Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2010
Posts
1,710
Reaction score
3,685
Miaka ya 80's mwanzoni nilipata kuishi Tabora Mjini,baadae nikaja kusoma Tabora Boys miaka ya 90's....leo nimekumbuka maisha ya Tabora,Ujio wa Baba Mtakatifu,enzi za ukuu wa Mkoa Ndugu Gama....Timu ya mpira ya Milambo chini ya akina Job Ayoub "kwasakwasa",Quresh Ufunguo,Dadi Phares,Hamad Mwinyimkuu,Abas Mchemba na Bubu fulani alikuwa na mashuti sana wengine siwakumbuki.

Matajili wa wakati huo ni matajili wa mbao wakiitwa "Digala",kuna jamaa alikuwa tajili wa mbao mitaa ya Kiyungi karibu na Filter akiitwa Fifi(sijui kama yu hai)...mitaa ya ng'ambo mtaa wa Rehani alikuwepo Mavyombo, Msabaha...! Kulikuwa na kina Said Kindamba, Waarabu wa Kwihara na Mrema wa Cheyo!...

Miaka hiyo Tabora ilisifika kwa kuwa na Majambazi hatari, wengi wakitokea mitaa ya Ng'ambo..kuna jambazi mmoja walimkata mguu ili aache kuiba akawa anatembea na gongo(nimemsahau jina), Vichaa(wehu) wa kutosha na maarufu kama Athumani Nuna, Super Tall, Aman n.k...

Mitaa ya wajanja ilikuwa National na Cheyo!! Misosi kama ugali muhogo, makopa, mawese na ngazi... Vipi nani wa Tabora anipe update za leo?muda sijafika.

Chemichemi, Gongoni, Bachu, Kanyenye, Kiloleni, Isevya, K'koo, Mwanza Road na Ipuli.... Wapi vijana wa enzi hizo wa Mboka Manyema?
 
enzi hizo mechi kati ya Tabora boyz na Milambo jamaa wa tabora boys walikuwa wakija na mikanda ya jeshi cha moto mtaka iona. Shule kama Uyui ikiongoza kwa utukutu na wanafunzi wake wengi wakishinnda nje ya madarasa, Nilikuwa pale Kazima sekondari miaka ya 90
 
dah enzi za hamisi ma mbwa, jambazi maarufu enzi zile akauwawa na aziz mwarabu, hahaa namkumbuka chizi mmoja alikuwa anaitwa mwajuma ringa, alikuwa soko kuu Tabora, ukienda disco na demu mzuri basi uwe na cha moto la sivyo utahadithia hadi wajukuu, diamond talks ndio ilikuwa jumba pekee la cinema, mh mengi ya kukumbuka Tabora ndio ya kwanza kuchoma jambazi alikuwa anaitwa athumani la wizi kabouru kundi lao liliitwa black scorpion
 
Simbamwene tulikuwa tunaenda kuangua zambalau na embe boribo juu ya makaburi...vp umekuwa mji?ha ha ha ha ha ha umenikumbusha Mwajuma Ringa?ivi kwanini Mboka Manyema vichaa wengi?...dah Hamis Mambwa aliogopwaje?Diamond near by TMP uwanja wa Chipukizi?ukumbi wa Disco hapo Mwanaisungu geti la kuingia Uhazili...video tunangalizia Maua Bar Opposite na Central Police
 
New session ya Video za mauaji na Uchochezi, kutoka video tutahamia kwenye Skype live!
 
Kwenye vichaa hapo umemsahau makamba jeki bana!........jamaa mmoja alikua kibarua maarufu tunamuita fulu saba......anapeleka pwani huyoooo!!!!nakumbuka nikiwa 'kinda' tu mwanajeshi mmoja aliuawa majaruba ya isevya kutokea stesheni pale.......basi 'wajeda' wakaenda zika mtu wao kimya kimya halafu wakaingia mtaani sasa.......weee....wiki nzima msako,waliokuwa watuhumiwa wa hata udokozi miaka ile walikufa vibaya kwa singe na vipigo vya washkaji,vilio vikatawala mji mzima na amani ya hata kulala mlango wazi ikarejea!

FIFI alikuwa anatuhumiwa kuwaambukiza ukimwi dada zetu kwa makusudi,one day alionekana mitaa ya kwetu na dada mmoja wa pale pale mtaani kwetu anaitwa Tatu Mazegembe........alikuwa na makalio makubwa huyooo wacha.........basi wacha tumtoe nduki na mawe huku tunamwambia yule dada 'unaenda kufa wewe!!!'......aaaaa mboka matata wee.....mji wangu wa utotoni uliokataa kukua!
 
wakuu kuna anaemkumbuka Adam Gosho na mazingaombwe yake ya uongo na vijana wake wale wa Karate!!?disco la mwanaisungu opp.uhazili.........upinzani wa timu za mpira miaka ile..........timu ya posta na polisi,magereza ya uyui na rhino ya nzega gemu zinapigwa uwanja wa kumbukumbu ya vita pale,watoto wa gongoni na bange zao!kisima cha kilimbika,bwawa la Taliani(kulisemekana kulikua na 'chunusi' kule....lol!)...................wahalifu maarufu aka zile kina Mafuta ya ndege(anakimbia huyo.....hatareeee,Bolt hakamati!),Jackson kuku,sinema za ukumbi wa Diamond miaka ile.

nakumbuka tukio la mabehewa ya petroli kuwaka moto pale stesheni..kilikuwa kipindi cha vita ya ghuba,basi tukajua marekani na saddam wameanza kukinukisha na huku tayari.....lol!
 
kwenye vichaa hapo umemsahau makamba jeki bana!........jamaa mmoja alikua kibarua maarufu tunamuita fulu saba......anapeleka pwani huyoooo!!!!nakumbuka nikiwa 'kinda' tu mwanajeshi mmoja aliuawa majaruba ya isevya kutokea stesheni pale.......basi 'wajeda' wakaenda zika mtu wao kimya kimya halafu wakaingia mtaani sasa.......weee....wiki nzima msako,waliokuwa watuhumiwa wa hata udokozi miaka ile walikufa vibaya kwa singe na vipigo vya washkaji,vilio vikatawala mji mzima na amani ya hata kulala mlango wazi ikarejea!

FIFI alikuwa anatuhumiwa kuwaambukiza ukimwi dada zetu kwa makusudi,one day alionekana mitaa ya kwetu na dada mmoja wa pale pale mtaani kwetu anaitwa Tatu Mazegembe........alikuwa na makalio makubwa huyooo wacha.........basi wacha tumtoe nduki na mawe huku tunamwambia yule dada 'unaenda kufa wewe!!!'......aaaaa mboka matata wee.....mji wangu wa utotoni uliokataa kukua!

haa haaa haaa, leo napata story za long time.
Katika vichaa wa Tabora MALINGUMU ndio mkurugenzi wao.
Hajawahi kutokea mchezaji mkali wa milambo kama Feruzi Teru alikua nooma.
Hakuna mtemi kama brother Mwene.
Mwizi namba moja ni kandege wengine wanafatia
Black scorpion hili kundi lilikua balaa
Muungano mess mnacheza disco mara nyuki wanatokea watu mbio haa haa haaaaa
 
Umeshau milambo wanaume VS Tabora boys siku moja tabora boys walikimbizwa mpaka mabwenini na Milambo wanaume. Aly mayai alikuwa anasoma Uyui sec, na victor mihayo, kidau na renatus njohore walikuwa tabora boys, pia kuna mtoto wa kiarabu wa tabora boys alikuwa hatari. milambo wanaume kulikuwa na kimti, goliati, mathew, na nk.
 
haa haaa haaa, leo napata story za long time.
Katika vichaa wa Tabora MALINGUMU ndio mkurugenzi wao.
Hajawahi kutokea mchezaji mkali wa milambo kama Feruzi Teru alikua nooma.
Hakuna mtemi kama brother Mwene.
Mwizi namba moja ni kandege wengine wanafatia
Black scorpion hili kundi lilikua balaa
Muungano mess mnacheza disco mara nyuki wanatokea watu mbio haa haa haaaaa


Maika ya father malio mgurunde, the late..MBOKA YA MIAKA HIYO HUWEZI ONA MBWA STATION KAMA HAKUNA TREN YA ABILIA, WALIKUWA WANAJUA RATIBA ILI WAPATE MISOSI
 
Ha ha ha ha Dah!Mboka Manyema umenikumbusha mbali sana MALINGUMU....Tatu "Mazeghembe"!hili Zeghembe ni kama leo tunavosema "masabuli"..Mboka imegoma kbsa kupiga hatua kimaendeleo
 
Dah wakuu! Mwamkumauka Jackson Kuku? Dogo alikuwa noma mji mzima.
 
haa haaa haaa, leo napata story za long time.
Katika vichaa wa Tabora MALINGUMU ndio mkurugenzi wao.
Hajawahi kutokea mchezaji mkali wa milambo kama Feruzi Teru alikua nooma.
Hakuna mtemi kama brother Mwene.
Mwizi namba moja ni kandege wengine wanafatia
Black scorpion hili kundi lilikua balaa
Muungano mess mnacheza disco mara nyuki wanatokea watu mbio haa haa haaaaa


hahahahahahhaha.........kaka unamkumbuka kandege!!!!?................kweli we mwenyeji!

niliwahi kumsikia Ally Mayay siku moja redioni anasema tangu azaliwe.........hajawahi ona mchezaji anapiga chenga mbaya na ufundi wa hatari uwanjani kama FERUZI TELU................namuunga mkono mia mia!
namkumbuka LUcas Simwanza,Jobe Ayoub,Queresh Ufunguo,kizazi cha hatari sana cha mpira hiki!
Black Scorpion ulikuwa mtandao mbaya kabisa wa ujambazi aka zile..wakati dar komando yosso wanatamba.....namkumbuka jambazi hatari la kundi hili alikamatwa baada ya kupiga tukio shinyanga....alikua akiitwa Inno!
 
Hahahhaa hii thread nouma!! inanikumbusha life la Tabora wakuu, maeneo ya Ng'ambo kwenye pilau usiku usiku!! Tukutuku kuchota maji, kwa Sonda kucheki UEFA, hahaha nilikuwapo miaka 10 hadi 12 iliyopita wakuu pale Tabora Boys.
 
hahahahahahhaha.........kaka unamkumbuka kandege!!!!?................kweli we mwenyeji!

niliwahi kumsikia Ally Mayay siku moja redioni anasema tangu azaliwe.........hajawahi ona mchezaji anapiga chenga mbaya na ufundi wa hatari uwanjani kama FERUZI TELU................namuunga mkono mia mia!
namkumbuka LUcas Simwanza,Jobe Ayoub,Queresh Ufunguo,kizazi cha hatari sana cha mpira hiki!
Black Scorpion ulikuwa mtandao mbaya kabisa wa ujambazi aka zile..wakati dar komando yosso wanatamba.....namkumbuka jambazi hatari la kundi hili alikamatwa baada ya kupiga tukio shinyanga....alikua akiitwa Inno!

Kweli mimi mwenyeji pale lakini wewe nakupa salute, kuna watu umenitajia mwenyewe nimechoka mfano Adam gosho,Makamba jeki haa haaa haaaa...katika wachezaji usimsahau wastara bari bari. kuna mtu alikua anaitwa albanda wiii kwa kula huyu jamaa hata makamba jeki anasubiri. Ahh Uyui Sec nakumbuka Remember Member sijui kuna mtu anaijua hii humu? anyway Mnamkumbuka Amani mwehu, Roshi, Jetha haa haa haaa
Chiku kaspoti haa haaa haaaa
 
Umeshau milambo wanaume VS Tabora boys siku moja tabora boys walikimbizwa mpaka mabwenini na Milambo wanaume. Aly mayai alikuwa anasoma Uyui sec, na victor mihayo, kidau na renatus njohore walikuwa tabora boys, pia kuna mtoto wa kiarabu wa tabora boys alikuwa hatari. milambo wanaume kulikuwa na kimti, goliati, mathew, na nk.

Sisi tulikuwa pale miaka ya 1970.Ahmed Amasha ilikuwa Uyui, Mwalusako alikuwa St. Mary's yaani Milambo.Mji ulikuwa na wanajeshi wengi ambao waliongezeka wakati wa vita ya Kagera. Nakumbuka treni ya abiria ikiingia mji unakuwa na pilika pilika nyingi na movements za watu na magari zinaelekea railway station
 
Simbamwene tulikuwa tunaenda kuangua zambalau na embe boribo juu ya makaburi...vp umekuwa mji?ha ha ha ha ha ha umenikumbusha Mwajuma Ringa?ivi kwanini Mboka Manyema vichaa wengi?...dah Hamis Mambwa aliogopwaje?Diamond near by TMP uwanja wa Chipukizi?ukumbi wa Disco hapo Mwanaisungu geti la kuingia Uhazili...video tunangalizia Maua Bar Opposite na Central Police
Dah ukienda utapotea nilienda 2008 sikujua nianzie wapi ikabidi nimuulize tax driver kwa vile baba yangu maarufu sana Tabora ndio nikapelekwa
 
Back
Top Bottom