kilinitoaga machozi hicho kitabu,hasa pale kijana anaanza ucargo alivokua akihangaika kubeba...mizambwa napenda kuli pale mwisho wa kitabu yaaaani unasoma kuanzia mwanzo ukifika mwisho unakutana na usemi huu "yana mwisho haya"
Baadhi ya Riwaya kama kufa na kupona, Njama na Kikomo.
Sikunyongwa
sasa hii riwaya inaendela au?japo kwa nimeshaona movie nyingi za aina hii lakini si mbaya na kusoma pia
Katika Mhanga wa Ikulu namkumbuka dereva tax ambaye mapema aliweza kumgundua Dickson kuwa ni njagu lakini Frank hakuamini lol, Beka amefanya vizuri sana katika riwaya hii pamoja zile zilizokuwa zikitoka magazetini hasa ya yule mdada wa chuo aliyeshuhudia na kurekodi mauaji ya kutisha (jina la kitabu limenitoka kwani ni siku zimepita tangu nikisome)
Nilikuwa sina nia ya kukitafuta.
Lakini kama bahati tu kukumbana nacho njiani.
Nikiwa Ubungo namsafirisha mtu anaenda mkoa si nikakiona, nimekinunua na kweli ni kizuri.
Kweli Beka kafanya kazi nzuri.
Now nimefika uk. wa 32 wakati mkurugenzi wa usalama wa taifa akiwa ameshauona mkanda wa video unaomuhusu Zumo. Hadithi ni nzuri sana.