Flexi lady
JF-Expert Member
- Nov 14, 2014
- 293
- 202
Sio rahisi hivyo. Unadhani kaka angekubali mdogo wake amdhalilishe mkwewe kimasikhara hivyo, kaka mwingine anakutia mibao na kukufukuza juu. Madam S alifanya vyema kuondoka kwa hekima tu maana ni kweli pale si kwake hana maamuzi nako. Ndugu akishaoa au kuolewa kwake wewe huna maamuzi ya chochote cha msingi ni kuwaacha tu maana ubaya huwa una mwisho wake....Unasamehewa kwa sababu tu ilikuwa bado mdogo!
Huu ndio unsfiki wetu waafrika ambao tunatakiwa kuupiga vita kwa nguvu zetu zote!
Umemsikia dhahiri shemeji yako na mama yake wanakusema na kukupangia ubaya wa kukufungia mlango ili wakunyime chakula alichonunua kaka yao, halafu Wewe ndio unasusa na kukimbilia kwenu hivi hivi?
Hapo Mimi ungenipenda Comrade.
Pamoja na Udogo wangu ningeliwatokea na kuwaambia nilichosikia na mipango yao dhalimu waliyopanga kunifanyia...na kaka ningemjulisha kilichotokea mbele yao na ndio ningeomba anipe nauli nirejee home nimuache na wajinga wake roho mbaya wale!!!