Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Hotuba ya msomi nguli wa sheria imetuacha na maswali mengi hasa mbona anaelekea ana khofu ya kushindwa uchaguzi wa ubunge 2025?
Katika hotuba yake ya leo tumejifunza mambo mengi yakiwemo ufahamu wake wa sheria unatuacha hoi bin taabani.
Kwanza kapendekeza wawekezaji watafutwe na kuongezwa bandari ya Dar-es-Salaam ikimaanisha hata mkataba wa DP World hajausoma na hata kama aliusoma hajauelewa
Mkataba wa DP World umeipa kampuni tajwa uendeshaji wa hiyo bandari ya Dar-es-Salaam bila kuingiliwa na yeyote yule sasa wawekezaji zaidi wa bandari ya Dar-es-Salaam wapi na wapi?
Pili, kaongea kwa niaba ya wana Mbeya lakini hakutueleza ni lini na wapi maana wanambeya wengi wanasema hajawahi hata kukutana nao kwahiyo aache uongo na amwogope Mwenyezi Mungu.
Tatu, taswira yake ilikuwa ya ghadhabu na shari ikiashiria kuna alama za nyakati kesha zisoma hususani za matumizi ya maneno ya ."...... kuna maneno mengi yamepita hapa Mbeya...."
Maneno yapi yamepita Mbeya zaidi ya wapigakura kukujadili utendaji wako mbovu bungeni?
Na ya kuwa, tayari wamepata msitiri anaitwa Msomi Boniface Mwabukusu ambaye sasa ni Mbunge Mtarajiwa wa Mbeya mjini?
Kwa khali tunayoiona huyu mama anaweza kupata kiharusi wakati wowote ule maana hii tafurani siyo ya bure ina jambo linakuja bado lipo jikoni.
Katika hotuba yake ya leo tumejifunza mambo mengi yakiwemo ufahamu wake wa sheria unatuacha hoi bin taabani.
Kwanza kapendekeza wawekezaji watafutwe na kuongezwa bandari ya Dar-es-Salaam ikimaanisha hata mkataba wa DP World hajausoma na hata kama aliusoma hajauelewa
Mkataba wa DP World umeipa kampuni tajwa uendeshaji wa hiyo bandari ya Dar-es-Salaam bila kuingiliwa na yeyote yule sasa wawekezaji zaidi wa bandari ya Dar-es-Salaam wapi na wapi?
Pili, kaongea kwa niaba ya wana Mbeya lakini hakutueleza ni lini na wapi maana wanambeya wengi wanasema hajawahi hata kukutana nao kwahiyo aache uongo na amwogope Mwenyezi Mungu.
Tatu, taswira yake ilikuwa ya ghadhabu na shari ikiashiria kuna alama za nyakati kesha zisoma hususani za matumizi ya maneno ya ."...... kuna maneno mengi yamepita hapa Mbeya...."
Maneno yapi yamepita Mbeya zaidi ya wapigakura kukujadili utendaji wako mbovu bungeni?
Na ya kuwa, tayari wamepata msitiri anaitwa Msomi Boniface Mwabukusu ambaye sasa ni Mbunge Mtarajiwa wa Mbeya mjini?
Kwa khali tunayoiona huyu mama anaweza kupata kiharusi wakati wowote ule maana hii tafurani siyo ya bure ina jambo linakuja bado lipo jikoni.