo za umeme unaendelea kwa kutoa nguzo za miti na kuweka nguzo za sasa zenye hadhi ya kimataifa maeneo mengi zoezi linaendelea

Tatu,Katiba ni muhimu sana sana. Kutoruhusu masuala ya kitaifa kurekebishwa na kila Rais aingiapo madarakani, Mipango ya Taifa isiingiliwe na nguvu ya Urais kuanza kurekebisha mambo wakati yalipitishwa na Bunge zima mfano mpango wa gesi Mtwara na mpango wa bandari ya Bagamoyo

Matumizi ya vyanzo mbadala vinavyotunza mazingira kama Solar system za kisasa na umeme wa upepo, Kodi ipunguzwe kwenye vifaa vya umeme mbadala kama Solar system na kuelimisha wananchi matumizi sahihi ya solar system

Kelele zote hizi Leo ni kutokana na mtu mmoja kuamua kufurahisha wanyonge kwa gharama ya kuliangamiza Taifa, Maamuzi kama ya kukwapua kodi kinguvu ilikuwa kufurahisha wanyonge huku ajira na uchumi ukijifia

Kelele zote hizi za umeme ni kutokana na wanyonge wasiozalisha kuwashiwa umeme mdogo tuliokuwa nao wote wao huku Uchumi wa viwanda ukikosa umeme na kujifia taratibu na kusababisha mfumuko wa bei wa bidhaa kwenda juu

Kumbuka umeme tulionao Tanzania kwa sasa unatosheleza matumizi ya nyumbani tu, Vikiongezeka viwanda vya magari hata kimoja tu, Huu umeme hautoshi mahitaji ndio maana watu walianzisha miradi wa gesi Kuongeza umeme viwandani

Wakati watu wanaambiwa Serikali ya awamu ya tano imekopa zaidi walikuwa wabishi sana kwani zilitumika Propaganda kuwafurahisha wanyonge kuwa ni pesa za ndani kumbe ni mikopo ya gharama kubwa

Hakuna siri tena, Awamu ya tano uzalishaji Mali ulishuka sana viwandani kutokana na gharama za uzalishaji mfano mzuri Dangote alilalamika fitina za Tanesco watu hawakumuelewa wakati ule, Sasa wameelewa kuwa viwandani umeme ulikuwa unakatwa ili wanyonge tupate mwanga wa kutosha kwa gharama za kuua uchumi na ajira

Propaganda hazina msaada kwenye mambo ya msingi kama umeme wetu huu ni kidogo sana, Kikwete JM hakuwa mjinga kuanzisha miradi ya umeme wa Gesi na kuachana na kutegemea mvua ambazo kwa sasa hazieleweki kwa mabadiliko ya tabia nchi

Ninaunga mkono kipindi cha mpito cha kuweka tatizo la umeme sawa hasa kwa Kuongeza nguvu ya uzalishaji toka kwenye gesi ili viwanda vipate umeme wa uhakika
 
Aiseee, kwa kweli Lowasa aliposema Elimu, Elimu, Elimu, alikuwa na maana kubwa sana! Tatizo la umeme lishughulikiwe Magufuli alishafariki. Hizi propaganda hazitisaidia kuondoa ukweli kwamba kuna ombwe katika suala la umeme, na tunachezewa na wapigaji, wakiwemo waliyokutuma. Kataa kuwa dekio la Wapigaji. Usisimame na watu, simama na Tanzania
 
Pia uzalishaji wa umeme Tanzania nzima (installed capacity) ni mdogo kulinganisha na mahitaji ya umeme Tanzania nzima tokea uhuru mpaka sasa hili halijawahi kubadilika.

Siwezi kushangaa juu ya viwanda kukatiwa umeme wakati wa awamu ya 5 ili kudanganya wananchi kuwa umeme unatosha, maana kila mtu anajua kuwa ilikuwa ni serikali ya Propaganda, uongo na ubabe. Hivyo lolote linawezekana.
 
Ukweli hakuna umeme na mgawo umeongezeka sana , sasa sijui unataka tuone hayo ni mafanikio ? umetumwa na nani?
Sasa kwa akili zako unataka waendelee kukata umeme viwandani

Yale maigizo yenu eti ohooo kwanini sukari na cement zimepanda bei? Mnamtuma Sabaya na Makonda wanajifanya wanakagua viwandani kwenye Cement na Madukani wakati Ukweli Tanesco walikuwa wanakata umeme viwandani na Kuongeza gharama za uzalishaji kwa kusababisha bei kupanda

Kiongozi uwe unatumia akili zako binafsi kufikiria mambo kwa upana wake

Jaribu kuwa mtu mzima, Anza kufanya analysis, Usisubiri kusaidiwa kufikiri


Unaleta aibu hapa JF, Umeambiwa umeme wetu kikawaida unatosha matumizi ya nyumbani tu, Na huo ndio ukweli

Sasa wewe unaongea ongea mambo ambayo yanasikitisha sana

Tumia akili kiongozi, Umeme uliopo ukitumika kwa haki viwandani na majumbani hautoshi
 
Aiseee, kwa kweli Lowasa aliposema Elimu, Elimu, Elimu, alikuwa na maana kubwa sana! Tatizo la umeme lishughulikiwe Magufuli alishafariki. Hizi propaganda hazitisaidia kuondoa ukweli kwamba kuna ombwe katika suala la umeme, na tunachezewa na wapigaji, wakiwemo waliyokutuma. Kataa kuwa dekio la Wapigaji. Usisimame na watu, simama na Tanzania
Tatizo Lake awamu ya tano mlikaririshwa mambo

Kila tajiri ni mpigaji hivyo Umaskini ndio sifa na kuitwa wanyonge, Kumbuka Wengine Mali ni za urithi

Kila mzungu ni Beberu wakati unaomba misaada na mikopo kwa siri kubwa

Tangu lini wewe ukatumia pesa za ndani kujenga Bwawa la umeme?
 
sio jukumu langu kukuelimisha..

Huna takwimu unataka kuleta uongo wako hapa.

Kwa kukusaidia tu ni kwamba technically haiwezekani uzalishe 1600 MW halafu utumie 1200 MW. Unless uwe unastore hiyo ziada somewhere ( Mechanical, Electrochemical storage e.g Battery, Flywheel etc).

.. laiti ungekuwa umesoma/umeelewa Physics ya angalau Form 2.

Kwa kifupi huna ulijualo..
 
Huna takwimu unataka kuleta uongo wako hapa..
Kwa kukusaidia tu ni kwamba technically haiwezekani uzalishe 1600 MW halafu utumie 1200 MW.
.. laiti ungekuwa umesoma/umeelewa Physics ya angalau Form 2.
kubwa jinga wewe
Screenshot_20220217-051428_Chrome.jpg
 

Wewe mjinga.. umeleta figure za uzalishaji, Je unafahamu mahitaji ya umeme Tanzania kwa sasa?

Mahitaji ya umeme Tanzania si chini ya MW 2000. Sasa hiyo ziada unatoa wapi? Chato au?

Mnaleta propaganda za kijinga sana nyie MABICHWA.. So unataka kusema umeme unakatwa makusudi na waziri?

Idiots sana nyinyi.
 
Wewe mjinga.. umeleta figure za uzalishaji, Je unafahamu mahitaji ya umeme Tanzania kwa sasa?
Mahitaji ya umeme Tanzania si chini ya MW 2000 sasa hiyo ziada unatoa wapi? Chato au?
tafadhali sana usinikoti tena tafta watotowenzio muendelee kutafta kile kuanacho 'suit your ego
 
Ugoro mtupu, umeme hakuna na mgawo kila siku then wewe na pumbu zako unatuambia sasa tuna afadhari, mpuuzi sana wewe
 
hivi unajua we ni hasara kwa baba yako yani huna akili mpumbavu wewe

we ndo umeleta hoja ya mahitaji af unanilazimisha mie nkupe data? unaakili wewe? unajielewa kweli?

Wewe si ndio umesema mahitaji ya umeme Tanzania ni 1200 MW mpaka 1300 MW. Lete hizo figure?

Unatunga uongo ili iweje?

Kwa taarifa yako mahitaji ya umeme Tanzania nzima hayapungui 2000 MW na yanaongezeka kila siku sababu umeme unaendelea kusambazwa vijijini.

Umeelewa wewe Fool? Au nirudie tena somo?
 
Awamu ya JPM ilikuwa awamu ya hovyo kabisa katika historia ya nchi hii, yaani takataka kabisa
 
Kwa taarifa yako mahitaji ya umeme Tanzania nzima hayapungui 2000 MW na yanaongezeka kila siku sababu umeme unaendelea kusambazwa vijijini.
Unathibitishaje hiyo 2000 MW? Hujaweka figure kama unavyowaambia wengine waweke, mimi mtazamaji nakuwa sielewi!

Mwisho wa siku, mada iko kisiasa zaidi na muendelezo wa chuki, kueneza hearsays ili watu wajiandae kisaikolojia bila wa kujua, tunapigwa pakubwa muda si mrefu!

Ukijisumbua kidogo tu ukaendea kwa hao wa Viwanda, hasa vile ambavyo uzalishaji wao bila umeme wa uhakika, mali inaoza, awataki umeme wa Tanesco.

Kipindi cha Jiwe, Tanesco wamepeleka Dedicated line kwenye viwanda ili kuwashawishi watumie umeme wa Tanesco tu, imeshindikana! Sheria ikawekwa, kuzalisha umeme wako mwenyewe ni lazima uombe vibali mia kidogo, wameomba.

Sasa wekeni facts zenu vizuri kwanza....kisha uweke figure hapa ni jinsi gani watumiaji wa vijijini wanaweza kupandisha matumizi ya umeme kwa kiwangi kikubwa hivyo!
 
Back
Top Bottom