Tukubaliane, hatuna wimbo wa Taifa

Tukubaliane, hatuna wimbo wa Taifa

Binafsi sina tatizo na mleta mada pamoja na historia aliyotoa lakini kwa sababu alikuwa na lengo la kutoa darasa juu ya wimbo wa taifa, alichopaswa pia ni kueleza hata kidogo namna tulivyocopy wimbo huo na ni nani alihusika kufanya hivyo lakini pia ni kwanini tuliamua kutumia wimbo huo. Na ni vipi nchi karibu tano zote zikopy wimbo huu? Habari za hati miliki zimekaa vipi katika hili?
Hard copy ya nyembo zote tano ni za Bi. MALKIA wa UENGERZA (ex wakiloni) God save the queen !!
 
1) SA wamekuwa na wimbo wao hata kabla ya mwaka 1994, huo wimbo ni tofauti kabisa na wimbo wa "sasa Nkosi sekelel", so SA tu hata bongo kabla ya uhuru kulikuwa na song tofauti kabisa sijui mungu msaidie malkia kama sikosei, then likapigwa chini.
2) Kuna vitu watu wengi wanachanganya, tune ya nkosi sekelel origin yake ni mwanamziki Joseph parry wa wales ikaja ikawa adopted na sontonga wa SA Enzi za 1897, baadae Tanzania wakaandaa wimbo kwa maneno yetu ya Kiswahili lakini kwa kutumia ile tune, hadi mwaka 1961 siku ya uhuru tukatumia wimbo wa mungu ibariki tukaondoa wimbo wa wakoloni, hivyo ukazidi kuchochea kasi ya mapambano ya kuondoa ukoloni Africa, hivyo mungu ibariki tune ikawa imeingia hadi nchi za Zambia/Zimbabwe wakitumia same tune but different words kulingana na makabila /lugha zao, so baada ya mwaka 1994 SA kapata uhuru nao pia wakapiga chini wimbo wao wa kikoloni na ndo wakaja na nkosi ambao haukuwa wimbo officially wa taifa, so walichofanya ni kutumia same nkosi tune na ku add maneno.
3) Kila nchi Kabla ya ukoloni kulikuwa na jeshi /police kila kitu, swali hapa je jeshi au police lilikuwa lina serve under for which interest? jeshi lilikuwa na lina serve black or white interests? kama lilikuwa lina serve under black interest je kulikuwa na sababu ya nchi za kusini kuomba hifadhi TZ? wanajeshi wengi ( weusi) wa SA walio fanikisha shughuli nyingi za uhuru SA walipata mafunzo Tz, Libya ,Nigeria na Zambia, ndo hao wakaja kuunda jeshi jipya baada ya mandela kuingia madarakani.
Ahsante kwa ufafanuzi.
 
SA Africa baada ya kupata uhuru chini ya mandela alikuwa hana uzoefu, kuna maafisa wa Tz waliopelekwa na serikali ya Tz kwa ajili ya maandalizi ya mandela kuchukua nchi, hata kutoa muongozo kwa mandela hata baada ya kuwa raisi. Baadhi ya vitu ambavyo walivifanya ni pamoja na kutoa mafunzo ya maandalizi ya siku ya kuapishwa kwa raisi mandela, kujifunza nyimbo zao za Taifa, bendera, bendi ,kutoa mafunzo ya awali kwa police/jeshi, gwaride na nk, mfano wimbo wa Taifa la Tanzania ulitolewa kwao ili waweze ku update , ili wapate wimbo wao wa SA, kilichofanyika wao SA badala ya ku update wakachukua kama ulivyo wakauweka katika lugha yao na kuimba kama ulivyo. Kwa nini huu wimbo wa Tz kwa sasa chimbuko lake linaonekana limetoka SA? kwanza SA imeendelea, watu wengi wako more aware kuhusu SA kuliko Tz, pili watu wengi wako aware na zaidi kuhusu story za SA na wanafuatilia mambo mengi ya SA kuliko Tanzania. Pili SA ina uwakilishi mkubwa kimichezo zaidi ya Tanzania ( rugby, Olympic, soccer, ) na kila wanapofanya hizo activities wimbo huimbwa na kujulikana. Tanzania haikucopy wimbo huu kutoka SA maana sisi tulipata uhuru mapema na tukaandika wimbo wetu kabla yao.
Mkuu soma vizuri, wimbo ulikopiwa kutoka nyimbo ya anc.
 
Komredi, wewe na wenzio mlikuwa mmevimbewa mkaanza leta vitu visivyo na tija na lililokuwa limewakutanisha, na hilo ndio unalojaribu lileta jamvini...!
...kwamba jamhuri ya muungano haina wimbo wa taifa?..."niwie radhi, ni imani nayoipigia saluti ya kidole cha kati"
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina wimbo wa taifa period.

Mbona wagumu kuelewa?
 
Acha uongo wewe, Kwanza unaonekana history ya south Africa hujui baada ya apartheid regime kuangushwa kwenye uchaguzi hakuna Kilichobadilika majeshi ni Yale Yale, uongozi wa nchi ndio uliobadilika, kumbuka kuwa Mandela alikua na uzoefu mzuri tuu maana alishakaa kwenye transition government for 5 years, makaburu walishajua kuwa ipo siku watatoka madarakani ndio maana waliwaaanda watu weusi kuongoza nchi, kilichochelewesha Mandela na wenzake wasipewe nchi mapema ni vinu vya nyulkia ambavyo South Africa ilikua inamiliki na hivi Declerk alikua hawaamini Akina Mandela walikua allied na viongozi Kama Gaddafi etc hivo hizi silaha zingeweza kuangukia mikononi mwao hivi ilibidi vinu viharibiwe Kwanza then ndio wakaja kupewa nchi.
Kwa taarifa yako

1. Apartheid regime haijaangushwa, ila ilibadili mikakati yake ya ubaguzi. Leo hii kuna ubaguzi wa kiuchumi. Makampuni na mashirika makubwa ya makaburu ndio yanayoendesha uchumi ya Afrika ya Kusini.

2. Mandela hakuchukua nchi, bali alikabidhiwa kwa makubaliano maalumu ambayo wewe huyajui.

3. Taasisi ya kiintelijensia na ujasusi ya Afrika ya Kusini (BOSS) bado inaendeshwa na makaburu.
 
Ubaguzi wa imani na assumtion kuwa wimbo wetu unafavor din flan ndo upumbavu wa mleta uzi huu.

ujinga na upumbavu wakiimani ukimvaa mtu hujiona anaonewa kwakila jambo. kisha kuzusha yakijinga kwanjia yoyote yakifedhuri akitafuta kuungwa mkono na wapumbuvu wenzake.

Mungu ibariki TANZANIA, Dumisha uhuru na amani .....
Utakutana matusi yote, lakini Ukweli utabaki palepale. Wimbo wa taifa ni copy and paste kutoka wimbo wa anc.
 
Wewe pia unatuambia, na unataka tuamini kuwa ati hatuna wimbo wetu wa taifa.....
...kwamba ni melody ya asili ktk kusini mwa afrika ndi sababu kuwa ati hatuna wimbo wa taifa?
Kinyesi!
Tanzania Tanzania nakupenda kwa moyo wote, ndio wimbo wetu wa Taifa.
 
Kwani kuna tatizo gani kuiga kitu cha Mwafrika mwenzetu? Mbona hausemi kwamba Tanzania hatuna Sheria zetu wenyewe kwa maana zote ni British common law? Au kwa kuwa tumeiga kwa Mzungu ni sawa ila kuiga kwa Mwafrika mwenzetu unataka kupinga?
Hakuna tatizo kuiga kitu cha Mwafrika mwenzetu. Lakini ukweli ni kwamba uli-copy and paste na sio kubuni mwenye.
 
Nadhan jamaa huna uzalendo tu manake tz ndo watunzi ndo wakwanza kupata uhuru kwa mara ya kwanza uliimbwa 1961 waat south haipo kwwnye raman kabisaaaa
Soma vizuri, wakati nyie mnaiimba wimbo mwaka 1961, wenzenu walisha urekodi na hata kupata hatimiliki kabla ya mwaka 1933.
 
Na zikiimbwa nyimbo zote mbili (Mungu Ibariki Afrika; na Tanzania nakupenda kwa moyo wote), ni dhahiri kwamba huu wa pili ndio unasikika na kuhisiwa wa kizalendo kwetu. Ni wimbo wetu.
Bado nasimama na kundi linalosema Tanzania kwa maana ya Tanzania kuwa hatuna wimbo wa Taifa. Hoja za utetezi ulizozitoa zilikuwa hazina mashiko.

Je, wimbo wa taifa wa Tanganyika kabla ya Muungano na huu unaouwita wa Tanzania una tofauti zaidi ya kubadilisha neno Tanganyika na kuliita Tanzania? Ukweli ni kuwa Tanzania haina wimbo wa Taifa wala Bendera. Muziki tumeukopa kutoka Kanisa na Bendera ya Tanganyika tumeigeuza mshadhari kuifanya kuwa ya Tanzania.

Pia kulikuwa hakuna haja ya kujiona mnyonge kukitetea kitu cha ukweli ni kuhusu msimamo wa Taifa la Tanganyika kuhusu udini. Kutoa tamko kuwa Tanzania haina dini ni kuwazidi akili tu watu wenye imani tofauti kuendelea kuzubaa huku Kanisa likiendelea kujiimarisha na kujitita kila sehemu ya uamuzi nchini. Ilianza kufilisi mali za waumini dini nyengine, kukipiga marufuku East African Muslim Association, kuondololwa madarakni Iddi Amin Dadah, kufukuzwa kwa Sheikh Hassan bin Ameir wa Zanzibar asikanyage/ kuhubiri Tanganyika na mambo kama hayo
 
Watanzania inabidi tujitahidi kuwa tunafikiria mambo ya maana kuliko kutumia muda kwenye keyboard kuandika mambo ambayo hayana maana yoyote. Wimbo wa Taifa lolote ni wimbo unaobeba mashairi yanazungumzia imani au pride ya nchi husika. Kwa vile wimbo wowote uni sifa kadhaa zikiwemo mdundo, mwafaka, mkong'osio na mashairi, cha muhimu katika wimbo wa Taifa ni yale mashari yake. Mdundo, mwafaka na mkong'osio na hata mashairi yenyewe vinaweza kuwa utunzi wa mtu yeyote hata ambaye siyo raia wa Taifa husika lakini mashairi yakawa yanalenga taifa husika.

Mtemi Milambo wa Tabora naye alikuwa na wimbo wake ukiitwa "oohh" chuma chabela mitwe", baadaye wimbo huu ulichukuliwa kuwa wimbo wa TANU "Oooh TANU yajenga nchi" na pia ukawa adopted kuwa wimbo wa KANU ya Kenya kuwa "Oooh KANU yajenga nchi" It is just a song, what matters are the lyrics.
Tunes na lyrics ni moja ya misingi ya hatimiliki.

Sasa ukakopi tunes na kubadilisha lyrics kwa lugha ya Kikwenu, utakuwa bado umekopi kazi ya watu.

Ukweli upo pale pale. Wimbo ulikopiwa kutoka wimbo wa chama cha anc cha Afrika ya Kusini.
 
Hakuna tatizo kuiga kitu cha Mwafrika mwenzetu. Lakini ukweli ni kwamba uli-copy and paste na sio kubuni mwenye.


Tatizo liko wapi? Mbona kwa Wazungu tume copy paste mpaka majina yetu hamlalamiki? Hata uwezekano wa wewe kuwa na jina la Kizungu ni mkubwa kama uwezekano wa kuona jua Dar kesho?

Sasa kwa nini hapo hamlalamiki ije kuwa ishu sisi kukopi kazi ya Mwafrika mwenzetu?
 
SA Africa baada ya kupata uhuru chini ya mandela alikuwa hana uzoefu, kuna maafisa wa Tz waliopelekwa na serikali ya Tz kwa ajili ya maandalizi ya mandela kuchukua nchi, hata kutoa muongozo kwa mandela hata baada ya kuwa raisi. Baadhi ya vitu ambavyo walivifanya ni pamoja na kutoa mafunzo ya maandalizi ya siku ya kuapishwa kwa raisi mandela, kujifunza nyimbo zao za Taifa, bendera, bendi ,kutoa mafunzo ya awali kwa police/jeshi, gwaride na nk, mfano wimbo wa Taifa la Tanzania ulitolewa kwao ili waweze ku update , ili wapate wimbo wao wa SA, kilichofanyika wao SA badala ya ku update wakachukua kama ulivyo wakauweka katika lugha yao na kuimba kama ulivyo. Kwa nini huu wimbo wa Tz kwa sasa chimbuko lake linaonekana limetoka SA? kwanza SA imeendelea, watu wengi wako more aware kuhusu SA kuliko Tz, pili watu wengi wako aware na zaidi kuhusu story za SA na wanafuatilia mambo mengi ya SA kuliko Tanzania. Pili SA ina uwakilishi mkubwa kimichezo zaidi ya Tanzania ( rugby, Olympic, soccer, ) na kila wanapofanya hizo activities wimbo huimbwa na kujulikana. Tanzania haikucopy wimbo huu kutoka SA maana sisi tulipata uhuru mapema na tukaandika wimbo wetu kabla yao.
Kuna shida hapa. Yaani unataka kutuambia kuwa, wimbo huu South Africa wameanza kuutumia baada ya Mandela kuwa Rais? Hata hili la Mandela kupewa mafunzo na Watanzania nalo linafaa kupelekwa chit chat
 
dah! maandishi yote kumbe ni uwongo...bado nusu ningemwamini mtoa mada, kumbe uwongo!
aiseeeeeeeee kunakaukweli ndani yake acha kubisha bisha usichokijua
 
Back
Top Bottom