Nataka kusema kitu, bado nakifikiria,
Nifikiri mara tatu, kisha nitawaambia,
Ninachotaka kusema.
Nimepatwa na ufyatu, mambo yamenizidia,
Msiotwe roho kutu, mwapaswa nisaidia,
Kuna kitu ntasema.
Miaka makumi tatu, mie naikaribia,
Nami kati yao watu, heshima naitakia,
Mwaelewa nachosema?
Na huu siyo upatu, nikaukurupukia,
Nitawashangaza watu, ovyo kujiamulia,
Niendelee kusema?
Moyo wangu siyo butu, pekee kujikalia,
Nao wahitaji kitu, kesho nitawaambia,
Basi kesho ntasema.
Au Niseme Leo ? Umefahamu nitakacho ?