Nilisoma shule ya kijijini sana kiasi kwamba kuvaa nguo yeyote haikua tatizo, uniform ilikua ni anasa, viatu ukivaa unaonekana kama mtoto wa Trump.
Nikajikusanyia masalia ya mahindi kwenye mashamba ya watu baada ya kuvuna, nikauza. Nikaenda kununua viwalo, kaptula nyeusi, shati la blue, mkanda na kandambili (Malapa).
Kesho yake kwa kutaka kuzoa ujiko nikapiga pamba zangu kwenda darasani, Baba alikua mwalimu mkuu na tayari alikua darasani anafundisha, alivyoniona tu mlangoni, nilichezea ngumi, mateke, bakora mithili ya mbwa mwizi. Kosa la kwanza nimechelewa kuja darasani, Pili na baya zaidi, sijavaa uniform kwa makusudi, nilipigwa balaa.
Baada ya hapo akanichagua kusoma paragraph alikua anatufundisha kiingereza (English), nikisoma na zile hasira, najikuta nalia nashindwa kusoma, ananishushia dozi havy, nilinyamaza na kujitahidi kumalizia kusoma.