MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,975
Ninadhani hakuna kitengo kilidhoofika sana kwa sasa ndani ya CHADEMA zaidi ya kitengo cha Ulinzi na Usalama.
Kitengo cha Ulinzi na Usalama kilichokuwa kinaongozwa na Wilfred Lwakatare ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Bukoba Mjini kabla ya ujio wa Edward Lowassa na genge lake kilikuwa proactive katika kugundua hujuma kabla hazijafanyika na kuhakikisha unakuwepo usalama ndani ya CHADEMA.
Ninakumbuka hata Mzee Slaa aliwahi kusema waliweza kuzijua hujuma na siri nyingi kwa sababu baadhi ya watu na waajiriwa wa taasisi ya usalama wa Taifa walikuwa wanawaamini na kuwapa siri mbali mbali.
Baada ya ujio wa Lowassa baadhi ya watu nadhani waliamini kuwa Ulinzi na Usalama ndani ya CHADEMA ungeimarika zaidi hasa baada ya Mtaalam wa masuala ya Ulinzi na Usalama ajulikanaye kwa jina la Matson chizi ambaye ni rafiki wa karibu wa Lowassa kujiunga pia CHADEMA akitokea CCM.
Kilichotokea ni kinyume kwa sasa ambapo hoja hii imesadifiwa hasa baada ya Wilfred Lwakatare kuondoka katika nafasi hiyo ya Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama. CHADEMA ya sasa ni dhoofu na reactive kwenye masuala ya hujuma, ulinzi na Usalama.
Katiba ya CHADEMA Toleo la 2016 katika Ibara ya 7.7.5 inasema, ‘’Kutakuwa na mfumo wa ulinzi na usalama wa mali, viongozi na maslahi ya chama utakaotambulika kama Brigedi Nyekundu (Red Brigade)’’. Majukumu ya msingi ya Brigedi Nyekundu (Red Brigade) ni kujishughulisha na usalama ndani ya chama kwa maana ya kulinda viongozi wa chama na idara mbalimbali, mali za chama na rasilimali za chama. Pia kulinda maslahi ya chama ili kisije kuhujumiwa.
Tukio la Mbunge Mwita Waitara kujiunga na CCM ambalo limewafanya viongozi wa juu wa CHADEMA na wanazi wao kupigwa butwaa limeendelea kudhihirisha CHADEMA ya sasa imedhoofika sana katika kitengo cha Ulinzi na Usalama. CHADEMA ya sasa haijui hata kinachoendelea ndani na nje ya chama.
Baada ya Mbunge Waitara kujivua uanachama wa CHADEMA niliwaona viongozi wa CHADEMA Dar es Salaam wakiita waandishi wa habari na kusema CHADEMA ilikuwa mbioni kumfukuza uanachama kwa sababu hata barua ya kumuonya walikuwa wamemwandikia na kilichokuwa kimebaki ni kumfukuza wakati wowote. Ukiwangalia kwa makini kwa kutumia body language utagundua kuwa walichokuwa wanakiongea sicho.
Kinachochekesha zaidi, of all people, eti Dk. Milton Makongoro Mahanga ndio alijitokeza kama msemaji wa CHADEMA na kudai kuwa Mwita Waitara alikuwa mzigo ndani ya CHADEMA na kwa sababu walikuwa mbioni kumfukuza. Mahanga ambaye alikuwa mzigo mzito ndani ya CCM kwa sasa anaweza kusimama kwa ruhusa ya CHADEMA na kusema watu kama Waitara eti ni mizigo! Hii ndio CHADEMA MPYA!
Tukio la Mwita Waitara linanifanya nikumbuke maneno ya Mzee Slaa alipowauliza viongozi wa CHADEMA, ‘’Lowassa anakuja kama mtaji au mzigo, yaani kwa lugha ya kiingeza ni asset au liability’’?
Kwa hali jinsi ilivyo ndani ya CHADEMA, Mbunge Waitara hatakuwa wa mwisho kujivua uanachama bila kitengo cha Ulinzi na Usalama kuwa na taarifa mapema.
Kitengo cha Ulinzi na Usalama kilichokuwa kinaongozwa na Wilfred Lwakatare ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Bukoba Mjini kabla ya ujio wa Edward Lowassa na genge lake kilikuwa proactive katika kugundua hujuma kabla hazijafanyika na kuhakikisha unakuwepo usalama ndani ya CHADEMA.
Ninakumbuka hata Mzee Slaa aliwahi kusema waliweza kuzijua hujuma na siri nyingi kwa sababu baadhi ya watu na waajiriwa wa taasisi ya usalama wa Taifa walikuwa wanawaamini na kuwapa siri mbali mbali.
Baada ya ujio wa Lowassa baadhi ya watu nadhani waliamini kuwa Ulinzi na Usalama ndani ya CHADEMA ungeimarika zaidi hasa baada ya Mtaalam wa masuala ya Ulinzi na Usalama ajulikanaye kwa jina la Matson chizi ambaye ni rafiki wa karibu wa Lowassa kujiunga pia CHADEMA akitokea CCM.
Kilichotokea ni kinyume kwa sasa ambapo hoja hii imesadifiwa hasa baada ya Wilfred Lwakatare kuondoka katika nafasi hiyo ya Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama. CHADEMA ya sasa ni dhoofu na reactive kwenye masuala ya hujuma, ulinzi na Usalama.
Katiba ya CHADEMA Toleo la 2016 katika Ibara ya 7.7.5 inasema, ‘’Kutakuwa na mfumo wa ulinzi na usalama wa mali, viongozi na maslahi ya chama utakaotambulika kama Brigedi Nyekundu (Red Brigade)’’. Majukumu ya msingi ya Brigedi Nyekundu (Red Brigade) ni kujishughulisha na usalama ndani ya chama kwa maana ya kulinda viongozi wa chama na idara mbalimbali, mali za chama na rasilimali za chama. Pia kulinda maslahi ya chama ili kisije kuhujumiwa.
Tukio la Mbunge Mwita Waitara kujiunga na CCM ambalo limewafanya viongozi wa juu wa CHADEMA na wanazi wao kupigwa butwaa limeendelea kudhihirisha CHADEMA ya sasa imedhoofika sana katika kitengo cha Ulinzi na Usalama. CHADEMA ya sasa haijui hata kinachoendelea ndani na nje ya chama.
Baada ya Mbunge Waitara kujivua uanachama wa CHADEMA niliwaona viongozi wa CHADEMA Dar es Salaam wakiita waandishi wa habari na kusema CHADEMA ilikuwa mbioni kumfukuza uanachama kwa sababu hata barua ya kumuonya walikuwa wamemwandikia na kilichokuwa kimebaki ni kumfukuza wakati wowote. Ukiwangalia kwa makini kwa kutumia body language utagundua kuwa walichokuwa wanakiongea sicho.
Kinachochekesha zaidi, of all people, eti Dk. Milton Makongoro Mahanga ndio alijitokeza kama msemaji wa CHADEMA na kudai kuwa Mwita Waitara alikuwa mzigo ndani ya CHADEMA na kwa sababu walikuwa mbioni kumfukuza. Mahanga ambaye alikuwa mzigo mzito ndani ya CCM kwa sasa anaweza kusimama kwa ruhusa ya CHADEMA na kusema watu kama Waitara eti ni mizigo! Hii ndio CHADEMA MPYA!
Tukio la Mwita Waitara linanifanya nikumbuke maneno ya Mzee Slaa alipowauliza viongozi wa CHADEMA, ‘’Lowassa anakuja kama mtaji au mzigo, yaani kwa lugha ya kiingeza ni asset au liability’’?
Kwa hali jinsi ilivyo ndani ya CHADEMA, Mbunge Waitara hatakuwa wa mwisho kujivua uanachama bila kitengo cha Ulinzi na Usalama kuwa na taarifa mapema.
Last edited: