mama kubwa
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 5,417
- 8,401
Sikumbuki mwaka vizuri Ila nilikuwa darasa la 4 Kati ya 78 au 79. Ilitangazwa kuwa Vita imeisha na MASHUJAA wetu wanarudi nyumbani.
Tulienda kuwapungia mkono stesheni wakati walipopita na treni, nakumbuka tuliimba nyimbo za kizalendo za kumsifu Baba wa Taifa hili na kumkashifu Dikteta Idd Amini Dada. Ulikuwa ni uzalendo wa kwenye damu kabisa.
Tukio moja ambalo sitalisahau kuna Shujaa (Mwanajeshi) alituona tuko kikundi watoto wa kike akatuuliza 'Nani mchumba wangu' wote tukajibu Mimi, Mimi akatupa biskuti. Biskuti zao zilikuwa za chumvi. Tulifurahi Sana maana tulikuwa tunaenda kishule hata watu binafsi walikuwa wanakuja.
Uzalendo huu natamani ungekuwepo leo. Karibuni mliobahatika kuwaenzi MASHUJAA WA Taifa hili.
Tulienda kuwapungia mkono stesheni wakati walipopita na treni, nakumbuka tuliimba nyimbo za kizalendo za kumsifu Baba wa Taifa hili na kumkashifu Dikteta Idd Amini Dada. Ulikuwa ni uzalendo wa kwenye damu kabisa.
Tukio moja ambalo sitalisahau kuna Shujaa (Mwanajeshi) alituona tuko kikundi watoto wa kike akatuuliza 'Nani mchumba wangu' wote tukajibu Mimi, Mimi akatupa biskuti. Biskuti zao zilikuwa za chumvi. Tulifurahi Sana maana tulikuwa tunaenda kishule hata watu binafsi walikuwa wanakuja.
Uzalendo huu natamani ungekuwepo leo. Karibuni mliobahatika kuwaenzi MASHUJAA WA Taifa hili.