Tukio la kusikitisha Arusha leo

Tukio la kusikitisha Arusha leo

Antar bin Shaddad

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2010
Posts
202
Reaction score
102
Leo arusha kumetokea tukio la kusikitisha sana:Gari la wagonjwa (ambulance) la hospitali ya Selian inayomilikiwa na kanisa la KKKT lilikuwa linampeleka mgonjwa moja aitwaye Hamad Salim Bawazir (familia maarufu arusha) kwenda hospitali ya KCMC ya mjini Moshi baada ya mgonjwa huyo kuzidiwa sana.Mgonjwza huyo alikuwa anatumia hewa ya oksijen kutokana na matatizo ya kupumua na ndani ya gari hilo kulikuwa na mashine iliyokuwa na hewa hiyo.

Katika hali ya kushangaza gari lilipofika eneo la Kikatiti wakati wanaelekea KCMC nesi aliyeambatana na ndugu wa mgonjwa aliwatangazia kuwa oksijen imeisha hivyo inabidi warudi arusha, na mgonjwa alifariki ndani ya dakika 10.
Hapo ikazuka sokomoko la kufa mtu kati ya ndugu wa mgonjwa na mwuguzi huyo pamoja na dereva ambapo paqmoja na kuchezea kichapo ndugu waliharibu gari hilo kwa kuvunja vioo vyote.

Pia jamaa na marafiki wa familia kutoka mitaa ya katikati ya mji wa Arusha kama Bondeni na pangani waliokuwa na hasira kutokana na kitendo hicho walivamia hospitali ya Selian wakitaka kuichoma moto hadi uongozi ulipolazimika kuwaita askari wa kutuliza ghasia.

Taarifa zinadai kuwa huyo ni mgonjwa pili kuishiwa oksijen njiani na tukio kama hilo lilitokea hivi karibuni ambapo mgonjwa moja alifia eneo la Philips ndani ya gari hilo hilo.

Hospitali ya Selian pamoja na kujengwa kwa gharama kuwa sana zaidi ya shilingi bilioni 10 imeshindwa kutoa huduma yenye viwango kwa wagonjwa na imekuwa kama machinjio ya wagonjwa kutokana na uzembe wa madaktari na wauguzi na pia kukosekana kwa menejimenti ya maana.
 
Chagua CCM,
Chagua Matatizo!!
 
Chagua CCM,
Chagua Matatizo!!

Kwani selian ni ya ccm..
Si wamejifanya hawataki hospitali yetu ya mount meru, baba lao arusha...sasa angalia wamempoteza mtanzania mwenzetu...na hapo hata udini utaibuka ...
 
Jamani, kweli hili ni jambo la kusikitisha sana. Nawapa pole sana wafiwa. Hata hivyo naomba wa Tz wote tujiandae kwa mambo kama haya kwa sababu watu wengi wamepoteza uhai na wengine kupata ulemavu wa kudumu kwa sababu ya uzembe kama huu.


Lakini tatizo hili halianzii kwenye hospitali ama wahudumu wa afya. Linaanzia katika uzembe wa regulatory na supervisory systems za serikali. Kama vile serikali ilivyo na uzembe, katika idara zake zote, na hata haiwezi kusimamia wananchi na hivyo walaliswa sumu na kuathirika kwa namna nyingi tu.


Bila kuiondoa ccm madarakani, tutaendelea kuteketea ndugu zangu. Hakuna nchi iliyo na mfumo wa uongozi makini inayoweza kuruhusu wananchi wake wapate substandard na fatal services or products whether is from the Government or anybody.
 
Leo arusha kumetokea tukio la kusikitisha sana:Gari la wagonjwa (ambulance) la hospitali ya Selian inayomilikiwa na kanisa la KKKT lilikuwa linampeleka mgonjwa moja aitwaye Hamad Salim Bawazir (familia maarufu arusha) kwenda hospitali ya KCMC ya mjini Moshi baada ya mgonjwa huyo kuzidiwa sana.Mgonjwza huyo alikuwa anatumia hewa ya oksijen kutokana na matatizo ya kupumua na ndani ya gari hilo kulikuwa na mashine iliyokuwa na hewa hiyo.

Katika hali ya kushangaza gari lilipofika eneo la Kikatiti wakati wanaelekea KCMC nesi aliyeambatana na ndugu wa mgonjwa aliwatangazia kuwa oksijen imeisha hivyo inabidi warudi arusha, na mgonjwa alifariki ndani ya dakika 10.
Hapo ikazuka sokomoko la kufa mtu kati ya ndugu wa mgonjwa na mwuguzi huyo pamoja na dereva ambapo paqmoja na kuchezea kichapo ndugu waliharibu gari hilo kwa kuvunja vioo vyote.

Pia jamaa na marafiki wa familia kutoka mitaa ya katikati ya mji wa Arusha kama Bondeni na pangani waliokuwa na hasira kutokana na kitendo hicho walivamia hospitali ya Selian wakitaka kuichoma moto hadi uongozi ulipolazimika kuwaita askari wa kutuliza ghasia.

Taarifa zinadai kuwa huyo ni mgonjwa pili kuishiwa oksijen njiani na tukio kama hilo lilitokea hivi karibuni ambapo mgonjwa moja alifia eneo la Philips ndani ya gari hilo hilo.

Hospitali ya Selian pamoja na kujengwa kwa gharama kuwa sana zaidi ya shilingi bilioni 10 imeshindwa kutoa huduma yenye viwango kwa wagonjwa na imekuwa kama machinjio ya wagonjwa kutokana na uzembe wa madaktari na wauguzi na pia kukosekana kwa menejimenti ya maana.

Kitendo walichokifanya hao ndugu wa Marehemu Mgonjwa sio cha busara, wanatakiwa wajilaumu wao wenyewe kwani hivi sasa watu wenye kipato cha juu wametokea kudharau Hoaspitali na Vituo vingine vya kutolea huduma za afya vya Serikali wakijinasibisha kwamba huko hakuna huduma bora, lakini kwa uhalisia vituo vya Serikali vina vifaa na watalam ambao wangeweza kuokoa maisha ya huyo marehemu lakini fedha yao na kiherehere ndiyo vimepelekea kwa yaliyowakuta. POLENI SANA WAFIWA. Tujifunze kutokana na makosa SIO KILA KITUO CHA KUTOLEA HUDUMA CHA BINAFSI KIANATOA HUDUMA BORA wengine wanachojali ni fedha huduma baadae.
 
Hao ndugu wa marehemu ni wakuburuzwa mahakamani mara moja,kitendo cha kuishambulia ambulance si cha kiungwana napendekeza jeshi la polisi likishirikiana na nurse au dereva kwenda kuwatambua hao wahuni kwenye matanga ili hatua kali zichukuliwe,
 
Ndugu wa marehemu ni kati ya kundi kubwa la wajinga wenye kuweka lawama mbele kuliko uhalisia...
Suala la oksijeni kupungua lipo nje ya uwezo wa hao wauguzi na hata dereva wa gari husika...
Swali la kwanza walitakiwa wajiulize, iweje hapo Arusha hakuna hospitali yenye hadhi kama KCMC maana ingalikuwepo hospitali ya hadhi hiyo basi huyo marehemu pengine angelikuwa hai...
 
Sasa unataka CCM izuie kifo cha mtu hata kama ahadi imefika? basi tungeanza na Nyerere.
Kiguuuuuumuuu!!!chama cha mafisadiiiii....
Chagua magamba,chagua dili za india kwa wakubwa hata kama ni mafua.......jeikeyi hoyeeeeeeee!!!
 
Tujifunze kubadilika kifikra na kimawazo imefikia wakati wa kuchukua hatua muda wa kulaumulaumu umepita tuamke kutoka usingizini,hima kila mtu ajipange sawasawa.
 
ccm ccm ccm....
hapo ni mjini je vijijini....ccm ccm
 
Back
Top Bottom