Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,468
- 23,744
Nakumbuka tukio hili kama vile ni jana. Ilikuwa miaka ya 80s nimeenda Mkoani likizo kumtembelea bibi. Kulikuwa na tabia za kibabe sana hiyo sehemu.
Bahati mbaya mimi nlikuwa mweupe, mnene naonekana kama mayai mayai sana wakataka kuwa wananionea sana mpirani.
Siku ya tukio nilienda kucheza nikiwa na mpira wangu wa kujazwa na pump ya baiskeli. Gozi. Ilikuwa nadra sana miaka hiyo kuwa na gozi lile la mabaka ya white and black. Mzee aliniletea toka UK alipokuwa masomoni.
Jamaa wakaanza rough kiasi nikawa naogopa hata kucheza mpira nikatoka nikawaacha wacheze wao kumbuka hapo mpirani mimi tu ndo nmevaa viatu. CHACHACHA.
Baadaye nikaona ni muda wa kurudi home, bibi ataanza nitafuta, mpira ulipotoka nikaufuata na kusema naondoka. Jamaa mmoja mbabe alinifuata akaupiga mpira mikononi mwangu ukaanguka. Nikamfuata akamrushia mwenzie, nilipomfuata naye akamrudishia huyu mwingine.
Nlisumbuliwa hivi kwa muda huku watu wakicheka. Alipoona wanafurahi akakimbia pembeni sehemu ya fundi fenicha akachukua kipande cha mbao na kilikuwa na msumali akautoboa mpira, nachokumbuka nliona kipande hicho hicho cha mbao na kumpiga nacho kichwani. Alipasuka na ule mshtuko akaanguka.
Nlimfuata nikamkalia juu nlimpiga ngumi nyingi usoni nikilia. Watu wengine wakaanza kimbia kwa hofu. Jamaa nadhani alipoteza fahamu maana aliangukia kisogo na hakuwa aki respond ingawa alikuwa mkubwa kwangu.
Then nilianza mburuza barabarani kutaka enda naye home kwa bibi. Watu walinishangaa maana nlikuwa napiga kelele kama mtu aliyepagawa nilimburuza mpaka sehemu moja kuna shamba nikaanza zoa mabua ya mahindi kumfunika nayo nikiomba kiberiti nimchome moto.
Maana watoto wa kule walikuwa wana tabia ya kutembea na viberiti ili jioni wakoke moto kutengeneza matanuru ya kuchomea mahindi na kuota pia.
Hapo ndio alipokuja bibi yangu anakimbia akipiga kelele na kuja nikamata huku akiongea maneno fulani ya kilugha akaja nishika kichwa na kifua, aliongea kama dakika kadhaa nikatulia.
Bibi alinishika mkono kunirudisha home. Akakimbia jirani kumwita mama wa yule kijana. Mimi niliwekwa chini ya ulinzi wa Baba Mdogo pale home nikiwa nimefungiwa chumbani.
Yule bwana alipelekwa Hospital na sikutoka kwenda nje kwa muda wa week moja mpaka alipokuja nichukua mzee kunirudisha Dar. Mpaka leo huwa nakumbuka hicho kitendo.
Baba yangu mdogo alikuja patwa na kesi ya kupiga askari wawili kisha akawa anawavuta kwenda kuwalaza shambani akawakanyage na tractor, kelele za watu zilimrudisha akili akakimbia hatukumwona tena mpaka after 15 years kumbe alitorokea nchi jirani. Bibi alipata kutuambia tulikuwa na shida flani hivyo tujiadhari sana na hasira au watu wanapotukwaza.
Kilikuwa ni kitendo cha kikatili sana nikiwa na umri mdogo sana.
Bahati mbaya mimi nlikuwa mweupe, mnene naonekana kama mayai mayai sana wakataka kuwa wananionea sana mpirani.
Siku ya tukio nilienda kucheza nikiwa na mpira wangu wa kujazwa na pump ya baiskeli. Gozi. Ilikuwa nadra sana miaka hiyo kuwa na gozi lile la mabaka ya white and black. Mzee aliniletea toka UK alipokuwa masomoni.
Jamaa wakaanza rough kiasi nikawa naogopa hata kucheza mpira nikatoka nikawaacha wacheze wao kumbuka hapo mpirani mimi tu ndo nmevaa viatu. CHACHACHA.
Baadaye nikaona ni muda wa kurudi home, bibi ataanza nitafuta, mpira ulipotoka nikaufuata na kusema naondoka. Jamaa mmoja mbabe alinifuata akaupiga mpira mikononi mwangu ukaanguka. Nikamfuata akamrushia mwenzie, nilipomfuata naye akamrudishia huyu mwingine.
Nlisumbuliwa hivi kwa muda huku watu wakicheka. Alipoona wanafurahi akakimbia pembeni sehemu ya fundi fenicha akachukua kipande cha mbao na kilikuwa na msumali akautoboa mpira, nachokumbuka nliona kipande hicho hicho cha mbao na kumpiga nacho kichwani. Alipasuka na ule mshtuko akaanguka.
Nlimfuata nikamkalia juu nlimpiga ngumi nyingi usoni nikilia. Watu wengine wakaanza kimbia kwa hofu. Jamaa nadhani alipoteza fahamu maana aliangukia kisogo na hakuwa aki respond ingawa alikuwa mkubwa kwangu.
Then nilianza mburuza barabarani kutaka enda naye home kwa bibi. Watu walinishangaa maana nlikuwa napiga kelele kama mtu aliyepagawa nilimburuza mpaka sehemu moja kuna shamba nikaanza zoa mabua ya mahindi kumfunika nayo nikiomba kiberiti nimchome moto.
Maana watoto wa kule walikuwa wana tabia ya kutembea na viberiti ili jioni wakoke moto kutengeneza matanuru ya kuchomea mahindi na kuota pia.
Hapo ndio alipokuja bibi yangu anakimbia akipiga kelele na kuja nikamata huku akiongea maneno fulani ya kilugha akaja nishika kichwa na kifua, aliongea kama dakika kadhaa nikatulia.
Bibi alinishika mkono kunirudisha home. Akakimbia jirani kumwita mama wa yule kijana. Mimi niliwekwa chini ya ulinzi wa Baba Mdogo pale home nikiwa nimefungiwa chumbani.
Yule bwana alipelekwa Hospital na sikutoka kwenda nje kwa muda wa week moja mpaka alipokuja nichukua mzee kunirudisha Dar. Mpaka leo huwa nakumbuka hicho kitendo.
Baba yangu mdogo alikuja patwa na kesi ya kupiga askari wawili kisha akawa anawavuta kwenda kuwalaza shambani akawakanyage na tractor, kelele za watu zilimrudisha akili akakimbia hatukumwona tena mpaka after 15 years kumbe alitorokea nchi jirani. Bibi alipata kutuambia tulikuwa na shida flani hivyo tujiadhari sana na hasira au watu wanapotukwaza.
Kilikuwa ni kitendo cha kikatili sana nikiwa na umri mdogo sana.